Ukistaajabu tozo za miamala kuna na hili la Kodi ya Jengo kulipwa kutumia LUKU

Missile of the Nation

JF-Expert Member
May 24, 2018
13,502
51,098
Yaani sijui wachumi wa rais Samia ni watu wa namna gani, wako out of touch kabisa na maisha ya mtanzania halisi.

Lakini tatizo kubwa ni kuteua watu wanaojipendekezapendekeza kwa watawala kwa ajili ya ambition binafsi, badala ya kuteua watu ambao wana principles zao, ambao wanawaza faida za maamuzi kwa faida ya wananchi wengi badala ya maslahi yao binafsi

Leo eti kuna kodi ya Jengo ambayo kusheria na kikawaida inabidi ilipwe na mwenye Jengo husika, Lakini leo akina Mwigulu wanasema hapana, Kodi hii alipe Mpangaji kwenye hilo jengo kupitia LUKU pindi anaponunua umeme, halafu eti Mpangaji na Mwenye Jengo watajuana wenyewe kwa wenyewe watarudishianaje hiyo hela!

Yaani hapa Wajibu wa serikali wa kukusanya kodi anatwishwa mpangaji ambaye ni wananchi wengi, eti mwananchi awe ndo mwenye kumlipia mwenye jengo kodi ya jengo lake halafu eti yeye atazireclaim hizo pesa.

Hapa Serikali isitake kutupiga changa la macho, technically wajibu wa kidi ya nyumba serikali imeuhamishia kwa mpangaji badala ya mwenye jengo kwa sababu kwanza

1. Serikali haijafanya survey ya majengo yote nchini ili kujua kila jengo linastahiki kodi ipi ya jengo

2. Nyumba za kupanga wakati mwingine wanakaa mpanfaji zaidi ya mmoja, wakati mwingine kila mpangaji na mita yake, na wakati. mwingine wapangaji wote wanashare mita. Sasa katika mazingira haya ambayo kila mpangaji ana mkataba binafsi na mwenye nyumba convenience ya kuingiza makato hayo ya LUKU kwenye mkataba wa upangaji yanakuwaje rahisi?.

3. Kiwango cha matumizi ya umeme ya wapangaji katika nyumba wanayoshare ni tofautitofauti, Sasa mechanism ya kukukotoa refund kutoka kwa mwenye nyumba imekaaje?

4. Serikali haijatunga sheria kulazimisha refund ya mwenye jengo kwenda kwa mpangaji, pindi mpangaji atakapolipa kodi ya Jengo kwa niaba ya mwenye Jengo pindi mpangaji akinunua LUKU

Kiufupi Samia yeye anakwenda kuchokonoachokonoa angle zote ambazo ziliwapa wananchi unafuu kwenye maisha yao ya kila siku, yaani hapimi consequence za makodikodi yake. Anayafanya maisha yetu kuwa magumu sana.

Hatuwezi kufika kwa mtindo huu
 
Serikali hii sio rafiki kwa watu wa kipato Cha chini.

Serikali imeamua isiwatoze Kodi wafanyabiashara wakubwa badala yake imeamua kuhamishia mzigo wa gap litalotokana na kutokusanya Kodi Toka kwa wafanyabiashara wakubwa Kwa watu wakipato Cha chini.

Ndio maana viongozi wakuu wanaona hata aibu kufanya ziara kutembelea wananchi wao wanakesha angani kwenda ngambo huko.

Mkuu anaruka tu angani , Hana muda kabisa na watu wa chini, anawaonea aibu atawaambia Nini.
 
Kodi ya jengo+kodi za miamala ya simu+kodi ya mafuta ya gari

Jaman tuendelee tu kuwapa tu hzi hela ili waendelee kulipana mishahara na marupurupu kibao
 
Endeleeni kushangilia mama anaupiga mwingi .

This is your bitter surprise you waited following the passing away of "Dikteta"

Mama yenu amezigeuza Airbus kuwa daladala za Dom-Dar, katiba amekataa kuibadili Kama mwenda zake!

Sukuma gang kawamaliza haya tulieni tule matunda ya "Uhuru" na demokrasia chini ya Tanzanite woman

"It was too early to celebrate"
 
Habari Greater thinker! Asante kwa uchambuzi, lakini naona umeonyeshwa udhaifu bila kupendekeza suluhisho. Njia zipo mbili na kila moja ina faida na hasara,

1. Mpangaji kulipa na kuwa refunded na mwenye nyumba kama ambavyo mwenye duka nakusanya VAT kutoka kwa mtumiaji kwa niaba ya Serikali. Faida hapa mpangaji atahakikisha kuwa analipa kwa wakati ili kuwa na uhakika wa umeme,kwani ukikatwa ni mwathirika wa kwanza

2. Mwenye nyumba kulipa moja kwa moja kupitia kulipa umeme,yaweza kuwa njia bora ila anaweza kuchelewa kulipa na kusababisha hasara kwa mpangaji. Njia zote zina faida na hasara nadhani tuje na suluhisho kuliko KULALAMIKA MWANZO MWISHO.

Mwisho, niliwahi kusema WATANZANIA HATUNA UTAMADUNI WA KULIPA KODI, na htupendi KULIPA KODI. Nchi haiwezi kujengwa bila kodi za wananchi wazalendo,nakumbuka kuna kipindi kodi za majengo zilikuwa elfu kumi (10,000) tu kwa mwaka ila tulikuwa hatulipi/tunalipa kwa shida sana. Naomba tubadirike tuungane na Mhe. Rais SSH kuijenga Nchi yetu.
 
Hapo kwenye kuweka kodi ya nyumba wamefeli kwa 100% wanashindwa nini kuweka mfumo mwingine wa kodi hadi waweke kwenye mfumo wa umeme
Mkuu hapa wanatafuta urahisi kwa kuwa waliacha miji ikajengwa kiholela na inakuwa si rahisi kuorodhesha Majengo yote ili wambane mwenye jengo kulipa Kodi.

Huu unyanyasaji kwa wapangaji.
 
Kodi hii ni buku 10 kwa mwaka yaani kama mpo wapangaji 4 na luku ni moja kila mtu anatoa buku 2500 kwa mwaka punguzeni kulamika
WATANZANIA HATUNA UTAMADUNI WA KULIPA KODI, na hatupendi KULIPA KODI. Nchi haiwezi kujengwa bila kodi za wananchi wazalendo,nakumbuka kuna kipindi kodi za majengo zilikuwa elfu kumi (10,000) tu kwa mwaka ila tulikuwa hatulipi/tunalipa kwa shida sana. Naomba tubadirike tuungane na Mhe. Rais SSH kuijenga Nchi yetu.
 
WATANZANIA HATUNA UTAMADUNI WA KULIPA KODI, na hatupendi KULIPA KODI. Nchi haiwezi kujengwa bila kodi za wananchi wazalendo,nakumbuka kuna kipindi kodi za majengo zilikuwa elfu kumi (10,000) tu kwa mwaka ila tulikuwa hatulipi/tunalipa kwa shida sana. Naomba tubadirike tuungane na Mhe. Rais SSH kuijenga Nchi yetu.
Ishu siyo kulipa kodi,hoja iliyopo mezani ni uhalali wa kodi ya jengo kulipwa na mpangaji badala ya mmiliki wa jengo.
 
Unampinga mwenyekiti wako wa chama?
Serikali hii sio rafiki kwa watu wa kipato Cha chini.

Serikali imeamua isiwatoze Kodi wafanyabiashara wakubwa badala yake imeamua kuhamishia mzigo wa gap litalotokana na kutokusanya Kodi Toka kwa wafanyabiashara wakubwa Kwa watu wakipato Cha chini.

Ndio maana viongozi wakuu wanaona hata aibu kufanya ziara kutembelea wananchi wao wanakesha angani kwenda ngambo huko.

Mkuu anaruka tu angani , Hana muda kabisa na watu wa chini, anawaonea aibu atawaambia Nini.
 
Serikali hii sio rafiki kwa watu wa kipato Cha chini.

Serikali imeamua isiwatoze Kodi wafanyabiashara wakubwa badala yake imeamua kuhamishia mzigo wa gap litalotokana na kutokusanya Kodi Toka kwa wafanyabiashara wakubwa Kwa watu wakipato Cha chini.

Ndio maana viongozi wakuu wanaona hata aibu kufanya ziara kutembelea wananchi wao wanakesha angani kwenda ngambo huko.

Mkuu anaruka tu angani , Hana muda kabisa na watu wa chini, anawaonea aibu atawaambia Nini.
Mwendazake alisafisha hazina,acha mama aongeze Kodi kila sehemu
1626514030009.png
 
Back
Top Bottom