Mugabe awe ni "trapeze artist" au jina lolote utakalopenda kumpa, kumbuka kwamba inahitaji ujasiri kutoa kauli kama hiyo kwa kiongozi wa taifa kubwa kama Amerika
Ujasiri is overrated, hata Idi Amin alikuwa jasiri lakini mpu.mbavu. Jasiri anayeua maelfu ya raia zake na kusema wazi wazi kwamba ana degree ya violence sio wa kumshangilia.
Generalities are caves for ignorance.Specificity is king.
Nimeona ukiongelea hicho kitu wamagharibi waige au waruhusu mila za kiafrika kwa lipi wanalotaka kutoka kwetu?
Kwa kuwa wanataka waafrika wafuate hayo ya kuruhusu ushoga.
na hata kama lipo viongozi wetu wameshindwa kufanya wamagharibi kujua msimamo wetu na tunanufaikaje na wao kupata hicho wanachokitaka kutoka kwetu.
Hili nimelisema hapo juu. Mahojiano ya Kikwete na Christian Amanpour yanaonesha hilo wazi. Viongozi wa Afrika wamesha give up ku negotiate mambo kama sovereigns. Kikwete anasema Waafrika watakubali haya mambo tu, ila hawawezi kukubali mara moja, itachukua muda, kwa hiyo wamagharibi wasiwe na shaka sana.
Wanachofanya ni kuhakikiha wanaendelea kupata/kunufaika zaidi na rasilimali za waafrika huku wakiendelea kutuletea mambo yao hata kama yanapingana na desturi na mila za kiafrika.
Katika hilo hata huyo Mugabe unayemsifia yumo, sasa nashangaa anasifiwa sana kwa kisa gani.
Kikwete alichekacheka alipoulizwa kuhusu ushoga licha ya kujua ukweli kwamba sio utamaduni wetu, alijua fika vitu gani anaweza kuvikosa kwa jibu lake. Mugabe tayari ana vikwazo vya kiuchumi ndio maana anaweza kuongea chochote kwa taifa lolote hasa wamagharibi, hana cha kupoteza kutoka kwao.
Kama Mugabe hana cha kupoteza ndio maana anaweza kuongea chochote kile, huwezi kusema ni jasiri.Jasiri ni yule atakaye blast licha ya kuwa na kitu cha kupoteza.
Hujaona mtu hata akiwa bwana mdogo kama ana uwezo watu wanamuogopa kumkosoa hata pale anapokosea kisa watakosa msaada wake?
Hili haliondoi ukweli kwamba Mugabe ni chinjachinja anayejisifia kwa uchinjachinja wake waziwazi.
Unafikiri ni kiongozi gani wa Afrika ambaye ameshatatua matatizo ya nchini kwake angestahili kutoa hiyo kauli ya kupinga ushoga? Kwa sababu Mugabe kwa mtazamo wako hana credibility kisa uchumi mbovu na mauaji ya wananchi wake.
Obviously hunisomi. Nimesema hapo juu kwamba mimi falsafa yangu ni "Mambo ya Ngoswe muachie Ngoswe mwenyewe". Haki ya mashoga ni sawa na haki yako kuwa muislamu, mkristo au straight.
Kwa nini unafikiri mimi naunga mkono kupinga ushoga?
Mimi ninachowalaumu viongozi wa Afrika ni kukosa negotiation skills za ku ensure reciprocity, kwamba Wamagharibi wakitaka tkubali wanayosema wao (ushoga kwa mfano) na sisi tuwape ajenda zetu kwa habari hiyo hiyo ya human rights (ukewenza kwa mfano)
Siojawahi kuunga mkono kupinga habari ya jinsi watu wazima wawili wanavyotaka kujamiiana. Hizo ni habari binafsi zinazopaswa kulindwa na ustaarabu wa faragha katika jamii yoyote ya watu wenye kujiheshimu.
Tukianza kupangiana sheria za ushoga kesho tutaanza kupanga sheria za kukataza katerero, keshokutwa sheria za kupangiana goli ngapi mwanamme anapaswa kupiga, mtondogoo tuta appoint waziri wa kukagua k za wake zetu kama zimezidi kina kilichopitishwa na serikali.
We do not want the government in people's private lives.
It has enough work already in the public sphere.
Mambo ya Ngoswe, muachie Ngoswe mwenyewe.