Ukara, Ukerewe: Kivuko cha MV Nyerere chazama, miili 229 ya waliopoteza maisha imeshaopolewa!

Una utaalam wa masuala ya Diving mkuu!?
Au unajaza server za JF na wewe uonekane! Kuna masuala ni ya kitaalam na hayahitaji Siasa na mihemko.
Mkuu wa mkoa alishauriwa na wataalam (Divers) kusitisha zoezi hilo kutokana na hali iliyojitokeza ndani ya maji.
Hayo masuala ya mke wako sijui mke wa jirani yaache huko huko kwenye vijiwe vya kahawa.
Mkuu, sijapingana na Mkuu wa Mkoa ila napingana na mtu kama wewe. Wewe ni Diver?
 
Wanasiasa hatar badala ya kujiuzuru kawageuzia kibao wataalam dah, hatutoendelea miaka 800 kwa akili hizi ambazo kwao maendeleo ni kuweka matuta yenye uwazi ambayo wanadai kuwa ni flaiova
 
Ndugu wanabodi;
Ajali ya MV Nyerere imeleta msiba wa kitaifa ambapo zaidi ya Watanzania wenzetu 225 wamepoteza maisha.

Idadi hiyo ni kubwa sana kwa taifa letu. Hivyo ni matarajio yangu kuwa hill si suala LA kutuma uwakilishi Bali viongozi wote wa kitaifa wa vyama vya siasa,madhehebu ya dini na taasisi binafsi wakiongozwa na Rais wa JMT walipaswa kuhudhuria.

Sasa ukipeleka uwakilishi kwenye jambo kubwa la kitaifa kama hill yaani wewe unakuwa na jambo gani la kitaifa jingine?

Namshauri Rais afike Ukara yeye mwenyewe asisimuliwe na MTU ktk hili.Nawashauri viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa wafike wenyewe Ukara wasipige lamli wakiwa DSM.

Tukishindwa kuonesha umoja wetu kama Watanzania ktk hili tutaonesha maadili na umoja wa Utanzania wetu ktk lipi?

Nasisitiza tena Rais ufike Ukara,tena ktk kipindi hiki cha majonzi vinginevyo Mimi kama RAIA mwema nitaona umelichukulia janga hili sio kwa uzito unaostahili.Nakumbuka ulivyowatembelea wagonjwa na majeruhi mbalimbali huko muhimbili .Naamini hata ktk hili utafika huko Ukara kuwafariji wafiwa ktk kipindi hiki hiki cha majonzi na si muda mwingine.

Nasisitiza tena viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa,madhehebu ya dini na taasisi mbalimbali mnapaswa kufika Ukara kufariji wafiwa ktk kipindi hikihiki cha majonzi. Hii itasaidia kudumisha maadili yetu kama Watanzania na kuonesha mshikamano wetu kama taifa ktk shida na raha.
 
Hapa ndipo kama nchi tunapokuwa wapumbavu kwa ujumla wetu.
Siku ya alhamis SAA 1.22 jioni nikiwa eneo la tukio nilimuona na kumsikia Mkuu wa Mkoa wa Mwanza John Mongela akitangaza kusitisha zoezi la uokozi kwa sababu ya giza. Na nikiri wazi sikumsikia akisema ameshauriwa na wataalamu au yalikuwa mawazo yake. Wakati anatoa tangazo lake kulikuwa na divers ndani ya kivuko ambao walitoka na miili kadhaa saa mbili kasoro hivi. Mara baada ya kutangaza kusitishwa kwa zoezi vilio vilisikika mwaloni toka kwa ndugu waliokuwa na matumaini labda kuna watu wako hai ndani. Baada ya kusoma mawazo ya waombolezaji Mkuu wa wilaya ya Ukerewe akalazimika kutuliza hali ya hewa kwa kusema, namnukuu; Ndugu zangu katika hali ya kawaida mtu hawezi kukaa ndani ya maji kwa masaa zaidi ya manne bado akawa hai kama hana vifaa vya kumsaidia kupumua, Sisi viongozi wenu tuna huzuni kama ninyi lakini kazi hii haiwezi kufanyika gizani, mwisho wa kunukuu". Kwa vile watanzania huwa tunaona kauli za viongozi ni kauli za mbingu wengi walitii lakini wachache wenye uchungu walitoa hoja wakaonekana wabishi mbele ya viongozi. Hilo ziwa lililochafuka SAA 1 jioni hapa Ukara ni lipi? Au waliondoka nalo sisi hatukuliona? Kivuko kimezama chini ya mita 100 toka ufukweni, wazoefu wa ziwa mnajua vizuri, hivi hata ziwa likichafuka kwa umbali huo na kwa watu wenye vifaa watashindwa kuendelea na kazi?
Kesho yake baada ya kelele za wananchi na mitandaoni zoezi lilifanyika hadi usiku siku ya Ijumaa. Hizi sababu za ziwa kuchafuka tumeanza kuzisikiaIjumaa jioni baada ya Waziri Mkuu kuwepo na walikuwa wanaongea kama kujikosha tu na Leo ndo zimeletwa hapa kama sababu rasmi.
Siasa zinatufanya watanzania tukose mawazo ya kuhoji hata vitu vya msingi. Nawashangaa vijana wa ccm mitandaoni mnavyokosa utu na kushabikia makosa ya kiutendaji kwa vile tu aliyekosea ni wa Chama chenu. Sidhani kama kuna mwanaccm mwenye uchungu na aliyepotelewa na ndugu/jamaaa/rafiki kama ilivyonitokea Mimi anayeweza kuunga mkono mawazo yenu. Mimi nilisafiri Jumanne na kivuko hicho hicho na alhamis kikapata ajali, lakini maneno ya usalama mdogo ndani ya kivuko yalikuwepo, na bado tulijaa ingawaje si kama siku ya gulio Bugolora. Siku za Gulio mpaka mitumbwi toka Chifule na Chibasi huwa inasadia kutokana na wingi wa watu.
Mbunge wa Ukerewe kawa mkweli kwamba kivuko kilifanyiwa ukarabati, napo ni kuwekewa injini mpya tu na hoja kuu hata kwenye baraza za madiwani ni kupatiwa kivuko kipya na kikubwa zaidi.
Acha nikae kimya Nina majonzi.
Cc Drlove66
 
Wanasiasa hatar badala ya kujiuzuru kawageuzia kibao wataalam dah, hatutoendelea miaka 800 kwa akili hizi ambazo kwao maendeleo ni kuweka matuta yenye uwazi ambayo wanadai kuwa ni flaiova
Mbowe amejihuzuru baada ya chama kunyauka??
 
Kwa sasa Taifa linaomboleza kutokana na Kilichotokea huko Mwanza.
Wengi wetu tumekuwa na Kasumba za Kuchukulia Vitu kwa kawaida(Mazoea), ajali hiyo imetokana na Uzembe wa Wathirika, kushindwa kugundua na kuthamini Maisha yao kutokana na tatizo la mazoea "(HUWA) tunapanda usafiri hivi" , Lazima jamii zetu ziweze kugundua kuwa Maisha hayana spare hivyo Hatuna budi kuchukua tahadhali na Kujithamini sisi na Wenzetu. Kama chombo cha Usafiri kimejaa ni vyema ukavuta Subira ukapata kheri kuliko Harakaharaka Isiyo na Baraka. Kama watu wangalikuwa wanalijua hili vifo vya kizembe kama vile Visingalitokea.


Mamlaka za Usafiri pia zinapashwa kutoa Elimu kwa raia na Kuwaajibisha Wavunja Sheria
Kama hizi mamlaka zingalikuwa makini basi wangaliweza kuzuia hili lisitokee, kwq vile watumishi wa hizi mamlaka ni wanajami wenzetu ambao wamezoea kuchukulia mambo kirahisi .


Maeneo kama ya Kariakoo na kwingineko watu wamezoea kupanda Usafiri kwa fujo ama kukimbilia Gari inakuja, nionavyo zile tabia za Mazoea zitakuja kemewa endapo watu wakipoteza maisha. Tahadhali ni Bora kuliko Tiba kama tukiendelea na Tabia hizi tulizojijengea tutaendelea kupoteza ndugu zetu na Kuishia Kubandika picha za Mishumaa Mitandaoni.
 
Mimi sioni kama waliyopakia watu wanatatizo lolote kwasababu akuna abiria ata mmoja aliyelazimishwa kupanda hiyo feri ikiwa imejaa mimi mwenyewe nikiona kitu hiki ni hatari siwezi kufanya kwasababu natambua kuishi ni mara moja tu siwezi kubet maisha yangu ila waliyopanda feri ikiwa imejaa walikuwa na akili timamu kabisa wala awakulazimishwa kupanda iweje walaumiwe wao
Ni elimu tunayotakiwa kupeana, na pia mamlaka husika kuchukua hatua stahiki kwa weledi na haki. Mfano, ikiwa imesemwa katika sheria kuwa mtumiaji wa barabara ana wajibu wa kulinda usalama wake na watumiaji wengine basi hili linahusu mtembea kwa miguu, mwendesha baskeli, pikipiki na gari. Naeleza hivi kwa kuwa nimeona nchi nyingine mtembea kwa miguu akivuka barabara sehemu isiyo na alama ya kuvukia akipatikana anapewa adhabu. Kwenye gari ndogo dereva wa gari alilopanda mtu asiyefunga mkanda adhabu ni kwa wote. Hapo na sisi tungelikuwa na utaratibu huo mtu asingelikubali kupigwa faini kwa kosa la kupanda chombo kikiwa kimejaa.
 
Ndugu wanabodi;
Ajali ya MV Nyerere imeleta msiba wa kitaifa ambapo zaidi ya Watanzania wenzetu 225 wamepoteza maisha.

Idadi hiyo ni kubwa sana kwa taifa letu. Hivyo ni matarajio yangu kuwa hill si suala LA kutuma uwakilishi Bali viongozi wote wa kitaifa wa vyama vya siasa,madhehebu ya dini na taasisi binafsi wakiongozwa na Rais wa JMT walipaswa kuhudhuria.

Sasa ukipeleka uwakilishi kwenye jambo kubwa la kitaifa kama hill yaani wewe unakuwa na jambo gani la kitaifa jingine?

Namshauri Rais afike Ukara yeye mwenyewe asisimuliwe na MTU ktk hili.Nawashauri viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa wafike wenyewe Ukara wasipige lamli wakiwa DSM.

Tukishindwa kuonesha umoja wetu kama Watanzania ktk hili tutaonesha maadili na umoja wa Utanzania wetu ktk lipi?

Nasisitiza tena Rais ufike Ukara,tena ktk kipindi hiki cha majonzi vinginevyo Mimi kama RAIA mwema nitaona umelichukulia janga hili sio kwa uzito unaostahili.Nakumbuka ulivyowatembelea wagonjwa na majeruhi mbalimbali huko muhimbili .Naamini hata ktk hili utafika huko Ukara kuwafariji wafiwa ktk kipindi hiki hiki cha majonzi na si muda mwingine.

Nasisitiza tena viongozi wa kitaifa wa vyama vya siasa,madhehebu ya dini na taasisi mbalimbali mnapaswa kufika Ukara kufariji wafiwa ktk kipindi hikihiki cha majonzi. Hii itasaidia kudumisha maadili yetu kama Watanzania na kuonesha mshikamano wetu kama taifa ktk shida na raha.
Angalia live sasa hivi
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Nchi hii ya maajabu, ilipozama MV Bukoba kuliundwa hadi kamati ya maafa, chini ya Waziri Mkuu. Leo hii wamekosa hata boat zenye mataa ya kumulika usiku wanategemea za wavuvi, halafu wanatutisha tusiwahoji! Only in Africa. Ajali zipo ila hii ya kujitakia, mnataka kutwambia CHADEMA ndio wamewaambia SUMATRA wawe bize Ubungo tu na barabarani na matochi yao na kusahau na Marine ni wao! Wapo bize Dar huko mikoani mjiendeshe wenyewe.
Wanatulazimisha tunyamaze na kututishia Polisi, siku moja nasi tutakuwa na nguvu kama hao Polisi tuone mwisho wake.
Kwa nini SUMATRA hawasimamii udadi ya abiria na mizigo inayobebwa na vyombo vya majini? Au hawa SUMATRA ni wapinzani? Najaga!
 
Mongela wasamehe bure.Hizo ni hasira na frustrations zao za kushindwa chaguzi wameaamua KU STEAM OUT FRUSTRATION zao kwenye hiyo ajali.

Wamegeuka ghafla wasomi na wataalamu wa vivuko.Nyoooo!!!! wangekuwa wasomi na wataalamu si wangetumia usomi na utaalamu wao kushinda chaguzi?. Wakshindwa chaguzi hata za udiwani tu hugeuka na kujifanya wasomi na wataalamu waliobobea wa ku analyize mambo ya kitaifa na kimataifa!!!! ha ha ha ha
hivi ww jamaa akili zako huwa zipo sawa!hivi kwa akili yako kweli unaacha watu wafe eti kisa huko chini ya maji kuna hali mbala??
 
Mongela wasamehe bure.Hizo ni hasira na frustrations zao za kushindwa chaguzi wameaamua KU STEAM OUT FRUSTRATION zao kwenye hiyo ajali.

Wamegeuka ghafla wasomi na wataalamu wa vivuko.Nyoooo!!!! wangekuwa wasomi na wataalamu si wangetumia usomi na utaalamu wao kushinda chaguzi?. Wakshindwa chaguzi hata za udiwani tu hugeuka na kujifanya wasomi na wataalamu waliobobea wa ku analyize mambo ya kitaifa na kimataifa!!!! ha ha ha ha
Ajali hizi zinaletwa na wataalam badala ya kutumia nyenzo za kitaaluma mume walazimisha kutembea na ilani na kuzitumia
 
Back
Top Bottom