Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 87,489
- 151,692
Kuna mambo ambayo kusema kuwa ni la maana au sio hutegemea na jamii husika. Ukienda India kwa mfano, mwanamke kuolewa akiwa bikra ni jambo la maana sana lakini ukiwa Marekani ni kitu ambacho watu hata hawafikirii. Kwa hiyo inabidi ujifunze kuielewa jamii husika kabla ya kurukia kuamua kuwa jambo fulani ni la maana au sio.
Hapa kuna mambo mawili. Kuna suala la ushoga ambalo kwako halina maana ila kwa wengi waliosoma huu uzi lina maana. Halafu kuna suala la uchumi. Kimsingi kukubaliana au kutokubaliana na ushoga hakuna uhusiano na hiyo "super hyper inflation" (Japokuwa kuna watu wanaweza kujenga hoja kuwa kuna uhusiano, kutokana na ukweli kuwa wanaamini maadili na uchumi wa jamii husika vinahusiana). Kwa hiyo utaona kuwa suala la Mugabe kusababisha tatizo la kiuchumi halina uhusiano wowote na yeye kupinga ushoga. Kwa mtu ambaye anaamini ushoga ni kosa, hawezi kukaa kimya kwa kuwa amevurunda kwenye uchumi (hususan kama kweli anaamini hivyo na zaidi ya hivyo, kupinga kwake kunaendelea kumpa nguvu ya kisiasa). Kwa hiyo mkuu hata kama suala hili Mugabe analitumia kisiasa sio tatizo maana ndivyo jamii inavyotaka.
Nimeshakujibu hapo juu kuhusu ni kwa vipi jambo fulani linaweza kuwa la msingi au la! Tatizo kubwa naloliona ni kujaribu kutumia viwango vya wazungu kuamua lipi ni la msingi au si la msingi. Na ndiyo maana ukiangalia wengi wa wale wanaoona masuala ya mavazi na ushoga si ya msingi ni watu ambao wanaishi au wameishi ughaibuni kwa muda mrefu. Hawa hufikia mahali hufikiria kuwa maadili ya jamii zote yanatakiwa kufuata mifumo ya kiliberali (mfano mzuri ni Kiranga na Ngabu, sina hakika sana kama wewe sio "mghaibu" pia).
Mkuu kuamua kuwavimbia au kutowavimbia wachina hakuondoi umuhimu wa kukataa ushoga kama jamii inaona hivyo. Wewe ulitakaje tuachane na ushoga tukomae na wachina kwanza?
Nimeeleza ni jinsi gani Waafrika wanaweza kuhakikisha raia wao wanapata human rights zao na Wamagharibi hawaendelezi "cultural imperialism".
Hunisomi, kama unanisoma hunielewi, kama unanielewa ni mbishi tu.
Quite possibly hunisomi, hunielewi na ni mbishi tu pia!