Ukiitegemea biashara yako mpya ikulishe, ikulipie kodi ya nyumba na kadhalika, jiandae kuanguka

Kuna jirani yangu yeye alifungua mini-supermarket daily anatupa vitu vilivyooza/haribika hajawahi kuuza hata mkate 1pc. Kweli biashara hizi tuwaachie Wapemba/wahindi/waarabu sisi waswahili tuendelee kupiga domo Kama Msemaji (aliyetimuliwa)
Hizi biashara za kuuza bidhaa zinataka moyo sana..
Mimi kuna miaka nilikuwa na biashara ya hardware, nikabebwa na ule ujinga wa vitu vya hardware haviozi, ndio haviozi ila je mzunguko upo?
Kuna items niliweka toka nafungua duka mpka limekuja kunishinda hazijauzika kabisa na hapo ni kama miaka mitatu.
Hizi physical business zimenipa uoga sana, hata kama nitarudi kwenye biashara basi nitafanya services na sio kuuza bidhaa.

Ila cha ajabu watu humo humo wanatoboa na wanafanya mambo makubwa kabisa ukiwa na imani ndogo utasema wanaroga .
 
Wazee wameniachia duka la dawa la jumla lenye mtaji wa mil 15 wakati duka lilikuwa na thamani ya mil 300 yaani nimedata aisee..duka halina items nyingi sana nikienda kwa importer hawataki kuniuzia kwa bei ya chini mpka nichukue kuanzia mzigo wa mil 4 ndio wananiuzia kwa bei ya chini na hiyo mil 4 wananipa items moja mfano kama ni ampiclox caps bhasi mil 4 nanunua ampiclox caps tu sio dawa mchanganyiko.kilichobaki nimekuwa mchuuzi sasa naingia k/koo napita kila duka kuangalia duka gani wanauza dawa bei rahisi ndio nanunua.
Duka kidogo linasogea kwa siku faida elfu 90 ingawa elfu 90 ni ndogo mno,Mungu ni mwema naendelea kupambana naamini duka litarudi litakuwa kwenye peak Kama zamani .

NB:biashara ngumu sana aisee

YAANI MILIONI 4 UNUNUE DAWA YA AINA MOJA PEKEE??!!

HUKO NI KUTAKA DAWA ZIJE KU_EXPIRE WAKATI MZIGO UPO MWINGI-
UPATE HASARA.

Sent from my TECNO LC6a using JamiiForums mobile app
 
Suala la msingi kwenye biashara yoyote mpya ni utafiti- hasa kwenye suala la mtaji sahihi wa biashara unayokusudia- biashara nyingi zinakuwa ngumu- kwa sababu ya mtaji kuwa mdogo- kwa hiyo mzunguko unakuwa mgumu- biashara ni mzunguko- ununue- uuze- ununue tena- uuze- Ile faida ijazie mtaji- kwenye starting phase- hutakiwi kula faida kabisa- angalau kwenye growth unaweza kula kwa tahadhali kubwa- ukifika maturity- hapo unajiachia- Mara nyingi starting phase ni mwaka mzima- na growth ni zaidi ya miaka miwili-ukiweza kutenga pesa ya Kodi ya frem ya mwaka unaofata- pamoja na pesa yako ya matumizi ya mwaka mzima bila kuathiri mtaji- na ukawasiliana na supernatural power wako-na location nzuri- biashara ikigoma- basi haikuwa ridhiki





-
Supernatural power...can you add something to this statement?
 
Kitu pekee ninachoweza kushauri watu katika hili:
1. Lazima ujifunze kutambua business location kabla ya ku inject money.
2. Kama pesa umekopa, make sure marejesho ya hiyo pesa haitegemei ustawi wa biashara yako mpya

3. Persistence, hili ni muhimu sana. Wabongo wengi tunafanya biashara kwa hearsay, fremu A leo utaona ni salon, six months later, fremu A utakuta ni duka la nguo za watoto, 9 months later , fremu hiyo hiyo utakuta imekuwa Restaurant.... yaani unaona kabisa hawa watu waliokuwa wanapita humo hawakuwa na long term business strategy and probably walikurupuka na nje ya mategemeo wakajiona kuwa kumbe ni ndoto.

Muhindi akichukua Fremu , basi anakuwa amefanya research ya long term na short term .... na utamkuta hapo hata baada ya miaka 10 na wajukuu zake pia watakuwepo. Na itafika mahali watu wanatoka mbali kuja hapo kupata huduma.

Kwa Experience yangu , a business unatakiwa kuanza kuijudge baada ya miaka 2 yaani 24 months , ndani ya kipindi hicho utakuwa pia wateja wauhakika that is wanakuja hapo kwa ajili yako na service zako.

Sasa wabongo anataka kuijudge biashara baada ya miezi 2, unapotea.

4. Jua mtu wa kumuweka kwenye biashara yako. Hili watu wanalipuuza. Some people hawana mvuto wa kukaa dukani nikiwa na maana kuwa they are irritable na hawana convincing kwa mteja. Unaweza ukaona hakuna biashara kumbe uliyemuweka au wewe Mwenyewe uliyekaa hapo dukani hufai kukaa dukani , huna mvuto kwa wateja or unachukiza Tu jinsi unavowasiliana na wateja hata kama huwajibu hovyo, I mean you are not presentable to customers.

5. Kama Una means , anzisha biashara kwa pesa yako , baada ya miezi kadhaa ya kuona movement na challenge na fast moving items, ndiyo ukakope bank purposely based on the weaknesses you have noticed kwa kipindi husika.

6. All in all biashara ni risk taking , usiogope ku fail , kufail ndiyo kupata Experience Na itakusaidia snaa kwa baadae.

Halafu haya maisha usichukulie SERIOUS sana; end of the day we all gonna die ... and leave everything. So we jaribu unapoweza, ukifeli jifunze, lianzishe tena songa mbele , it is just a game , play it and don’t take it too serious.... kupitia game hiyo , utakuja Tu kupata majibu ya maswali yako na utatoboa.

Keep playing the game , never stop eti kwa kuwa umefeli game ya kwanza.
very nice observation..noted something..stay blessed!
 
Hizi biashara za kuuza bidhaa zinataka moyo sana..
Mimi kuna miaka nilikuwa na biashara ya hardware, nikabebwa na ule ujinga wa vitu vya hardware haviozi, ndio haviozi ila je mzunguko upo?
Kuna items niliweka toka nafungua duka mpka limekuja kunishinda hazijauzika kabisa na hapo ni kama miaka mitatu.
Hizi physical business zimenipa uoga sana, hata kama nitarudi kwenye biashara basi nitafanya services na sio kuuza bidhaa.

Ila cha ajabu watu humo humo wanatoboa na wanafanya mambo makubwa kabisa ukiwa na imani ndogo utasema wanaroga .
Hili ndo la kushangaza aise, biashara iyo iyo kuna waja wanafanikiwa na biashara igo iyo kuna waja wanafeli kbs yani...ndo hapa msemo wa kupata ni majaaliwa unapochukua nafasi yake.
 
Hii ni kwa experience yako Au general!?
Kwangu imefanya kazi
It goes well so far.
Frame paid in advance

kama lengo lako limesimama
Na unajua unachotaka
Izo ulizotaja ni simple challenges.

(mtazamo wangu)
Huwezi lipa frame in advance kka kwa bongo hii Cha msingii kma upo na business ambyo ndio inaianza na waotegemea in running ur life cha msingii tafta biashara ndgo ambyo waifanya kila siku inakuwa Kama part ya biashara means unaweza ukaianza hiyo mfno fungua genge la matunda au kijiwe chchote kaanga samaki kuku broiler au chchote kisichohitaji investment kubwa Wala Mambo y Kody Anza na hichoo Cha msingii iwe biashara ambayo inagusa direct maisha ya watu kwa kila siku ukianza kupta hta 5000 -10000 kwa sikuu Anza biashara yako Sasa
Badae njoo nishukuru
 
Huwezi lipa frame in advance kka kwa bongo hii Cha msingii kma upo na business ambyo ndio inaianza na waotegemea in running ur life cha msingii tafta biashara ndgo ambyo waifanya kila siku inakuwa Kama part ya biashara means unaweza ukaianza hiyo mfno fungua genge la matunda au kijiwe chchote kaanga samaki kuku broiler au chchote kisichohitaji investment kubwa Wala Mambo y Kody Anza na hichoo Cha msingii iwe biashara ambayo inagusa direct maisha ya watu kwa kila siku ukianza kupta hta 5000 -10000 kwa sikuu Anza biashara yako Sasa
Badae njoo nishukuru
Ntakushukuru vipi na hujajua biashara pia!
Bytheway frame ishalipiwa!

kwa ulichosema sijui Kama kinaeleweka.
Yani ili niwe na biashara mpya inabidi niwe na biashara ndogo kwanza!?

kuna biashara isiyogusa maisha!?
Hapo ndio kwenye makosa.
What is that!!?😂

(naheshim wazo lako)

na kwanini kila anaeanza biashara anaita biashara ndogo ndogo!?
Kwanini uanze na fikra ndogo!?

na kama kwako haijafanyakazi haimaanishi wote haijawezekana.

kama uliweka mkakati wako sawa
Ukajua unachotaka hiwezi ita biashara yako ndogo.

kwanza mtaji si pesa Pekee(ingawa ni mhimili mkubwa)
WAZO lako kwanza ni mtaji.
The rest is to get your butt up and work hard

PERIOD.
 
Wazee vipi biashara ya dagaa wakavu toka ziwa victoria hasa mikoa ya Kanda ya kusini,wenye uzoefu na hii watoe ushuhuda hapa
 
Nimefungua fremu ya viatu vya watoto na wanawake siku 8 sijauza hata pair 1, frame laki 2x 6 months!! Naona nyotanyota! Mzigo (gharama)1.5m, leseni+bills (bado sijapigia hesabu). Halafu utashangaa TRA sijui manispaa na ving'ora.

Biashara sasa hivi waru wengi wananunua mtandaoni i mean inst gram anaona kitu anaagiza kupitia inst ukikaa usubiri wateja wa kupita mamaweeh itakula kwako na kama hiyi fremu yako ipo sehemu haiko busy ishakula kwako
 
Biashara sasa hivi waru wengi wananunua mtandaoni i mean inst gram anaona kitu anaagiza kupitia inst ukikaa usubiri wateja wa kupita mamaweeh itakula kwako na kama hiyi fremu yako ipo sehemu haiko busy ishakula kwako
Poa Mama. Ila uswazi hiyo mitandao wanatumia kuchambana SI kununua bidhaa
 
Nilikuwa nafanya biashara kama yako mkoani Morogoro, sikuwa na frame nilikuwa nauzia minadani, minada ya pale Moro town tu, ila bado ilinikata.

Tatizo kubwa lilikuwa kama alivyoeleza Dube hapo juu, yani pesa hiyo hiyo nile,nilipe kodi, maji, umeme, bia, n.k.

Nikafunga vilago kwenda mkoa mwingine kuzisaka.
Mkuu, unaizungumziaje Morogoro mjini kwa kijana anaetaka kwenda kuanza kutafuta maisha kwa upande wa biashara?
 
Morogoro ni mkoa ambao karibia raia wote ni wafanyabiashara sijui mnunuzi atakuwa nani?

Hakuna biashara utaikosa Moro.
Mkuu, unaizungumziaje Morogoro mjini kwa kijana anaetaka kwenda kuanza kutafuta maisha kwa upande wa biashara?
 
Huo ndiyo Ukweli Mkuu!

Nilianza biashara ya M-Pesa kwa miaka 6 iliyopita. Niliweka pesa kama Million 2 tu, baada ya kulipia frame, leseni na kila kitu. Lakini, sikuwa na wazo lolote la kuniletea faida kwa wakati huo.

Mwezi wa kwanza katika biashara nilipata 36,000 tu. Imagine kama ndiyo nilikuwa naitegemea initoe.

Biashara hiyo ilinipigisha kwata miezi nane bila return ya maana. Hata mdada aliyekuwa akinisaidia nammegea sehemu ya Mshahara wangu.

Baadae hali ikachachamaa, mambo yakaanza kuwa mazuri. Angalau sasa malipo ya binti yakaanza kulipwa na Commission. Sipati kitu. Lakini it worth fighting.

Miaka sita sasa, nina mtaji wa zaidi ya Million 40 na sijawahi kutia mia yangu nyingine tangu niweke ile 2M. Imejizalisha mpaka kufika hapo.

Sema nilikuwa sichukui faida. Ikipatikana, narudisha humo humo. 2019 mwishoni ndiyo nikaanza kuchukua Commission inayopatikana huku kiasi kingine nakiacha.

Sasa imagine kama ndiyo nilikuwa naitegemea. Ndani ya miezi mitatu tu hiyo hela ingeshaisha. Kuwa na kipato kingine tofauti kitakachokuwezesha kuishi wewe kama wewe na backup ya biashara yako kama beginner.
Vipi ujio wa tozo za mama haijaathiri hii biashara ya mitandao? Na kama ndio ni kwa kiasi gani?
 
Vya mtumba au special??
Nina biashara ndogo tofauti tofauti kote kuna changamoto lakini angalau biashara ya viatu inalipa, mimi nachanganya mtumba na special ila mtumba ndio unaenda sana, nazungumizia mtumba grade 1, weekend hii liyopita nimechukua mzigo dar nikachanganya na pull meck maana ni maeneo yenye baridi hasa, mzigo ukafunguliwa pale dukani jumanne, ndani ya siku tatu(mpk alhamis) namuuliza muuzaji kaachia pea 70, na pull neck zikawa tayari zimeisha mpk nikajuta kuchukua chache..

Najua moja ya sababu za kuuza kwa haraka ni kua kuna watu wengi walishaweka oda hivyo walikua wanasubiri tuu, ila si kwamba kila siku mambo yanaenda hivyo, inaweza pita hata siku mbili sijauza chochote au uuze pea moja kwa siku, kwa ufupi ni mauzo ambayo kipindi kingine inanichukua mwezi na zaidi kuyafikia, kwahio kushuka au kupanda kwa mauzo ni ka upepo tuu, kikubwa jipe mda pale kabla hujaanza kuhukumu biashara, nakushauri usiwaze kufunga hio biashara mapema, hata mimi nilipitia hapo, na bado kuna siku haziendi vizuri ila najipa mda.

Hili la kutegemea hio biashara ndio ikupe kila kitu ndio kulinifanya nirudishe mpira kwa kipa kwanza, nikamwambia mfanyakazi afunge kwanza sitaweza kumlipa, Kwa kweli kitu ambacho sikuamini Mwenyewe kwa Hiari yake Akasema hapana atauza bila malipo maana anaona kweli ndani hamna kitu ila tukifunga kabisa ndio tutapoteza wateja na pia fursa itaenda na mwingine, aliuza 2 months bila mshahara, mimi ndio nikawa najiongeza kwa uungwana alioonesha, mpk nikaleta mzigo.
Huyu msaidizi wako, Mungu amjalie kwa moyo wake wa kupambana.
 
Wazee wameniachia duka la dawa la jumla lenye mtaji wa mil 15 wakati duka lilikuwa na thamani ya mil 300 yaani nimedata aisee..duka halina items nyingi sana nikienda kwa importer hawataki kuniuzia kwa bei ya chini mpka nichukue kuanzia mzigo wa mil 4 ndio wananiuzia kwa bei ya chini na hiyo mil 4 wananipa items moja mfano kama ni ampiclox caps bhasi mil 4 nanunua ampiclox caps tu sio dawa mchanganyiko.kilichobaki nimekuwa mchuuzi sasa naingia k/koo napita kila duka kuangalia duka gani wanauza dawa bei rahisi ndio nanunua.
Duka kidogo linasogea kwa siku faida elfu 90 ingawa elfu 90 ni ndogo mno,Mungu ni mwema naendelea kupambana naamini duka litarudi litakuwa kwenye peak Kama zamani .

NB:biashara ngumu sana aisee
Kaza mkuu utatoboa kuwa mvumilivu
 
Back
Top Bottom