Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Timu ya uongozi wa CCM yenye wajumbe sita inayoongozwa na Kanali mstaafu Ngemela Lubinga na Ndg. Humphrey Polepole ambao ni wakuu wa idara za CCM Makao Makuu na katibu wa UVCCM Taifa Mwl Raymond Stephen Mwangwala, tayari imewasili na kuweka kambi mkoani Mwanza wilaya ya Ukerewe katika kisiwa cha Ukara ili kuhakikisha mambo yote yanayoendelea kusimamiwa na Serikali yanakwenda vizuri ikiwa ni pamoja na kuhakikisha majeruhi wanapatiwa matibabu ya haraka pamoja na wale wote ambao wamepoteza maisha kuhakikisha kuna kuwepo na utaratibu mzuri wa kuwasitiri na kuwahifadhi.


#WapumzikeKwaAmani #PoleTanzania
IMG-20180923-WA0037.jpeg
IMG-20180923-WA0040.jpeg
IMG-20180923-WA0044.jpeg
 
Mkuu, mfariji pekee kwenye jambo kama hili na asiye mnafiki ni MUNGU. Tumwombe kwa nguvu zote, atoe faraja na roho za matumaini mapya kwa waliopotelewa na Ndugu zao na wale majeruhi wapone haraka. Sisi binadamu ndo muda wa kujionyesha mara nyingi kinafiki sana kana kwamba hili suala ni la mtu mmoja au wa aina fulani, ndo wao tuu waongee!!!! Wengine wataambiwa wanaongea siasa!! Duu, sijawahi ona haya mambo!! Msiba ni wa Taifa, watu wawe huru kutoa maoni yao ili tupate machungu au faraja, tuone la kufanyia kazi ili kesho yasitusibu tena!!!!
Nakumbuka hapo nyuma kidogo, jambo kubwa kama hili kunakuwa na coverage kubwa ya viongozi wa kitaifa, kivyama, kidini kupewa fursa kutoa maoni.
Mfano kuna clips nyingi zisizo rasmi kwenye you tube, mpaka wenyeviti wa vijiji wanasema,walishaomba siku nyingi na kupiga kelele kuhusu kurekebishwa usafiri wa eneo hilo.
Nimemsikiliza mzee mmoja ,nafikiri ni Bugora pale alishauri mambo 3.
1. Kivuko kile kiongeze safari , ziwe 4 badala ya 1 au 2 kwa siku ili kupunguza mlundikano.
2. Waliomba zamani tuu, waletewe kivuko kukubwa au kuongezewa kivuko kingine kukidhi ongezeko la idadi ya wasafiri na mizigo
3. Kuwe na soko jingine kule Ukara kupunguza idadi ya wanaovuka kwenda kuhemea Bugorora.
Najiuliza, kutisha mtu kama huyu ili asitoe maoni, yawafikie wadau wengine ni jambo jema? Na je, hiyo nayo ni siasa?
Ninafikiri, Nia ya Raisi wetu ni njema sana, huenda tunaangushwa sana na watendaji wake. Na huenda ndo maana, anajtahidi kwa kiasi chake,afanye ziara nyingi ajionee mwenyewe hali halisi. Pia aliyasema mengi akiwa Simiyu namna mambo mengine hapewi ukweli.
Magufuli ndo mtoa vitisho namba moja hao wengine wana muiga.
 
Ungekuwa wewe ungewalazimisha divers
Soma vizuri utanielewa.

Divers walikwepa jukumu lao au kwa uzembe, au kwa kukosa vifaa au kwa kukosa maarifa. Tuna wataalam wasio na utaalam. Haikutosha kwa RC kuwakubalia tu bali ilibidi wapatikane watu wenye uwezo.

Fuatilia taarifa za uokoaji. Karibu wote 40 walioopolewa hai waliokolewa na wavuvi na siyo wataalam wa serikali.
 
Una utaalam wa masuala ya Diving mkuu!?
Au unajaza server za JF na wewe uonekane! Kuna masuala ni ya kitaalam na hayahitaji Siasa na mihemko.
Mkuu wa mkoa alishauriwa na wataalam (Divers) kusitisha zoezi hilo kutokana na hali iliyojitokeza ndani ya maji.
Hayo masuala ya mke wako sijui mke wa jirani yaache huko huko kwenye vijiwe vya kahawa.
Divers waliogopa giza! WTF!
 
Hapa ndipo kama nchi tunapokuwa wapumbavu kwa ujumla wetu.
Siku ya alhamis SAA 1.22 jioni nikiwa eneo la tukio nilimuona na kumsikia Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela akitangaza kusitisha zoezi la uokozi kwa sababu ya giza. Na nikiri wazi sikumsikia akisema ameshauriwa na wataalamu au yalikuwa mawazo yake. Wakati anatoa tangazo lake kulikuwa na divers ndani ya kivuko ambao walitoka na miili kadhaa saa mbili kasoro hivi. Mara baada ya kutangaza kusitishwa kwa zoezi vilio vilisikika mwaloni toka kwa ndugu waliokuwa na matumaini labda kuna watu wako hai ndani. Baada ya kusoma mawazo ya waombolezaji Mkuu wa wilaya ya Ukerewe akalazimika kutuliza hali ya hewa kwa kusema, namnukuu; Ndugu zangu katika hali ya kawaida mtu hawezi kukaa ndani ya maji kwa masaa zaidi ya manne bado akawa hai kama hana vifaa vya kumsaidia kupumua, Sisi viongozi wenu tuna huzuni kama ninyi lakini kazi hii haiwezi kufanyika gizani, mwisho wa kunukuu". Kwa vile watanzania huwa tunaona kauli za viongozi ni kauli za mbingu wengi walitii lakini wachache wenye uchungu walitoa hoja wakaonekana wabishi mbele ya viongozi. Hilo ziwa lililochafuka SAA 1 jioni hapa Ukara ni lipi? Au waliondoka nalo sisi hatukuliona? Kivuko kimezama chini ya mita 100 toka ufukweni, wazoefu wa ziwa mnajua vizuri, hivi hata ziwa likichafuka kwa umbali huo na kwa watu wenye vifaa watashindwa kuendelea na kazi?
Kesho yake baada ya kelele za wananchi na mitandaoni zoezi lilifanyika hadi usiku siku ya Ijumaa. Hizi sababu za ziwa kuchafuka tumeanza kuzisikiaIjumaa jioni baada ya Waziri Mkuu kuwepo na walikuwa wanaongea kama kujikosha tu na Leo ndo zimeletwa hapa kama sababu rasmi.
Siasa zinatufanya watanzania tukose mawazo ya kuhoji hata vitu vya msingi. Nawashangaa vijana wa ccm mitandaoni mnavyokosa utu na kushabikia makosa ya kiutendaji kwa vile tu aliyekosea ni wa Chama chenu. Sidhani kama kuna mwanaccm mwenye uchungu na aliyepotelewa na ndugu/jamaaa/rafiki kama ilivyonitokea Mimi anayeweza kuunga mkono mawazo yenu. Mimi nilisafiri Jumanne na kivuko hicho hicho na alhamis kikapata ajali, lakini maneno ya usalama mdogo ndani ya kivuko yalikuwepo, na bado tulijaa ingawaje si kama siku ya gulio Bugolora. Siku za Gulio mpaka mitumbwi toka Chifule na Chibasi huwa inasadia kutokana na wingi wa watu.
Mbunge wa Ukerewe kawa mkweli kwamba kivuko kilifanyiwa ukarabati, napo ni kuwekewa injini mpya tu na hoja kuu hata kwenye baraza za madiwani ni kupatiwa kivuko kipya na kikubwa zaidi.
Acha nikae kimya Nina majonzi.
 
Kwa mara nyingine CCM imenunua msiba ambalo ulitarajiwa ufanyike kiserikali bila jezi za kijani. Kwenye eneo la maziko nguo za kijani zimeanza kutawala na ni za haohao wanaoshauri tuache tofauti za kiitikadi za kisiasa! Hali hii ndiyo inayotufarakanisha watanzania na lawama wanapewa wanaotengwa!
Mbona Mbowe alivaa gwanda alipoongea na waandishi wa habari, hukuona hilo?
 
Uchafu huu sio tu kuwaajibisha watu wachache hapa kuna donda ndugu la shughuli ya vyombo vya majini ni kukubali makosa tukajipanga upya.
Tupo baadhi yetu ni wadau au wanataaluma kwa muda mrefu tumejaribu bila mafanikio ya kushauri uwepo wa vyombo/taasisi chache na imara,lakini sababu ya ubinafsi na uroho,baadhi ya shughuli hizi zinaendeshwa kwa maslahi ya watu waovu.
Kuna wakati maamuzi yenye tija kwa taifa yamepigwa dana dana au kupindishwa na hao wakorofi.
Matokeo yake tunaendelea kuona matamko na maazimio lukuki baada ya ajali,lakini ikipita miezi 6 wanasahau tunarudi kule kule.Na hii ndio Tanzania ya kutowajibika hakuna nidhamu ya kazi.
 
Mongela wasamehe bure.Hizo ni hasira na frustrations zao za kushindwa chaguzi wameaamua KU STEAM OUT FRUSTRATION zao kwenye hiyo ajali.

Wamegeuka ghafla wasomi na wataalamu wa vivuko.Nyoooo!!!! wangekuwa wasomi na wataalamu si wangetumia usomi na utaalamu wao kushinda chaguzi?. Wakshindwa chaguzi hata za udiwani tu hugeuka na kujifanya wasomi na wataalamu waliobobea wa ku analyize mambo ya kitaifa na kimataifa!!!! ha ha ha ha
Walioshindwa uchaguzi sio mbowe, zitto wala mbatia. Ni wananchi ndio walioshindwa uchaguzi. Najua hutaelewa
 
Kwa mara nyingine CCM imenunua msiba ambalo ulitarajiwa ufanyike kiserikali bila jezi za kijani. Kwenye eneo la maziko nguo za kijani zimeanza kutawala na ni za haohao wanaoshauri tuache tofauti za kiitikadi za kisiasa! Hali hii ndiyo inayotufarakanisha watanzania na lawama wanapewa wanaotengwa!
Kweli tuna matatizo ya kuchambua mambo kwani wanaposema tusiweke mambo ya siasa na mambo ya vyama wana maana ya watu wasivae nguo za vyama vyao? Nadhani hapo kuna shida ya kutafakari mambo
 
Soma vizuri utanielewa.

Divers walikwepa jukumu lao au kwa uzembe, au kwa kukosa vifaa au kwa kukosa maarifa. Tuna wataalam wasio na utaalam. Haikutosha kwa RC kuwakubalia tu bali ilibidi wapatikane watu wenye uwezo.

Fuatilia taarifa za uokoaji. Karibu wote 40 walioopolewa hai waliokolewa na wavuvi na siyo wataalam wa serikali.
Vipi hao divers wangelazimishwa na mkuu wa mkoa alafu wakaenda kufa ,vipi usingekuja kumlalamikia mkuu wa mkoa kwa kushindwa kusaidia wataalam??
 
Sasa unaweza kuwazuia watu wasivae vile wanajisikia siku hiyo, acheni siasa kwenye mambo yanayowaumiza wengine
 
Back
Top Bottom