Ukifuta yaani "delete" picha ni kama umeificha tu kwenye simu na unaijulisha simu yako kuwa hiyo nafasi inayotumiwa na hiyo picha inaweza kutumika kuhifadhi kitu kingine. Hiyo picha inaweza kurudishwa kwa kutumia programu mbali mbali, njia pekee ya kuifanya hiyo picha isiweze kurudishwa ni kama ume delete hiyo picha na sehemu (space) iliyokuwa inatumika na hiyo picha ikatumika na faili lingine. Kuna programu zinazofuta kabisa "erase" file, hizo huchukua muda mrefu maana hufuta hiyo picha na kuandika data nyingi kwenye simu au kompyuta ili kupunguza uwezekano wa hiyo picha yako kurudishwa.
Nakumbuka zamani nilikuwa nasaidia watu walioformat flash disk au kufuta file kimakosa, hatua ya kwanza ilikuwa ni kuhakikisha haweki kitu chochote kwenye hiyo flash, kuna programu ukiweka file zote zinarudi.