Traxtion
JF-Expert Member
- Dec 10, 2021
- 7,595
- 15,506
Wengine wanatoa sababu kama nyumba za matope, slums, barabara mbovu, mpangilio mbovu wa mji na vumbi kama sababu halisi za kunyima Mbeya hadhi ya kuwa jiji. Lakini madai haya kwa asilimia kubwa yanapuuzia sababu halisi zinazofanya Mbeya iwe na hadhi ya jiji. Ukiniuliza mimi, nitakuambia ni kweli Mbeya ina barabara mbovu na mpangilio wa hovyo sana. Lakini je, hizi ni sababu za kufanya Mbeya lisiwe jiji? Hapana, sababu hizi zinafanya Mbeya kuwa jiji lenye barabara mbovu, au jiji lenye mpangilio wa hovyo na si kuondoa hadhi ya jiji moja kwa moja.
Nini maana ya jiji?
“Jiji ni mji mkubwa sana ulioendelea kiviwanda, kiuchumi na kijamii wenye idadi kubwa ya watu na hadhi maalumu kisheria au kiutawala. Mara nyingi linakuwa kitovu cha utawala kama vile kuwa makao makuu ya mkoa au nchi”
Hakuna vigezo vya dunia nzima vinavyotumika kuclassify majiji, mara nyingi hutegemea vigezo vya nchi husika, na hapa ndio confusion kubwa inatokea. Hata hivyo kuna sifa za msingi ambavyo majiji huwa navyo in common ambavyo kwa asilimia kubwa Mbeya ina sifa hizi zote.
Hapa nitataja sifa mbalimbali zinatofautisha Mbeya na miji ya kawaida kama Morogoro, Moshi na Iringa.
1.Mbeya ina mapato makubwa sana na biashara nyingi
Jiji la Mbeya ndio makao makuu ya mkoa wa Mbeya lakini pia ni sehemu inayokusanya mapato makubwa sana. Jiji la Mbeya always lipo top 5 ya miji yenye mapato makubwa zaidi Tanzania. Maana yake ni jiji linalojitosheleza sana kimapato kuliko miji mingi Tanzania kwa hiyo haiwezi kufanana na Iringa au Moshi. Jiji la Mbeya lina very big magnetic effect, watu kutoka maeneo kama Songwe, Makambako, Sumbawanga, Iringa, Njombe nk wanafanya movements kubwa sana za kuingia na kutoka ndani ya jiji la Mbeya kwa ajili ya biashara.
Jiji la Mbeya ni centre ya biashara kwa ukanda huu. Pia ni gateway ya kuingilia nchi jirani ya Zambia, kitu kilichofanya Mbeya kuwa very busy hadi barabara ya TANZAM imeharibika kutokana na shughuli hizi na bado inaonekana haitoshi, kwa sasa inapanuliwa kuwa njia nne (Japo kwa speed ya konokono)
2. Mbeya ina idadi kubwa sana ya watu
Jiji la Mbeya lina idadi kubwa sana ya watu, takribani watu laki 6 kwa eneo la jiji pekee. Hii inarudi moja kwa moja kwenye maana ya jiji. Siku zote sifa ya jiji lolote lile ni kuwa na watu wengi na kwa Tanzania watu alaki 6 katika mji mmoja ni wengi sana. Ndio sababu Mbeya always iko busy na biashara nyingi, ina population kubwa
3. Jiji la Mbeya ni kubwa sana kieneo
Moja ya sifa inayotofautisha Mbeya na miji kama Iringa au Mtwara sio tu population bali size ya mji pia. Jiji la Mbeya lina ukubwa wa takribani 250km2 . Size hii ni moja ya tatu ya jiji la Nairobi, meaning makazi ya watu yamesambaa kwa eneo kubwa sana. Eneo hili tayari ni kubwa sana kutosha sehemu kuwa jiji. Fun fact, watu wengi wanaishi Mbeya miaka na miaka bila kukanyaga maeneo mengine ya jiji hilo au bila hata kujua kama yanaexist. Mfano, ninajua wakazi wengi wa Uyole hawapajui Maziwa au St Marcus ambako ni 20km kutoka wanapoishi lakini ni ndani ya jiji moja.
4. Jiji la Mbeya limeendelea sana kwenye huduma nyingi za kijamii
Jiji la Mbeya liko mbali sana kwenye huduma nyingi za kijamii, kitu ambacho wengi wanakiouuzia wanapoanza kui judge Mbeya kuwa ni jiji au la.
Kwanza tukianza na shule. Jiji la Mbeya lina shule nyingi na zimezagaa karibia kila kona ya jiji kuanzia shule za serikali hadi za private, shule za primary hadi high school, za day hadi za bweni ikiwemo shule famous ya wasichana “St Francis Secondary School” na shule kongwe kama “Iyunga Technical Secondary School”
Kama shule si big deal basi angazia vyuo vinavyopatikana ndani ya jiji la Mbeya, kuanzia vya kati hadi vikuu ngazi ya Diploma hadi PHD. Mbeya ndio jiji la pili kwa kuwa na vyuo vingi nchini Tanzania, inazidiwa na Dar es Salaam pekee. Mfano wa vyuo vinavyopatikana Mbeya ni
- Mbeya University of Science and Technology (MUST)
- University of Dar es Salaam, Mbeya branch (MCHAS)
- Catholic University of Mbeya (CuoM)
- College of Business and Education, Mbeya branch (CBE)
- Tanzania Institute of Accountancy, Mbeya branch (TIA)
- Mzumbe University, Mbeya branch (MU)
- Teofilo Kisanji University (TEKU)
- Southern Highlands College of Health and Allied Sciences
- Agricultural Research Institute, Uyole
- Chuo cha Utumishi wa Umma Tanzania
- St John College of Health Science
- K’s Royal College of Health and Allied Sciences
- Mbeya Polytechnic College nk
Hivi vuo vyote zaidi ya 10 vipo ndani ya jiji la Mbeya na vyuo kama MUST na MCHAS ni among the best in Tanzania. Ukitazama kwa makini utagundua Mbeya ina vyuo vya kila aina kuanzia Uhandisi, biashara, Afya, Kilimo, sanaa nk
Tukija kwenye hospitali, kuanzia za serikali mpaka za private zimezagaa kila sehemu hapa Mbeya. Mfano wa hospitali za Mbeya ni
- Meta Maternity Hospital, (Biggest maternity hospital in Tanzania)
- K’s Hospital Mbeya
- Maranatha Hospital
- Mbeya Surgical Clinic
- Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya
- UWATA HOSPITAL, IVUMWE MBEYA
- UHAI Health Care nk
Mbeya kuna masoko mengi ikiwemo soko kubwa la Mwanjelwa, Kuna stendi za mabasi mbili, Nanenane na Stendi Kuu na pia stendi mpya inajengwa pale Old Airport.
Umeme na maji Mbeya uko available muda mwingi kuliko miji mingi Tanzania. Tena kwa sekta hii Mbeya ipo vizuri kuliko hata Dar. Ni nadra sana kusikia umeme umekatika Mbeya. Wanakata umeme lakini si mara nyingi na hawakawii kurudisha.
5. Mbeya ina viwanda vingi
Moja ya sifa inayotofautisha Mbeya na miji mingi ya kawaida Tanzania ni pamoja na viwanda vingi au makao makuu ya baadhi ya viwanda. Jiji la Mbeya lina hadi eneo lililotengwa kwa ajili ya viwanda “Iyunga Industrial Area” kuna viwanda vya Pepsi na Mirinda, Cocacola, TBL, tiles, magodoro, kuprocess kahawa, kiwanda cha madawa msd na vingine vingi
Mbeya iko busy sana kiuchumi, inaingiza na kutoa mizigo mingi sana kwenda mikoa mingine na nchi jirani. Isitoshe Mbeya ina hadi Bandari Kavu kutokana na shughuli za kiuchumi zilivyo nyingi
Now sisemi kuwa changamoto za Mbeya si za kweli. Changamoto zipo nyingi na asilimia kubwa ni kwa sababu ya uzembe wa serikali na hazifanyi Mbeya kutokuwa jiji. Barabara nyingi za Mbeya ni mbovu, bado zina mashimo, hakuna streetlights, mpangomji ni hovyo kabisa, vumbi kali pembezoni mwa barabara ya TANZAM kutokana na kuchelewa kupanua barabara hiyo, bado kuna uhaba wa mitaro na iliyokuwepo mingi imejaa mchanga na slums ni nyingi sana.
Licha ya serikali kuiacha Mbeya nyuma kwa miaka mingi kwa kutoipa miradi mingi inayostahili Mbeya bado imebaki kuwa kitovu cha uchumi Nyanda za Juu Kusini na watu hawajastop kujenge jiji lao. Mbeya inakua kwa kasi sana. Kila siku neighbourhoods mpya zinaibuka, watu wanafungua biashara, wanajenga nyumba nzuri, mji unakua. Ni miundombinu na mpangomji ndio vinaangusha jiji la Mbeya
Kutokana na Mbeya kuwa na nguvu kubwa sana kiuchumi, solution ya matatizo yake cha kwanza ni kuunda serikali za majimbo. Hii itawezesha mapato makubwa ya Mbeya kuweza kuboresha hali ya jiji la Mbeya na sio miji mingine na Mbeya itakuwa mbali sana kimiundombinu
Kwa sasa serikali inaona Mbeya kama tu just another town in Tanzania. Hawaichukulii serious enough ukilinganisha na potential ya jiji hili lakini siku Mbeya ikiweza kujitawala kama jimbo itafika mbali sana.