Ulaji wa Panya mikoa ya Kusini: Safari yangu ya siku 37 ilivyonifungua mambo mengi

Kwahiyo kiislam panya Ni haram au?
 
Satoh Hirosh yupo sahihi panya wanaliwa sana hata mkoa wa Lindi maeneo yenye wakristo wengi.
Jamaa nimeamua kumkaushia Tu..sipendagi ligi,tena kaungana na Peramiho yetu wakawa wawili wananipinga,wakati Mimi nayajua nje ndani maeneo ya mikoa ya Lindi na Mtwara

Mkoa wa Lindi sehemu km Nyangao,mahiwa,namupa,sehemu za Rondo,Namangale,Baadhi ya vitongoji vya mtama,Nachingwea na baadhi ya vijiji vya Ruangwa vyenye wakristo wengi km luagalala,namahema NK panya wanalika vizuri tu
 
aisee umenichekesha sana, inaonekana kuna vingi vitamu kumbe hatujavionja tu!

ngoka nijaribu kuongezea kidogo kuhusu huyo mwalimu wako...........

very rough,
baadae alipata ukuu wa shule katika shule moja inaitwa nahukahuka,
baadae akahamia shule flani inaitwa mtua (bado yupo) kama mwalimu wa kawaida,
mkulima mzuri wa nyanya na mbogamboga zingine.....haoni hatari kujitwisha tenga la mchicha/nyanya kichwani na kutembeza!
 
Nimesoma o level pale Kaka
Nimemaliza 2011..Bila Shaka Kwa hili swali lako unapajua mahiwa
Hongera kijana mdogo. Nimesoma Ndanda, tulikua tunakimbia mchaka mchaka toka Ndanda mpaka Nangoo mtoni darajani pale.

Unayoyasema ni sahihi. Wamakonde, ambao wengi ni Waislam hawali panya. Panya huliwa sana wilaya ya Masasi kwa Wamakuwa.
 
Hongera kijana mdogo. Nimesoma Ndanda, tulikua tunakimbia mchaka mchaka toka Ndanda mpaka Nangoo mtoni darajani pale.

Unayoyasema ni sahihi. Wamakonde, ambao wengi ni Waislam hawali panya. Panya huliwa sana wilaya ya Masasi kwa Wamakuwa.
Yes ni kweli kabisa.masasi ndy wanakula sn samaki nchanga

Ila mm siyo kijana mdogo mkuu😁😁..tengua kauli yako
 
Kula panya wa porini si mikoa ya Kusini tu, hata Zambia na Malawi. Malawi wakati mwingine watoto wanakacha kwenda shuleni ili waende kutafuta panya porini wakati wa kipindi cha jua ambapo almost chakula kinakuwa hakuna. Zambia wanakula pia 'caterpillars' na kama umetembelea familia mara ya kwanza huenda utakaribishwa na bakuli au sahani ya caterpillars kama alama ya kuonyesha heshima kwa mgeni wao.
 

Ni kweli, hata Lindi na Mtwara mjini huwezi kukuta wanakula hao panya, ni baadhi ya maeneo wilaya za masasi na nachingwea
 
Sjui lini na mie nitembelee Kusini,

Na panya hawana msimu. Hahah

SUKAH
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…