Ukiitegemea biashara yako mpya ikulishe, ikulipie kodi ya nyumba na kadhalika, jiandae kuanguka

Habari wakuu,

Ukosefu wa ajira serikalini, taasisi mbali mbali, viwandani n.k imekuwa ndio chanzo cha vijana wengi mpaka wazee kukimbilia kwenye biashara,

Wengi tunapoanza biashara huwa hatuna uelewa wa kutosha, maarifa tunayoyapata kwa kuulizia ulizia kwa watu, mtandaoni au kwa ndugu na marafiki huwa hayajitoshelezi, hili jambo ni hatari sana.

Unakuta mtu ameanzisha biashara yake mpya hapo hapo anaitegemea imlipie kodi ya fremu, umeme, TRA, taka, ulinzi, kodi ya anakoishi, maji, chakula, vocha, usafiri n.k,

Ukiona upo kwenye hali kama hiyo jua moja kwa moja ushaanguka, siku si nyingi utafilisika au kuanza kuhisi unachawiwa kumbe tatizo niwewe mwenyewe,

ukitaka kuanzisha biashara hakikisha una kazi (ajira), kipato kingine cha ziada cha kukulisha, kukuvisha, kukulipia kodi ya nyumba, vocha n.k hapo utatoboa mapema tu ndani ya miezi hata 9 au 10,

ila ukianzisha biashara wakati unanjaa, au umepigika ndugu wamekuchangia mtaji wa milioni 3 au umekusanya pesa ukaacha kazi, au umefungua biashara kwa pesa za pensheni baada ya kustaafu tegemea anguko, kufirisika kuhama mtaa au kurudi nyumbani kwenu. Ndio maana waswahili wanasema mwenye nacho huongezewa


Hii ndio sababu inayopelekea biashara nyingi mpya kufa haraka hata bila kumaliza miezi 8 au mwaka,

NB: USIANZISHE BIASHARA WAKATI UKIWA NA NJAA. Akili ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO

Nawasilisha
Changamoto inayokabili huwez Anza biashara ukiwa umeshiba
 
Nimefungua fremu ya viatu vya watoto na wanawake siku 8 sijauza hata pair 1, frame laki 2x 6 months!! Naona nyotanyota! Mzigo (gharama)1.5m, leseni+bills (bado sijapigia hesabu). Halafu utashangaa TRA sijui manispaa na ving'ora.
Watu mna mitaji ila hamjui mfanyie nini jamani. Hiyo hela ingetosha kupata hela ya kuikuza kabisa
 
Mwenye uzoefu wa biashara ya pombe reja reja anipe elimu kidogo tafadhali
Unataka kufungua grosary au bar,kama ni ivyo tafuta location nzuri karibu na soko au stendi au maeneo ya starehe palipochangamka, weka msichana mzuuri mwenye kishundu alafu weka mzigo mpigiane mahesabu n.k asikopeshe narudia asikopeshe ,wwka sabufa miziki kama yote sehemu isiwe wazi sana . ila zamani pombe iliku na faida wacha kabisa ,nimeuza grosar ya mama wakati nipo seko nilikua nalewa sana na viroba hadi naingia navyo skuli
 
Njooni tupige bodaboda, mimi nikitoka zangu kazini mida ya jioni naingia kijiweni kupose na boda yangu. Kufikia saa tatu usiku sikosi 10 kama faida ingawa hii kazi ni risk saana.
 
Nashukuru kwa kulileta hili hapa jukwaani maana imenigusa haswa. Niliwahi kuanguka kwa kutegemea biashara moja kwa moja!

Moja ya somo ambalo nililipata ndio hili ambalo umepost hapa. You can never succeed in business kama huna namna ya kui support (probation period) mpaka itakapoanza kujiendesha yenyewe kwa uhakika. Wengi tunaanzisha biashara with expectations kwamba zitufanyie kila kitu which is not realistic kwa biashara mpya!

Ndio maana watu ambao wana extra sources of income wana succeed kirahisi sana na ku realize ukuaji wa biashara sababu anaitazama kwa kando biashara yake inavyokwenda na mahesabu yake! Haigusi kabisa mpaka itakapoanza kuzalisha faida kubwa. Ila wengine mtu anaanzisha genge na kuanza kulitafuna pre-maturely lazma ukaange mtaji!
Vipi kuhusu usimamizi wa biashara ukiwa muajiriwa?
 
Habari wakuu,

Ukosefu wa ajira serikalini, taasisi mbali mbali, viwandani n.k imekuwa ndio chanzo cha vijana wengi mpaka wazee kukimbilia kwenye biashara,

Wengi tunapoanza biashara huwa hatuna uelewa wa kutosha, maarifa tunayoyapata kwa kuulizia ulizia kwa watu, mtandaoni au kwa ndugu na marafiki huwa hayajitoshelezi, hili jambo ni hatari sana.

Unakuta mtu ameanzisha biashara yake mpya hapo hapo anaitegemea imlipie kodi ya fremu, umeme, TRA, taka, ulinzi, kodi ya anakoishi, maji, chakula, vocha, usafiri n.k,

Ukiona upo kwenye hali kama hiyo jua moja kwa moja ushaanguka, siku si nyingi utafilisika au kuanza kuhisi unachawiwa kumbe tatizo niwewe mwenyewe,

ukitaka kuanzisha biashara hakikisha una kazi (ajira), kipato kingine cha ziada cha kukulisha, kukuvisha, kukulipia kodi ya nyumba, vocha n.k hapo utatoboa mapema tu ndani ya miezi hata 9 au 10,

ila ukianzisha biashara wakati unanjaa, au umepigika ndugu wamekuchangia mtaji wa milioni 3 au umekusanya pesa ukaacha kazi, au umefungua biashara kwa pesa za pensheni baada ya kustaafu tegemea anguko, kufirisika kuhama mtaa au kurudi nyumbani kwenu. Ndio maana waswahili wanasema mwenye nacho huongezewa


Hii ndio sababu inayopelekea biashara nyingi mpya kufa haraka hata bila kumaliza miezi 8 au mwaka,

NB: USIANZISHE BIASHARA WAKATI UKIWA NA NJAA. Akili ZA KUAMBIWA CHANGANYA NA ZAKO

Nawasilisha
Vipi kuhusu usimamizi wa biashara ukiwa muajiriwa? Wapo walioanguka kibiashara wakiwa waajiriwa na hawakuwa tegemezi wa biashara zoo ila changamoto kubwa ni usimamizi wa hizo biashara zao
 
Huo ndiyo Ukweli Mkuu!

Nilianza biashara ya M-Pesa kwa miaka 6 iliyopita. Niliweka pesa kama Million 2 tu, baada ya kulipia frame, leseni na kila kitu. Lakini, sikuwa na wazo lolote la kuniletea faida kwa wakati huo.

Mwezi wa kwanza katika biashara nilipata 36,000 tu. Imagine kama ndiyo nilikuwa naitegemea initoe.

Biashara hiyo ilinipigisha kwata miezi nane bila return ya maana. Hata mdada aliyekuwa akinisaidia nammegea sehemu ya Mshahara wangu.

Baadae hali ikachachamaa, mambo yakaanza kuwa mazuri. Angalau sasa malipo ya binti yakaanza kulipwa na Commission. Sipati kitu. Lakini it worth fighting.

Miaka sita sasa, nina mtaji wa zaidi ya Million 40 na sijawahi kutia mia yangu nyingine tangu niweke ile 2M. Imejizalisha mpaka kufika hapo.

Sema nilikuwa sichukui faida. Ikipatikana, narudisha humo humo. 2019 mwishoni ndiyo nikaanza kuchukua Commission inayopatikana huku kiasi kingine nakiacha.

Sasa imagine kama ndiyo nilikuwa naitegemea. Ndani ya miezi mitatu tu hiyo hela ingeshaisha. Kuwa na kipato kingine tofauti kitakachokuwezesha kuishi wewe kama wewe na backup ya biashara yako kama beginner.
2m to 40 m , umejitahidi sana bro na pesa una nidhamu nayo , kudos
 
Wazee wameniachia duka la dawa la jumla lenye mtaji wa mil 15 wakati duka lilikuwa na thamani ya mil 300 yaani nimedata aisee..duka halina items nyingi sana nikienda kwa importer hawataki kuniuzia kwa bei ya chini mpka nichukue kuanzia mzigo wa mil 4 ndio wananiuzia kwa bei ya chini na hiyo mil 4 wananipa items moja mfano kama ni ampiclox caps bhasi mil 4 nanunua ampiclox caps tu sio dawa mchanganyiko.kilichobaki nimekuwa mchuuzi sasa naingia k/koo napita kila duka kuangalia duka gani wanauza dawa bei rahisi ndio nanunua.
Duka kidogo linasogea kwa siku faida elfu 90 ingawa elfu 90 ni ndogo mno,Mungu ni mwema naendelea kupambana naamini duka litarudi litakuwa kwenye peak Kama zamani .

NB:biashara ngumu sana aisee
 
Back
Top Bottom