All about Tanzania life
Member
- Jul 6, 2023
- 23
- 28
Imetimia idadi ya mikoa 19 Tanzania bara na mkoa mmoja Tanzania visiwani na wilaya zaidi ya 25 nilizotembelea hadi sasa. Wasalaam ndugu zangu.
Mwezi wa saba mwaka huu 2023 nilibahatika kutembelea mkoa wa Iringa. Ilikuwa ni safari kutembelea mikoa mitano tofauti ndani ya kanda mbili tofauti, kanda ya kati na kanda ya nyanda za juu kusini. Hapa nitaangazia niliyobahatika kujionea na kujifunza kutoka katika safari yangu kutembelea mkoa wa Iringa na baadhi ya wilaya zake.
Safari yangu kuelekea Iringa nilianzia Dodoma. Kutoka Dar es salaam hadi Dodoma mji mkuu wa Tanzania ilikuwa safari nzuri sana, nilifanya safari ya kwanza kuanzia hapo jijini Dar es salaam kupitia barabara kwa kutumia mabasi ya abiria hadi katikati ya Tanzania. Lengo lilikuwa ni kupata uzoefu wa kupita barabara iendayo Iringa kutokea Dodoma, niliambiwa njia hii ni nzuri na inavutia haswaa kutazama Mandhari pembezoni mwa barabara hii.
Nilifanikiwa kupata gari kutoka eneo moja maarufu kwa jina MAGOROFANI hapo Dodoma, nadhani kama sijakosea ni jina maana nilikuwa mgeni na ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika eneo hilo. Ni majira ya jioni muda wa saa kumi na moja na nusu ndio nilipata kupanda gari ya abiria kutokea Mwanza. Japo sikupanga kufanya safari hiyo majira ya jioni lakini ilinibidi niondoke mapema jijini Dodoma ili kuweza kuokoa muda wa kutembelea vivutio vingi nilivyopanga kuvifikia ndani ya mkoa wa Iringa.
Njiani safari ilikuwa nzuri na gari kampuni ya Capricorn ilikuwa na mwendo mzuri na salama kabisa kwa abiria wake na watumiaji wengine wa barabara. Safari ilikuwa nzuri tulipita maeneo ya Mkonze, Mpunguzi, na kupitia Google map niliona eneo linaitwa Manzese😁 na jingine likiitwa Fufu, kiukweli nyakati jua likikaribia kutoweka nilibahatika kuona hali ya ujangwa jangwa inayopatikana maeneo yale.
Kuna baadhi ya maeneo ni kame sana kwa kweli, wakati tunakatiza bwawa la Mtera ilishakuwa giza na usiku umeingia rasmi, hivyo kwa uchache niliona eneo la daraja na baadhi ya miundombinu inayotumika kukamilishia uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji. Eneo hili nililipenda sana, maana ni kati ya maeneo machache niliyotamani kuyaona hadi ikanifanya nipite njia hiyo.
Tulivuka salama na kuanza kupandisha vilima taratibu, hadi pale nilipoona eneo linaloitwa Nyang'oro kupitia simu yangu ya mkononi. Mwanzo niliona michoro ya kona kona nyingi kwenye ramani ya simu yangu na kisha kwa bahati mbaya sana mwendo mfupi mbele sikuweza tena kupata huduma ya mtandao kutokana na eneo hilo kutokuwa na mtandao wa uhakika. Kiukweli nili_enjoy sana maeneo hayo, fikilia kwa mara ya kwanza kukaa siti ya mbele ya gari tena nyakati za usiku na kuona barabara yenye kona kona nyingi mithili ya alama ya "S" na muonekano mzuri wa mlima Nyang'oro🙂 ulinifanya nione maisha ni ya thamani sana kama utafanya jambo ambalo moyo wako unalitamani zaidi.
Kutoka Nyang'oro tulisogea mbele zaidi na kufika eneo linaloitwa Ismani, nadhani ni eneo maarufu na watu wengi hapa wanalifahamu, kutoka Ismani gari yetu ilisimama Kihesa ambapo kwa msaada wa maelezo kutoka kwa abiria mwenzangu alinishauri nishukie hapo Kihesa kutokana na kuweza kupata huduma nafuu za malazi tofauti na kushukia mjini kati kabisa. Niliona ni wazo zuri na pia kwa kuwa niliona umbali kutoka Kihesa nitakaposhukia hadi kufikia kivutio cha kwanza nitachoanza kutembelea asubuhi yake ni karibu zaidi, basi niliafikia kushuka hapo. Aisee ile kushuka tu nikapokelewa na baridi kaliiiiii🥶🥶 almanusura nirudi ndani ya basi🙃.
Lakini nashukuru Mungu niliandaa koti nzito kwaajiri ya kukabiliana na hali ya baridi ambayo nilitegemea kabisa kukutana nayo huko.
Safari mpya ilianza sasa, kama kawaida kufumba na kufumbua nakuta bodaboda kama kumi hivi wameshanizunguka, ingekuwa kwa mji kama Dar es salaam ningezani ni majambazi maana sio kwa mikoti ile😃😀 ila jamaa ni waaminifu na wenye busala sana. Nilimchagua bodaboda mmoja na kumwomba anipeleke katika lodge moja isiyokuwa na bar wala kelele nyingi, pia isiwe mbali na barabara kuu na yenye ghalama nafuu. Bila hiyana akaniambia kalia sofa mzee!! Kwenye bodaboda baridi inapuliza haswaa, mwendo mfupi tu kama mita mia moja buku yangu ikawa imeshaliwa, yaani sehemu ya kutembea kwa miguu huku umefumba macho ikawa ndio nimeshafika hivyo😀😀.
Nilimshukuru na ukweli alinipeleka sehemu sahihi ambapo vigezo vyangu vyote nilivyovitaka vilikuwepo. Lodge ipo kimya sana, muhudumu wa kiume, na hadi naondoka majira ya asubuhi sikuweza kubahatika kuonana na mteja awaye yeyote hapo😎. Nilionyeshwa chumba changu juu mlangoni kikiwa na jina la Tembo, nikaweka begi langu moja dogo kisha nikarudi mapokezi na kuomba msaada wa kufika eneo la karibu lenye huduma ya vyakula na vinywaji.
Jamaa akanipa maelezo mafupi na muda mfupi baadae nilikuwa ndani ya bar moja kubwa na yenye mziki mkubwaaaa si mchezo. Kwa wale wakazi wa Dar es salaam na mikoa ya Pwani huko ambao hamjawahi kutembelea mikoa yenye baridi msidhani bar na pub za huku zipo waziwazi kama kule Buza, Mabibo sinza au hapo mtaani kwako. Aisee huku ni unaingia ndani ya mjengo, milango ya vioo ni kama unaingia club kwa huko Dar es salaam, hii yote inatokana na hali ya baridi inayokuwa imetawala muda wote huko nje.
(Nitaendelea hapa, muda ujao.)
Kuona zaidi mambo mengi kuhusu safari hii unaweza kutazama #All about Tanzania life kupitia Facebook/ All about Tanzania life.
Mwezi wa saba mwaka huu 2023 nilibahatika kutembelea mkoa wa Iringa. Ilikuwa ni safari kutembelea mikoa mitano tofauti ndani ya kanda mbili tofauti, kanda ya kati na kanda ya nyanda za juu kusini. Hapa nitaangazia niliyobahatika kujionea na kujifunza kutoka katika safari yangu kutembelea mkoa wa Iringa na baadhi ya wilaya zake.
Safari yangu kuelekea Iringa nilianzia Dodoma. Kutoka Dar es salaam hadi Dodoma mji mkuu wa Tanzania ilikuwa safari nzuri sana, nilifanya safari ya kwanza kuanzia hapo jijini Dar es salaam kupitia barabara kwa kutumia mabasi ya abiria hadi katikati ya Tanzania. Lengo lilikuwa ni kupata uzoefu wa kupita barabara iendayo Iringa kutokea Dodoma, niliambiwa njia hii ni nzuri na inavutia haswaa kutazama Mandhari pembezoni mwa barabara hii.
Nilifanikiwa kupata gari kutoka eneo moja maarufu kwa jina MAGOROFANI hapo Dodoma, nadhani kama sijakosea ni jina maana nilikuwa mgeni na ilikuwa mara yangu ya kwanza kufika eneo hilo. Ni majira ya jioni muda wa saa kumi na moja na nusu ndio nilipata kupanda gari ya abiria kutokea Mwanza. Japo sikupanga kufanya safari hiyo majira ya jioni lakini ilinibidi niondoke mapema jijini Dodoma ili kuweza kuokoa muda wa kutembelea vivutio vingi nilivyopanga kuvifikia ndani ya mkoa wa Iringa.
Njiani safari ilikuwa nzuri na gari kampuni ya Capricorn ilikuwa na mwendo mzuri na salama kabisa kwa abiria wake na watumiaji wengine wa barabara. Safari ilikuwa nzuri tulipita maeneo ya Mkonze, Mpunguzi, na kupitia Google map niliona eneo linaitwa Manzese😁 na jingine likiitwa Fufu, kiukweli nyakati jua likikaribia kutoweka nilibahatika kuona hali ya ujangwa jangwa inayopatikana maeneo yale.
Kuna baadhi ya maeneo ni kame sana kwa kweli, wakati tunakatiza bwawa la Mtera ilishakuwa giza na usiku umeingia rasmi, hivyo kwa uchache niliona eneo la daraja na baadhi ya miundombinu inayotumika kukamilishia uzalishaji wa umeme kwa kutumia maji. Eneo hili nililipenda sana, maana ni kati ya maeneo machache niliyotamani kuyaona hadi ikanifanya nipite njia hiyo.
Tulivuka salama na kuanza kupandisha vilima taratibu, hadi pale nilipoona eneo linaloitwa Nyang'oro kupitia simu yangu ya mkononi. Mwanzo niliona michoro ya kona kona nyingi kwenye ramani ya simu yangu na kisha kwa bahati mbaya sana mwendo mfupi mbele sikuweza tena kupata huduma ya mtandao kutokana na eneo hilo kutokuwa na mtandao wa uhakika. Kiukweli nili_enjoy sana maeneo hayo, fikilia kwa mara ya kwanza kukaa siti ya mbele ya gari tena nyakati za usiku na kuona barabara yenye kona kona nyingi mithili ya alama ya "S" na muonekano mzuri wa mlima Nyang'oro🙂 ulinifanya nione maisha ni ya thamani sana kama utafanya jambo ambalo moyo wako unalitamani zaidi.
Kutoka Nyang'oro tulisogea mbele zaidi na kufika eneo linaloitwa Ismani, nadhani ni eneo maarufu na watu wengi hapa wanalifahamu, kutoka Ismani gari yetu ilisimama Kihesa ambapo kwa msaada wa maelezo kutoka kwa abiria mwenzangu alinishauri nishukie hapo Kihesa kutokana na kuweza kupata huduma nafuu za malazi tofauti na kushukia mjini kati kabisa. Niliona ni wazo zuri na pia kwa kuwa niliona umbali kutoka Kihesa nitakaposhukia hadi kufikia kivutio cha kwanza nitachoanza kutembelea asubuhi yake ni karibu zaidi, basi niliafikia kushuka hapo. Aisee ile kushuka tu nikapokelewa na baridi kaliiiiii🥶🥶 almanusura nirudi ndani ya basi🙃.
Lakini nashukuru Mungu niliandaa koti nzito kwaajiri ya kukabiliana na hali ya baridi ambayo nilitegemea kabisa kukutana nayo huko.
Safari mpya ilianza sasa, kama kawaida kufumba na kufumbua nakuta bodaboda kama kumi hivi wameshanizunguka, ingekuwa kwa mji kama Dar es salaam ningezani ni majambazi maana sio kwa mikoti ile😃😀 ila jamaa ni waaminifu na wenye busala sana. Nilimchagua bodaboda mmoja na kumwomba anipeleke katika lodge moja isiyokuwa na bar wala kelele nyingi, pia isiwe mbali na barabara kuu na yenye ghalama nafuu. Bila hiyana akaniambia kalia sofa mzee!! Kwenye bodaboda baridi inapuliza haswaa, mwendo mfupi tu kama mita mia moja buku yangu ikawa imeshaliwa, yaani sehemu ya kutembea kwa miguu huku umefumba macho ikawa ndio nimeshafika hivyo😀😀.
Nilimshukuru na ukweli alinipeleka sehemu sahihi ambapo vigezo vyangu vyote nilivyovitaka vilikuwepo. Lodge ipo kimya sana, muhudumu wa kiume, na hadi naondoka majira ya asubuhi sikuweza kubahatika kuonana na mteja awaye yeyote hapo😎. Nilionyeshwa chumba changu juu mlangoni kikiwa na jina la Tembo, nikaweka begi langu moja dogo kisha nikarudi mapokezi na kuomba msaada wa kufika eneo la karibu lenye huduma ya vyakula na vinywaji.
Jamaa akanipa maelezo mafupi na muda mfupi baadae nilikuwa ndani ya bar moja kubwa na yenye mziki mkubwaaaa si mchezo. Kwa wale wakazi wa Dar es salaam na mikoa ya Pwani huko ambao hamjawahi kutembelea mikoa yenye baridi msidhani bar na pub za huku zipo waziwazi kama kule Buza, Mabibo sinza au hapo mtaani kwako. Aisee huku ni unaingia ndani ya mjengo, milango ya vioo ni kama unaingia club kwa huko Dar es salaam, hii yote inatokana na hali ya baridi inayokuwa imetawala muda wote huko nje.
(Nitaendelea hapa, muda ujao.)
Kuona zaidi mambo mengi kuhusu safari hii unaweza kutazama #All about Tanzania life kupitia Facebook/ All about Tanzania life.