Ni Rahisi kwenda Kanisani ama Msikitini kwamba unaenda kwenda kupokea vitu vya ki Mungu vitakavyo kusaidia katika maisha haya ya dunian.
Ndo maana unatoa sadaka kwamba anakupa vya Rohoni na wewe unampa vya mwilini wafanya vyema ni agizo la Mungu.
Tamaa za mwili na Mawazo mabaya ni dhahiri anaekupa vya Rohoni hakutendei haki basi wote hamwezi kutenda haki ya Mungu.
Wakolosai 3:5 - Basi, vifisheni viungo vyenu vilivyo katika nchi, uasherati, uchafu, tamaa mbaya, mawazo mabaya, na kutamani, ndiyo ibada ya sanamu;
Kwamba waabudu sanamu bila kujua na kiongozi wako hajui. Sanamu ni kitu unachokipenda ambacho hakina utukufu wa Mungu. Je unakuwa na tofauti gani na MPAGANI AHERI YAKE BASI KUMBE MAANA HAUJUI MLANGO WA KANISA.
Wapendwa kila mtu anapenda kutenda haki lakini shetani hataki. Ni jukumu lako kuomba ili Mungu akuone akutengenezee njia.
Maana njia iendayo uzimani ni Nyembamba tena imesonga songa.
Tamani kumuona bwana na Bwana akupe kuona. Maana dini zimeshindwa kuwasaidia watu bali watu wanazisaidia dini. Kumbe dini ni upuuzi tu kama upo kwenye dini na bado unalamba Mavi ati umflaishe mtu mdomo huo huo uende nao kwa Mungu ati unaomba kweli


umekula choo afu unafanya nn. Umepiga Mashine mke wa mwenzio, mke wa mwezio amekukula afu unaenda kanisani bila haya pasipo toba ya kweli. Yesu alipindua Mezza za wafanyabiashara, waliouza njiwa na mbuzi na wakabadilishana pesa. Akawaambia wazi Nyumba ya Baba yangu ni Nyumba ya Sala. Sasa mnajazana makanisani na misikitini kwa mambo haya ya matabia haya si ndo Yesu aliwakalipia ninyi.
Kuna ubaya gani mimi kuwakumbusha Habari njema kwamba upo uzima nao watoka kwa Bwana. Kama unaona haupo tayari kuacha dhambi si uache kupoteza pesa zako za zaka na sadaka piga Mbususu mwanawane.
Unajifanya VUGUVUGU huko mtaani kwako kwamba kanisani umo na kwenye uchafu UMO.
Heeeeeiii Neno la Mungu lipo wazi.
Ufunuo wa Yohana 3:16 - Basi, kwa sababu una uvuguvugu, wala hu baridi wala moto, nitakutapika utoke katika kinywa changu.
Ni aheri ya mpagani aliye Baridi Mungu anamtaka. Kanisani, msikitini umo na kwenye na sanamu umo. Mungu atakutapika sasa Nipo hapa sikutishi mpendwa. Mungu ni wa rehema anataka turejee kwake nami Nakukumbusha ni hasara kufa hujasahihisha haya ndo mana hamjui siku wala saa. Lakini ukisahihisha ukaishi katika Pendo lake Mungu. uwe na hakika utaijua siku na saa maana Yeye ni BABA TENA NI RAFIKI ATAKUPASHA HABARI.
Basi niache sasa tutaonana jioni KIMASIHARA ZIENDELEE WAPENDWA MLOPENDWA NA BWANA MPAKA AKAMTUMA MWANAE MIMI HAPA NIJE NIWAPE HABARI NJEMA. Ninyi niwapendwa. Baba anawapenda