Shirika la kitaifa la ndege la Sri Lanka limelaumu uwepo wa panya kwenye ndege kwa kusitisha safari za ndege kwa siku tatu

Kaka yake shetani

JF-Expert Member
Feb 1, 2023
3,595
8,729
Shirika la kitaifa la ndege la Sri Lanka limelaumu uwepo wa panya kwenye ndege kwa kusitisha safari za ndege kwa siku tatu.

Panya huyo aliyejificha bila kupatikana kwa siku tatu, alionekana kufurahia safari ya ndege ya Srilankan Airlines Airbus A330 kutoka mji wa Lahore, nchini Pakistan siku ya Alhamisi, na kusababisha utafutaji wake ndani ya ndege ili kuhakikisha kuwa haikuleta madhara kwa ndege.

Shirika la Ndege la Taifa la Sri Lanka Jumanne limemlaumu panya kwa kulemaza safari za ndege kwa siku tatu, na kusababisha hofu kwamba tukio hilo litawatisha wawekezaji kwa shirika hilo la ndege lenye changamoto nyingi.

Afisa mmoja wa shirika la ndege alisema kuwa ndege hiyo sasa imeanza tena safari zake, lakini kwamba kutua kwake kulikuwa na athari ya kusambaratisha ratiba nzima.
Source TRT afrika habari
FB_IMG_1709466056972.jpg
 
Hahaaa, Panya Analaumiwa???
Anyway wana hoja, Akipita na Waya Sensitive tuu ni shoo, hamna parking angani.
Haa noma sana! Ukute sasa ndege ipo kwenye auto pilot mode af akate waya wa mfumo wa kompyuta. Hakika ni shidaa.
 
Panya hawana maana kabisa,nakumbuka siku moja nimesafiri nikachukua tu begi nikajaza nguo,ile nimefika hoteli niko chumbani nafungua zipu panya karuka nje,nikasema hii ndio ingenikuta pale reception mbona ingekuwa tafrani,maana niliingia kwa pozi za hatari...
 
Panya hawana maana kabisa,nakumbuka siku moja nimesafiri nikachukua tu begi nikajaza nguo,ile nimefika hoteli niko chumbani nafungua zipu panya karuka nje,nikasema hii ndio ingenikuta pale reception mbona ingekuwa tafrani,maana niliingia kwa pozi za hatari...
Hahahaha
 
Back
Top Bottom