Ukweli una pande mbili

Ukweli una pande mbili

realMamy

JF-Expert Member
Joined
Apr 28, 2024
Posts
7,307
Reaction score
18,240
1000144661.jpg


Kamwe usiamini hadithi ya upande mmoja. Daima huwa na kurasa zilizokosekana.

Watu wengi wamekuwa wakihukumu watu kwa kutumia upande mmoja wa hadithi, bila kujali ni kwa namna gani wanaumiza wengine.

Kusikia upande mmoja tu wa story ni hatari. Mara nyingi mtu anakwambia sehemu inayomfaa yeye na kuacha zile zinazomtoa kwenye lawama.

Hadithi yoyote ya upande mmoja inakosa ukamilifu. Ni kama kitabu kilichoraruliwa kurasa kadhaa - huwezi kuelewa mwisho wake vizuri.

Hii inatufundisha kuwa wavumilivu na kutafuta ukweli wa pande zote kabla ya kuhukumu watu Katika urafiki, kazi, na hata kwenye mitandao.

Na uvumi mwingi unatokea kwa sababu watu wanasikiliza upande mmoja tu wa hadithi.
1000144664.jpg


Kwa hiyo unapoletewa story au hadithi yoyote kuhusu mke,mfanyakazi wako,mwanao,rafiki Yako na wengine tumia muda kufuatilia, kuuliza, kusikiliza, na kuelewa kwanza ndipo utapata ukweli kamili utakaokusaidia kuhukumu.

1000144665.jpg
 
Ni kama story tunazolishwa na wazazi wetu haswa akina mama,kuhusu Baba zetu ukiwasikiliza sana bila kutafuta ukweli wa pili unaweza mchukia Baba Hadi unakufa
 

Attachments

  • 20260721_213659.jpg
    20260721_213659.jpg
    431.6 KB · Views: 5
Wanakuwa na masirahi yao, kwa mfano umkute mwanamke aliyeachika anasimulia yaliyomfanya aachike utasema wanaume wote ni mbwa, haya mkute mwanaume aliyeachika akuambie kuhusu wanawake utawaona wanawake wote fisi maji
Kwamba ikiwa ni wewe uta hadithia nini kuhusu mtalaka wako?

Watu wakiachana kila mmoja huamini kakosewa so hakuna tatizo lolote akihadithia muhimu asimdhalilishe na kutweza utu wake

Waswahili wanasema usimalize maneno
 
Wanakuwa na masirahi yao, kwa mfano umkute mwanamke aliyeachika anasimulia yaliyomfanya aachike utasema wanaume wote ni mbwa, haya mkute mwanaume aliyeachika akuambie kuhusu wanawake utawaona wanawake wote fisi maji
Umejua kunifurahisha 😅
 
Kwamba ikiwa ni wewe uta hadithia nini kuhusu mtalaka wako?

Watu wakiachana kila mmoja huamini kakosewa so hakuna tatizo lolote akihadithia muhimu asimdhalilishe na kutweza utu wake

Waswahili wanasema usimalize maneno
Unaeleza ukweli, mpaka mnatalakiana maana yake wote mna makosa kuna mahali mwanaume amezingua na kuna mahali mwanamke amezingua kuliko kupeleka mzigo kwa mmoja ili wewe uonekane uko safi
 
Back
Top Bottom