Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Mkoa wa Mbeya ni moja kati ya mkoa iliyopo katika Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania. Matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 yanaonesha kuwa idadi ya watukatika Mkoa wa Mbeya ni 2,343,754; wanaume 1,123,823 na wanawake 1,219,926
Mji wa Mbeya ulianzishwa na wakoloni Waingereza mnamo mwaka 1927. Wakati huo dhahabu ilianza kupatikana katika milima iliyopo karibu na Mbeya hadi Chunya hivyo Mbeya ulikuwa ni mji wa mapumziko kwa Wazungu kutokana na hali yake nzuri ya hewa, hali iliyosababisha mji wa Mbeya kupewa jina la utani kama "The Scotland of Africa"
Halmashauri za Mkoa wa Mbeya
Busokelo, Chunya, Kyela, Mbarali, Mbeya Mjini, Mbeya Vijijini na Rungwe.
Soma Pia: Orodha ya CV za Wabunge kwa mwaka 2020 - 2025 kutoka kila mkoa Tanzania
MAJIMBO YA MKOA WA MBEYA
Lupa: Watu 344,471
Mbarali: Watu 446,336
Mbeya Mjini: Watu 541,603
Mbeya Vijijini: Watu 371,259
Rungwe Magharibi: Watu 273,536
Busokelo: Watu 100,123
Kyela: Watu 266,426
Hali ya kisiasa
Katika uchaguzi wa mwaka 2020, Jiji la Mbeya lilishuhudia mabadiliko makubwa ya kisiasa. Ukilinganisha na chaguzi zilizopita ambapo vyama vya upinzani, hususan CHADEMA, vilikuwa na nguvu kubwa, CCM ilipata ushindi mkubwa katika maeneo yote. Hali hii ilivutia mjadala wa kisiasa kwa sababu Mbeya ilikuwa mojawapo ya ngome muhimu za upinzani.
Katika jimbo la Mbeya Mjini, Tulia Ackson (CCM) alipata kura 75,225, akimshinda Joseph Mbilinyi maarufu kama "Sugu" wa CHADEMA aliyepata kura 37,591.
Majimbo mengine kama Busekelo, Kyela, Lupa, Mbalali, Mbeya Vijijini, na Rungwe yote yalichukuliwa na wagombea wa CCM.
Matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu 2025
JANUARI
- CHADEMA Mbeya wamuonya Sugu na wenzake wasipomchagua Lissu, Dkt Tulia atapita bila kupingwa
- Pre GE2025 Wanafunzi wa vyuo wamchangia Rais Samia na Rais Mwinyi fedha ya fomu
- Meya wa jiji la Mbeya: Kila mtanzania anatamani Dkt. Tulia awe mbunge wa jimbo lake, Mbeya mkikataa aendelee atagombea jimbo lolote atashinda
- Mwenyekiti BAVICHA Mbeya: CHADEMA inahitaji kiongozi wa maamuzi magumu kama Lissu
- Mbunge wa Mbarali awataka UWT kutangaza habari za Rais Samia hadi msibani
- Pre GE2025 Spika Tulia: Hakutakuwa na ugumu wowote kwenye kampeni za mwaka huu. Mengi yaliyokuwa yanalalamikiwa, sheria zimebadilishwa
- Pre GE2025 Mwenyekiti BAVICHA Mbeya: CHADEMA inahitaji kiongozi wa maamuzi magumu kama Lissu
- Pre GE2025 Spika Tulia: Hakutakuwa na ugumu wowote kwenye kampeni za mwaka huu. Mengi yaliyokuwa yanalalamikiwa, sheria zimebadilishwa
- Dkt. Tulia alilipia Tiketi 1000, mechi ya Mbeya City FC dhidi ya African Sports!
- Pre GE2025 CHAUMMA kugawa ubwabwa kwa wananchi wa Jiji la Mbeya bure
- Pre GE2025 BAVICHA Mbeya: Tunamtaka Amani Manengelo aliyotoweka arudishwe akiwa mzima, tusije tukavuka mstari ambao hatutaki kuuvuka
- Pre GE2025 Kyela: CCM yasikitishwa kusuasua kwa utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Mbeya
- Pre GE2025 Mbunge David Silinde: Anaetamani kugombea jimbo la Tunduma aje, tutamnyoosha kuliko kipindi chochote
- Pre GE2025 Picha: Haya maandamano ya kuzindua Samia Legal Aid Campaign mkoani Mbeya yalikuwa na umuhimu gani?
- Pre GE2025 Mwenyekiti CCM, Mbeya: Tuwe waadilifu tusipokee wala kutoa rushwa ili tukipambanie chama
- Pre GE2025 Rais Samia ametoa zaidi ya TSh. Milioni 26 kwa Wahanga wa ajali Mbeya
- Pre GE2025 Video: Spika Tulia akiwa anacheza kwenye hafla ya utoaji wa bima za afya kwa wananchi 9,000 jijini Mbeya
- Pre GE2025 Madereva daladala jiji la mbeya wamtaka Dkt. Tulia kugombea tena ubunge 2025
- Pre GE2025 Bodaboda wamchangia Dkt. Tulia fomu ya ubunge Mbeya
- Mbunge kasaka ashiriki siku ya wanawake kwa aina yake, atoa mitungi ya gesi 100 na milioni 3 kwa akinamama
- Pre GE2025 Mbeya: Kikundi cha 'Wanawake shujaa' wilaya ya Rungwe, wamemchangia shilingi milioni moja Rais Samia fomu ya kugombea Urais
- Pre GE2025 Halmashauri ya Jiji la Mbeya imependekeza kuanza mchakato wa kuligawa jimbo la Mbeya mjini kupata jimbo jipya la Uyole
- Pre GE2025 Dkt. Tulia kuijengea nyumba familia yenye uhitaji Kyela, atoa msaada wa chakula na mavazi
- Pre GE2025 Mbeya: Dkt. Tulia amjengea nyumba mwananchi aliyeomba kujengewa na Rais