DaudiAiko
JF-Expert Member
- Dec 2, 2012
- 302
- 274
Wanabodi,
Tumeshuhudia nguvu iliyotumiwa na serikali katika kuhakikisha kwamba kuna tozo kwenye miamala ya kielektroniki inayofanywa na wananchi. Hii inaweza ikawa njia ya serikali kutanua wigo wa kodi ya kuwa wezesha kufanya shughuli zingine za ziada ambazo zinaweza zikawa na manufaa kwa wananchi.
Lakini je, kodi hizi za ziada zinatumikaje na zinaleta manufaa kwa wananchi kwa njia zipi?
kwanza kabisa tukubaliane kwamba mwananchi yeyote wa nchi hii analipa kodi nyingi sana ambazo zinaweza zikawa za moja kwa moja au kwa njia ambayo siyo za moja kwa moja.
Kama umeajiriwa kwenye shirika lolote, utakuwa unalipa "Pay as you earn (PAYE)" na katika shughuli zako zingine ambazo hazina uhusiano na ajira yako, utakuwa unalipa kodi zingine. Kwa mfano: kodi ya majengo, kodi kila unapo nunua bidhaa zozote, kodi kila unapo nunua vocha za simu, kodi kila unapo nunua kifurushi cha intaneti, kodi kila unapo hamisha fedha kutoka kwenye akaunti yako ya benki kwenda kwenye akaunti yako ya M-PESA, tigo pesa n.k.
Hata ukinunua kitu chochote kutoka kwa mtu mwenye biashara yake, hata mwenye biashara lazima naye alipe kodi kulingana na mauzo yake. Kodi kila unapo nunua umeme, kodi kila unapo nunua pombe, kodi kila unapo nunua mafuta, kodi kwenye pensheni yako utakapo staafu, Kodi kila unaposhinda bahati nasibu na kadhalika.
Kwa haraka haraka ni rahisi sana kuona na kuelewa kwamba karibia nusu au zaidi ya mapato ya watanzania yanarudi serikalini. Kitu ambacho nimezidi kutafakari na bado sijapata jibu ni kama mapato haya yanatumiwa kwa ufanisi zaidi kuhakikisha kwamba wananchi wanafaidika kwa njia moja au nyingine.
Kila mwaka, serikali huwasilisha bajeti bungeni katika mchakato ambao huweka wazi matumizi ya serikali kwa kipindi hicho. Kitu cha kushangaza ni kwamba serikali yetu bado haiwezi kumudu kugharamikia bajeti yake kila mwaka na pia kodi katika sekta mbalimbali na bidhaa tofauti tofauti hupanda karibia kila mwaka katika njia inayotumiwa na serikali kuongeza mapato na kutanua wigo wa kodi kwenye sekta ambazo hazikuwa zinatozwa kodi katika kipindi cha awali.
kila mwaka kuna asilimia fulani ya mfumuko wa bei na kwasababu hiyo, ongezeko la kodi kwenye bajeti na ongezeko la mishahara haiendani na uhalisia uliopo mitaani. Je, huu ni ungwana?
Na kama serikali ina mantiki ya kuweka kodi hizo je fedha hizi zote huelekezwa katika miradi ipi?. Ni kweli, kodi inayo kusanywa na serikali haiendani na miradi ya maendeleo inayofanywa.
Tumeshuhudia nguvu iliyotumiwa na serikali katika kuhakikisha kwamba kuna tozo kwenye miamala ya kielektroniki inayofanywa na wananchi. Hii inaweza ikawa njia ya serikali kutanua wigo wa kodi ya kuwa wezesha kufanya shughuli zingine za ziada ambazo zinaweza zikawa na manufaa kwa wananchi.
Lakini je, kodi hizi za ziada zinatumikaje na zinaleta manufaa kwa wananchi kwa njia zipi?
kwanza kabisa tukubaliane kwamba mwananchi yeyote wa nchi hii analipa kodi nyingi sana ambazo zinaweza zikawa za moja kwa moja au kwa njia ambayo siyo za moja kwa moja.
Kama umeajiriwa kwenye shirika lolote, utakuwa unalipa "Pay as you earn (PAYE)" na katika shughuli zako zingine ambazo hazina uhusiano na ajira yako, utakuwa unalipa kodi zingine. Kwa mfano: kodi ya majengo, kodi kila unapo nunua bidhaa zozote, kodi kila unapo nunua vocha za simu, kodi kila unapo nunua kifurushi cha intaneti, kodi kila unapo hamisha fedha kutoka kwenye akaunti yako ya benki kwenda kwenye akaunti yako ya M-PESA, tigo pesa n.k.
Hata ukinunua kitu chochote kutoka kwa mtu mwenye biashara yake, hata mwenye biashara lazima naye alipe kodi kulingana na mauzo yake. Kodi kila unapo nunua umeme, kodi kila unapo nunua pombe, kodi kila unapo nunua mafuta, kodi kwenye pensheni yako utakapo staafu, Kodi kila unaposhinda bahati nasibu na kadhalika.
Kwa haraka haraka ni rahisi sana kuona na kuelewa kwamba karibia nusu au zaidi ya mapato ya watanzania yanarudi serikalini. Kitu ambacho nimezidi kutafakari na bado sijapata jibu ni kama mapato haya yanatumiwa kwa ufanisi zaidi kuhakikisha kwamba wananchi wanafaidika kwa njia moja au nyingine.
Kila mwaka, serikali huwasilisha bajeti bungeni katika mchakato ambao huweka wazi matumizi ya serikali kwa kipindi hicho. Kitu cha kushangaza ni kwamba serikali yetu bado haiwezi kumudu kugharamikia bajeti yake kila mwaka na pia kodi katika sekta mbalimbali na bidhaa tofauti tofauti hupanda karibia kila mwaka katika njia inayotumiwa na serikali kuongeza mapato na kutanua wigo wa kodi kwenye sekta ambazo hazikuwa zinatozwa kodi katika kipindi cha awali.
kila mwaka kuna asilimia fulani ya mfumuko wa bei na kwasababu hiyo, ongezeko la kodi kwenye bajeti na ongezeko la mishahara haiendani na uhalisia uliopo mitaani. Je, huu ni ungwana?
Na kama serikali ina mantiki ya kuweka kodi hizo je fedha hizi zote huelekezwa katika miradi ipi?. Ni kweli, kodi inayo kusanywa na serikali haiendani na miradi ya maendeleo inayofanywa.