Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Mkuu wa nchi amekataza siasa kwanini ajaribiwe? Kwani msipovaa hayo mashati ya kijani mtaonekana hamkwenda kuzika?

Mkuu wa nchi anakataza siasa lakini yeye ndio kinara wa siasa. Asichotaka na kuweza ni siasa za ushindani. Ila ukifanya siasa kwa mgongo wa ccm hana shida, kwake na wanaccm wenzake siasa zinaanzia pindi cdm na cuf wakijiingiza kwenye jambo. Sasa kama yeye alipokea makada waliohama upinzani na kuhamia ccm kwenye hafla ya kijeshi unategemea nini?
 
Sasa unaweza kuwazuia watu wasivae vile wanajisikia siku hiyo, acheni siasa kwenye mambo yanayowaumiza wengine

Hivi unafahamu watu walivaa tshirt ya Lissu na kutaka kumuombea, kodi za wananchi zikatumika kutuma polisi kuvuruga hilo huku kila aliyekutwa Amevaa tshirt ya Lissu akaishia police?
 
Siasa Tanzania Inatia Kinyaa Yaani Kila Uchao Hadi Eneo Lisilohitaji Siasa Watu Wanaingiza

Tuvumiliane
 
Daaah Mkuu maelezo yako yamenihuzunisha sana. Watu wanaropoka humu kwa kutetea ujinga kwa sababu tu hawajaondokewa na Ndugu zao .
 
Ni vema angekaa kimya kuliko kutangaza usitishaji wa uokoaji.Kama kuna watu wameokolewa siku mbili baada ya tukio je tungeendelea na uokoaji tungeokoa wangapi?
 
Tupo standby tunasubiri uchambuzi wako.
ova
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…