Ukifuta picha kwenye simu zinakwenda wapi?

Ukifuta picha kwenye simu zinakwenda wapi?

Mimi naomba mnishawishi kwamba wazungu sio freemason wakati unaweza chaji simu kwa wireless charge
Pili mziki na picha tunatumianaje kwa Bluetooth
Hakuna uchawi wowote simu by wireless

Ni Hadi simu iwe wezeshi means iwe na coil kwa nyuma kupokea magnetic waves hamna uchawi wowote Ni maswala ya kawaida
 
Ukifuta yaani "delete" picha ni kama umeificha tu kwenye simu na unaijulisha simu yako kuwa hiyo nafasi inayotumiwa na hiyo picha inaweza kutumika kuhifadhi kitu kingine. Hiyo picha inaweza kurudishwa kwa kutumia programu mbali mbali, njia pekee ya kuifanya hiyo picha isiweze kurudishwa ni kama ume delete hiyo picha na sehemu (space) iliyokuwa inatumika na hiyo picha ikatumika na faili lingine. Kuna programu zinazofuta kabisa "erase" file, hizo huchukua muda mrefu maana hufuta hiyo picha na kuandika data nyingi kwenye simu au kompyuta ili kupunguza uwezekano wa hiyo picha yako kurudishwa.

Nakumbuka zamani nilikuwa nasaidia watu walioformat flash disk au kufuta file kimakosa, hatua ya kwanza ilikuwa ni kuhakikisha haweki kitu chochote kwenye hiyo flash, kuna programu ukiweka file zote zinarudi.
Hili ndiyo jibu sahihi la swali alilouliza mleta mada.
 
Hata kama hukufanya backup??
WhatsApp huwa ina automatic backup na mara nyingi huwa inaleta tu pop-up page inaonyesha muda wa backup: 1 day, 1 week, 1 month au never. Usipoweka never itafanya backup kulingana na ulivyochagua na watu wengi huwa hawasomi yale maelezo.
 
Inategemea na mambo kadhaa

Simu au pc huwa zina limited storage kuhifadhi data

Kuna data tunazo ziona na kuzitumia kila siku na kuna data zinazo baki kwenye kifaa baada ya kuwa deleted(hizi huzioni)

Kwa bahati mbaya storage ambayo data zilizo kuwa deleted huwa haiwekwi wazi wala kuonyeshwa kwenye storage ya kifaa chako

Mfano ukidelete series ya gb 10 storage ya kifaa chako itaongezeka nafasi

Data zinapokuwa deleted huwa zinabadilika mfumo na zinakwenda kwenye storage ambayo haionyeshwi kwenye kifaa chako
Na storage hiyo huwa inakikomo
Kwa msingi huo kikomo kikifika data zilizo hifadhiwa mwanzoni kabisa zinaanza kufutika mazima kupisha uhifadhi wa data mpya zinazo hifadhiwa

Ili kupada data zilizokuwa deleted ni lazima ziwe hazijawa erased mazima

Kuna details nyingi kitaalamu lakini angalau hii ndio concept yake
 
Hiyo Recycle bin imewekwa ili kurudisha ulichokifuta, actually ni folder tu inayotumika kuhifadhi vitu usivyotumia.

Kama una flash ya 4GB utakuta ina actual space ya 3.7GB na sio 4GB. Hizo 300Mb zipo wapi?? Hizo ndio hua zinatumika kuhifadhi vitu vilivyofutwa. Ukifuta kitu kwenye computer hua kinakua compressed na kutupia kwenye partition maalumu ambazo hua zinatumika kuhifadhi vitu. Ukisoma CPU Architecture ndio unakuta mambo haya.

Hivyo basi kila unachoona kimefutwa hua kipo humohumo kwenye computer ila kinakua compressed na kua na size ndogo sana. Ndio maana wataalam huweza kufanya data recovery
Hio ya flash kuwa na size ndogo kuliko iliyoandikwa kwenye flash mfano 4Gb kuwa 3.7Gb sababu yake ni kama ifuatavyo;

Nitatumia hesabu ndogo mfano kwanini 1 TB inakuwa na usable space ya 931 GB?

Mtengenezaji ametengenesa flash inayo kuwa na 1,000,000,000,000 bytes.

Lakini kwakuwa computer inaitambua 1KB kama 1024 na sio 1000 bytes then naafasi (storage) halisi itapungua na kuwa ndogo;

Tunafahamu kuwa:
1 TB = 1000,000,000,000 Bytes

Lakini kwenye computer, 1000,000,000,000 bytes = 1000,000,000,000/1024 KB. = 976562500 KB.

Vilevile ukichukuwa;
976562500 KB = 976562500/1024 MB = 953674.32 MB.

Alafu itakuwa
953674 MB = 953674.32/1024 GB = 931.32 GB.

1 GB = 1024 MB
1 MB = 1024 KB
1 KB = 1024 B

Hence 931GB

Ndio maana flash drive yenye storage space ya 1Tb storage yake halisi ni 931 GB.

Naomba kuwasilisha na nipo tayari kukosolewa ili nifahamu zaidi.

Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
 
Unajua Bunge la Marekani lilishindwa pata SMS za Secret Service sababu zilifutwa na walijaribu njia zote ikafika mwisho hawakupata kitu
Je, hao bunge la Marekani wana technical capacity kupata hizo taarifa? Na wao ndio waliotengeneza hiyo device yenye hizo SMS?
 
Hio ya flash kuwa na size ndogo kuliko iliyoandikwa kwenye flash mfano 4Gb kuwa 3.7Gb sababu yake ni kama ifuatavyo;

Nitatumia hesabu ndogo mfano kwanini 1 TB inakuwa na usable space ya 931 GB?

Mtengenezaji ametengenesa flash inayo kuwa na 1,000,000,000,000 bytes.

Lakini kwakuwa computer inaitambua 1KB kama 1024 na sio 1000 bytes then naafasi (storage) halisi itapungua na kuwa ndogo;

Tunafahamu kuwa:
1 TB = 1000,000,000,000 Bytes

Lakini kwenye computer, 1000,000,000,000 bytes = 1000,000,000,000/1024 KB. = 976562500 KB.

Vilevile ukichukuwa;
976562500 KB = 976562500/1024 MB = 953674.32 MB.

Alafu itakuwa
953674 MB = 953674.32/1024 GB = 931.32 GB.

1 GB = 1024 MB
1 MB = 1024 KB
1 KB = 1024 B

Hence 931GB

Ndio maana flash drive yenye storage space ya 1Tb storage yake halisi ni 931 GB.

Naomba kuwasilisha na nipo tayari kukosolewa ili nifahamu zaidi.

Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
Unapoteza muda wako kunielezea coz It ndio profession yangu. Hayo unayoeleza niliyaconsider wakati naendika comment yangu
 
Unapoteza muda wako kunielezea coz It ndio profession yangu. Hayo unayoeleza niliyaconsider wakati naendika comment yangu
Sawa mkuu tuendelee kuelimishana
Hizo 300Mb kwaajili ya kuhifadhi deleted data zinapatikaje,, maana kwa hizo hesabu nilizoweka hapo tunaona jinsi storage ya flash drive inavopungua
Naomba kueleweshwa zaidi hapo

Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
 
Hio ya flash kuwa na size ndogo kuliko iliyoandikwa kwenye flash mfano 4Gb kuwa 3.7Gb sababu yake ni kama ifuatavyo;

Nitatumia hesabu ndogo mfano kwanini 1 TB inakuwa na usable space ya 931 GB?

Mtengenezaji ametengenesa flash inayo kuwa na 1,000,000,000,000 bytes.

Lakini kwakuwa computer inaitambua 1KB kama 1024 na sio 1000 bytes then naafasi (storage) halisi itapungua na kuwa ndogo;

Tunafahamu kuwa:
1 TB = 1000,000,000,000 Bytes

Lakini kwenye computer, 1000,000,000,000 bytes = 1000,000,000,000/1024 KB. = 976562500 KB.

Vilevile ukichukuwa;
976562500 KB = 976562500/1024 MB = 953674.32 MB.

Alafu itakuwa
953674 MB = 953674.32/1024 GB = 931.32 GB.

1 GB = 1024 MB
1 MB = 1024 KB
1 KB = 1024 B

Hence 931GB

Ndio maana flash drive yenye storage space ya 1Tb storage yake halisi ni 931 GB.

Naomba kuwasilisha na nipo tayari kukosolewa ili nifahamu zaidi.

Sent from my TECNO PR651H using JamiiForums mobile app
Asante sana, nimejialumu kwa kutotembelea Jukwaa hili muda mrefu tena mara kwa mara!
 
Natamani mtu anayeweza ama kujua hili amalize mjadala kwa kuelezea jinsi inavyowezekana, ama laah hakuna basi tukubali imepotea moja kwa moja
 
Nilikuwa nafanya kazi photography moja hivi town uwa tulikuwa tunasafisha picha, tunapiga piga, tunatengeneza frame za picha na mambo mengi tu ya edit na nk

Nilikuwa nipo reception sometimes natoka naenda operator room, kuna siku kaja mdada akawa anatafuta baadhi ya picha aziprint palee oficen kwetu Na akashindwa kuzitafuta yeye mwenyewe

Akanipa sim nikaiunganisha na laptop kupitia wire cable kazi ikaanza ya kuzitafuta picha zake, wee si ndio nikafika sehemu nikakuta amejichukua picha na video za utupu wee ilikuwa hatari maana tulikuwa tunaangalia wote kwa pamoja tulipokuwa tunatafuta

Alichukua mkono wake kwanza na akauweka begani kwangu na akanambia, sorry kaka angu na kuanza kujielezea kuwa alishazifuta zote na sim aliifrash, akaniomba nimfutie tena na akaniomba nisizicopy, nikamwambia asijali kwani mm nipo kazini na siwezi fanya chochote kibaya na akaniombaga namba yangu ila sikutakaga mazoea nae kabsa

Taarifa zako kwenye sim hazifutiki maana kuna program maalum za kuzirudisha hata kama ukizifuta vipi? Recover zipo za uwezo tofaut za kupata chochote kutoka kwenye sim yako hata kama ukifuta

Be careful
 
Chief-Mkwawa neno lako linahitajika pia.
Hakuna Cha kuongeza mkuu imeshajibiwa huko juu Taarifa hazifutiki, na zinaweza kurudishwa.

Sema unapo overwrite sana inaweza sababisha data za zamani zisipatikane, mfano una Storage ya 32GB, kila siku unaweka movies za 32GB unaangalia ukimaliza unaweka nyengine, baada ya muda storage yako inaweza ikasahau data za zamani. Ila hili nalo sina uhakika nalo maana recovery tool ambazo tunazo sisi sio kila kitu, pengine kuna recovery nyengine ambazo taasisi za usalama wanazo zenye uwezo zaidi.
 
Navojua mfano memory yangu ilizingua nikakosea ingiza vitu vingne vipya (overwrite) vile vingne Ni ngumu kupata
 
Back
Top Bottom