Mie nilidhani Nyanda za Juu Kusini mkoa wenye wachawi wa wazi ni Njombe kwa kuwa nina ushahidi wa watu waliologwa hadharani. mfano wa kwanza kuna ndugu yangu anafanya kazi huko Njombe, Lupembe, Havanga, Kidegembiye aliamua kufuga nguruwe, nguruwe wake mmoja akawa na mimba, akapita bibi akamwambia maneno haya "hivi unatarajia kupata vitoto vya nguruwe eee, nakwambia hiyo sahau" na kweli siku nguruwe ana zaa akawa anatoa placenta a.k.a kondo la nyuma tuu hakuna kitoto hata kimoja!
Mfano wa pili ni yule binti Bernadetha Msigwa aliyepata upofu akiwa anasoma Mzumbe mwaka wa tatu na JPM akachangia 10,000,000 baada ya kusikia habari zake Clouds, yule binti baba yake ni mwalimu mkuu wa shule ya msingi, alikuwa hana mkopo wa masomo, majirani walisema hadharani kuwa tutaona kama kweli atamaliza hiyo chuo kikuu yake, na kweli Berna amekuwa kipofu hadi leo