Uliza chochote kuhusu Rwanda

Uliza chochote kuhusu Rwanda

Ni kweli FDLR Bado ni tishio kwa usalama wa rwanda.mbona hao migambo hawafiki hata 5000 ni wachache ila tu idealogy Yao ndo mbaya..ila nguvu hawana..ni kweli wanapewa sapoti na majeshi ya DRC?
 
wananunua sh ngap kwa mchele grade one
Grade I sijawahi kuiona Rwanda, kwa mchele wa Tanzania. Ila, Grade II au III ndo ikifika huko inaitwa Grade I, na kwa pesa ya huku, ni kama 3,500-4,000. Grade I ya uhakika ukiwa na yo ni zaidi. Kwa rejareja hapo. Ila kwa jumla, haizijaachana mbali. Ukiwa na uwezo mkubwa, ukaweza kuwa na ghara lako, hakika kitu kipo.
 
Watanzania mna raha sana, na mna bahati nyingi mnazochezea.

Maisha si rahisi kama kwenu.

Uhalisia, ni kwamba Rwanda ni nchi ambayo inajitafuta, ukizingatia mauaji dhidi ya watutsi, mwaka 1994, yamefuta nchi na kuanza upya.

Mwaka 1994, Rwanda ilikuwa na wakazi si zaidi ya milioni 7.
Baada ya vita, wakimbizi wengi warirudi.
Ina maana hawakuwa na pa kushika, mbali na ardhi iliyopo. Kilichofanyika, ni serikali kuweka chini na kugawanya ardhi hiyo familia zote.
Nijambo lililofanikiwa kwa asilimia hata 95, 5 nyingine ikiwa wengine hawakufurahia kunyang'anywa ardhi yao.

Mpaka leo hii, wanyarwanda ni zaidi ya Milioni 14. Ardhi hiyo hiyo ya square kilometa 26,000 na kitu.

Miaka 30 ni muda mfupi sana kuweza kujenga uchumi na sekta zote za maisha.

Hivyo, changamoto hizo, ajira, makazi, na vitu kama hivyo, haviwapi watu maisha kama ya Tanzania au nchi nyingine ambazo hazijakumbana na historia kama ya Rwanda. Hivyo, kwa ujumla, ugumu wa maisha upo, na kulingana na mtu.

Hiyo ni sawa na Tanzania, kwa mtu asie na chanzo cha uhakika cha pesa, atakwambia maisha ni magumu
Vipi suala la miundo mbinu? na je rwanda wameweza vipi kudhibiti suala la ujenzi holela?
 
Cha kwanza kabisa kuna certificate of import, inapatikana kwa fedha ya Rwanda laki mbili(200,000 Frws), ushuru, kilo moja mara ya mwisho ilikuwa 500 kwa kilo, hapo uhakika wa 100% unapata kwa watu wa forodha mpakani.
Hii Certificate of import Unapata kwa kupeleka samples Au ni taratibu gani Unafanya,Au mpaka mzigo ukiwa boda
 
Nipe historia ya chuki ya wahutu na watutsi!!!
Hii ni ndefu sana.

Ila cha kukukumbusha, ni kwamba watutsi na wahutu kwa ujumla hawana chuki. Wanaona na kuzaliana, na kwa yale mambo yetu, wanadinyana fresh tu.

Tatizo kubwa ni viongozi.

Mwanzo wa hivi vitu, wakoloni waliwalisha watu matango, kwamba watutsi wanataka kumaliza wahutu, hivyo wajikomboe.
Walikuta wanyarwanda wana umoja, kabila hizo zilikuwa kama matabaka ya kwenu.
Baada ya kuona ni ngumu, walianzisha mfumo uitwao DIVIDE AND RULE. Walifanikisha kugawa watu sasa kupitia urefu,urefu wa pua,na vitu kama hivyo. Na wakafanikiwa.

Kikawaida, binadamu yeyote ana asili ya kulipiza kisasi. Kwa hiyo, tokea enzi hizo mpaka miaka ya nyuma, japo na mpaka sasa bado unayaona; uchu wa madaraka umekuwa kikwazo kikubwa.
Mwaka wa 1994, wahutu ndio walikuwa na uongozi. Watoto wa viongozi wote, walikuwa na matumaini ya kurithi uongozi.

Mpaka sasa, ni kama wengi bado hawajakubali matokeo. Wengi wakiwa nchi za nje, zenye uwezo mkubwa, wao kumwaga pesa kwa wenzao waliopo nchini Rwanda, si tatizo. Jiulize, mtu hawawahi kumiliki hata laki moja, mpe milioni moja, akamharass mtu, akamuue, akaue mifugo yake, ndo hayo yanayoendelea.

Sasa, inahappen kwamba ukishamjua huyo anaekufanyia hivo, ni ngumu kukaa kimya.
 
Ntakujibu kwa ninavyoelewa mimi( si precision ya 100%):

1. Si kweli. kwa sababu mifano ya taasisi zenye wasomi wa mfumo wa Kifaransa, ambao walio wengi ni wale wajulikanao kama wahutu, zipo. Mfano wa Rwanda Revenue Authority, na sehemu nyingine zinazohusika na pesa. Hawa, wana nidhamu ya hali ya juu. Si watu wa kukaa na kusubiri mshahara.

2. Si kweli kwa sababu ukifatilia, utagundua vigezo vinavyotumika kuweka watu kwenye makundi hayo ya ukabila, kila upande vipo. Utampata mtutsi mfupi, kiujumla zile sifa za watutsi hana. Na mhutu, utakuta ana kila sifa ya mtutsi. Na mbali na hilo, kwa sasa hivi ni ngumu, kwa sababu watu wanazaliana.

mfano mwingine, wanawake waliobakwa na Interahamwe mwaka 1994, ni watutsi, lakini wamezaa wahutu(kwa tunavoelewa kwamba mtoto ni kabila la baba'ke). Hawa, mbona wapo kwenye hizo ngazi?

3. Hata nyumbani kwako, huwezi kumuamini sana mjakazi kuliko mke wa ndoa. Hivyo,kutokana na historia ya nchi yenyewe, kuna watu wanaujua uchungu wa maisha kuliko wengine.
Sifa mojawapo kubwa ya kabila ni LUGHA. sasa inakuaje wahutu na watusi ni kabila wakat wote wanaongea lugha moja?
Hizo ni tribes au just ethnic groups??
 
Chaguzi zote kagame anaonekana kushinda kwa zaidi ya asilimia 90 ni kweli au anaiba kura
Kiukweli,ukiachana na wasomi na wanasisa wenye masirahi yao binafsi, raia wa kawaida wanampenda sana.

Mpaka leo, kila mmoja hujiuliza nani anaweza kuitawala Rwanda, kwa sababu Mr. tall hana hisia. Umekosea, hajali we ni nani, na una nini, unachostahili ndo utakachokipata.
Alipoingia madarakani, au RPF iliposhika nchi, kulikuwa na sababu 1000 za kulipisa kisasi.

Ni kweli wapo waliolipiza, sikatai. Lakini chama chake kingekuwa na nia ya kuua kila mhutu, ilikuwa rahisi.

Hivyo, wanaoitwa watutsi waliookolewa, lazima ndo chaguo lao.
Wahutu walionusurika, watoto wao wakasoma, waliouwa wakasamehewa, ni mambo ambayo ni kama hayawezekani.

Hivyo, Rwanda haina upinzani wa kufanya jambo lolote la maana.

Ukweli usemwe kama ulivyo, uongozi wake ni wa haki kwa walala hoi, ila mwiba kwa wapigaji. Ndo maana jambo hilo litalalamikiwa na watu wazito, ila raia wa kawaida hata ukiwambia kaja Yesu, sidhani
 
Kwann hawaamini kuwa Tz sio salama kwa wanyarwanda!? Walifanywa nini?
Ukianzia hapa mtandaoni, utaona.

Siku za nyuma, wanyarwanda Kagera wamefukuzwa, na wenye sura za kinyarwanda,walifukuzwa. Watu walinyang'anywa wake na waume, wapo watu waliozaliwa Tanzania na kufukuzwa, hao waliishia kambini kwa sababu hawakua na ukoo huko. Hizo ndo sababu kuubwa
 
Hebu nipe siri ya Amata na haswa 'Ikivuguto' kinatengenezwaje mbona ni matamu sana? Haswaa yale ya Nyabisindu hivi bado yako?

Na inawezekana kweli kufungua Branch katika miji yetu ya huku Bongo Cauntri?
Maziwa yapo mengi sana, maandalizi tu ndo changamoto.

Hata haya ya maduka ya vinywaji, yakiandaliwa vizuri, utadata. Achana na yale ya kunywea vijiko na kuchanganya na sukari.
Kuhusu kufungua Branch, sidhani kama ni rahisi, ukizingatia makubaliano ya kibiashara baina ya nchi husika, huenda uendeshaji ukawa mgumu.

Lakiini naamini, ukijifunza kutengeneza na ukawa na mtaji wako, Tanzania ngombe wapo wa uhakika.
Hasa ukizingatia nyie huko, mnao ngombe wanaokula majani ya asili,
 
1. ni kwa nn kagame amepenyeza watu wake ktk serikali ya tz, kwann isiwe ug au burundi?? tz ina nn hasa ambacho kinamtoa undenda mzee kgm

2. kati ya jwtz na jeshi la rwanda lipi unaliona jeshi bora kwako? ikitokea vita nani unampa ushindi?
 
Sifa mojawapo kubwa ya kabila ni LUGHA. sasa inakuaje wahutu na watusi ni kabila wakat wote wanaongea lugha moja?
Hizo ni tribes au just ethnic groups??
Ndo maana ni kasema hivi vitu alileta mkoloni, mfumo wa Divide and rule, kwa sababu jitihada za mwanzo alizokuwa amejaribu aliferi.
Hivo, kwa sababu bado historia inajirudia, bado hayo majina yapo, ila kiuhalisia ni matabaka
 
1. ni kwa nn kagame amepenyeza watu wake ktk serikali ya tz, kwann isiwe ug au burundi?? tz ina nn hasa ambacho kinamtoa undenda mzee kgm

2. kati ya jwtz na jeshi la rwanda lipi unaliona jeshi bora kwako?
1. Kama kweli kuna wanyarwanda wamepenyezwa, japo hilo silijui, naongea mimi kama mimi, huo ni udhaifu wa nchi walikopenyezwa. Tz haina chochote cha kumtoa udenda, kwa sababu kila nchi inaishi kwa uwezo ilio nao.


2. Hapa ntaongopa. Ila, kwa nachokiona, kila moja lina sehemu lipo imara, na sehemu haliko vizuri. Tuchukulie mfano: nahisi(japo kijeshi najua mambo yao ni siri zao), jeshi la Tanzania lina vifaa vingi mno. Lakini uzoefu wa vita, halina. Sababu ikiwa toka miaka ya zamani, hao kina Kagame, wamekuwa vitani toka miaka ya ujana wao mpaka leo, kulia na kushoto, wanajeshi wake wanaendelea na vita, hivyo uzoefu wanao wa kutosha.
 
Back
Top Bottom