Ukifa, hutatamani tena kuishi duniani!

Ukifa, hutatamani tena kuishi duniani!

Ndiyo, swali ni uhakika gani ulio nao kuwa internal observer huwa inazima kabisa?

Vipi kama huwa hailali wala kuzima?
Huenda sijaelewa hiyo internal observer unayoizungumzia. Hebu fafanua jinsi hiyo internal observer inavyofanya kazi.
 
natamani niache wosia nichomwe moto usiku km hv huko kaburini sijui itakuwaje nikiwakumbuka wapendwa wangu na jf daaah sijui wale wachaga watakubali?
Siyo mpaka uchomwe, unaweza ukajichoma. Kwani petroli na kiberiti TSH ngapi?
 
Wewe mawazo yakounafanana na mawazo yangu .Je wajua kuwa katika maisha ni siku mbili tu ambazo mwanadamu haishi masaa 24, siku ya kuzaliwa kwake na siku ya kufa kwake.
Well said mkuu, japo watakuja kukupinga.
 
Kifo si mwisho wa mchakato wa uhai wetu, bali ni mlango mtakatifu unaofungua ukurasa wa mwanzo mpya na wa milele.

Mwili wa nyama unaporudi mavumbini na kukamilisha safari yake ya kibiolojia, roho haifi; inavua vazi hili la udongo lenye mipaka, maumivu, na machozi, tayari kuvuka ng’ambo ya mto wa uzima.

Huu ni wakati wa kiroho ambapo nishati ya kimungu iliyomo ndani yetu inarejea kwenye chanzo chake kikuu, ikiwa imeandaliwa kuanza safari mpya katika ulimwengu wa utukufu na mwanga usiotiwa giza.

Katika hatua hii, fahamu yetu haizimiki bali inalindwa na kufanywa upya, ikisafiri kwa amani kuelekea maskani ya milele ambako hakuna tena muda, uzee, wala uharibifu, bali ukamilifu wa upendo wa kimungu.
Hizi ni nadharia tu, practically no one can tell.
 
Back
Top Bottom