Ujumbe wa Mengi katika Twitter, kejeli kwa Prof. Muhongo?

Ujumbe wa Mengi katika Twitter, kejeli kwa Prof. Muhongo?

Jana Mr Reginald Mengi alipost kwenye Istagram yake kwamba kuna Mtu aliwahi kurudia la Saba mara tau na leo ni Le Porofeseri bila shaka akimaanisha Sospeter Muhongo

Je ana hoja>?

Mh inawezakua hakumlenga muhongo ila kutokana na upepo huu ndo inakua nshu
 
kwenye hizo comment nimesoma wengine wanasemq ni mkuu,Dr Profesa...
 
Mengi anazeeka vibaya, muda sio mrefu atakuwa mchawi, huwezi kumchukia binad mwenzake kiasi hicho kisa kitalu cha gesi

Hela ya kuwekeza kwenye kitalu cha gesi hana,muhongo kamwambia ukweli kwamba hana hela,hela yake ni ya juisi na maji,watanzania hawataki kuambiwa ukwei,ukiwaambia ukweli wanadai umewatukana.
 
Ndo maana nampongeza mhe: Rais suala pr Muhongo kulichukulia umakini wa hali ya juu maana mabepari waliumia kuambiwa ukweli wakitaka waachiwe wakafanye jujalee zao Hongera Jk ,Angalia majungu yao ,wengine tuliumizwa Zanzibar kwa Ufisadi wa Watu tu ,na hatuna hatia Mzee.
 
Tatizo sio kurudia mara 3,tatizo la Prof. ni kujifanya "GENIOUS". Mtu mwenye akili zisizo za kawaida na kudharau wengine. Sasa hilo ni "DONGO". Kama yeye ameungaunga na kufika hapo alipo iweje awakebehi wengine, au kuungaunga ni kwenye kusoma tu kwenye biashara hakuna ruksa.
 
Mengi Hakutakiwa kutumia maneno yale... Kiungwana, kibusara, kihekima alitakiwa awasilishe ujumbe wake kwa maneno haya "Tujitathimini tulipofika na nyazifa tulizonazo kisha tukumbuke tulikotoka, na tunyenyekee".

Umeongea vyema, ila hii ni kauli ya kwenye nyumba za ibada mkuu. Huku beleshi linaitwa beleshi.
 
Sasa Tanzania kama hujaungaunga shule za kata ungetokaje na wewe siyo mtoto wa mwalimu,miaka ya 90 huko shule ya msingi yote anaweza asifaulu hata mmoja watu wanarudia japo wafaulu,kwahiyo mheshimiwa kurudia primary sishangai

Kwa SASA ni kweli- kama ni mtoto wa maskini lazima uunge uunge shule. Lakini enzi za Mwl Nyerere, nafasi za kusoma sekondari zilikuwa haba sana lakini watoto wote walipata elimu- elimu ilikuwa bure. Kusogea kwako ilikuwa ni jitihada zako mwenyewe. Yumkini waliofaulu kwenda sekondari ni wale waliokuwa wamepata alama za juu sana. Kwa ajili hio kama mtu alirudia rudia ni kwa kuwa hakuweza kufikia alama zilizohitajika.

Na kulikuwepo na sera ya upendeleo maalumu kwa mikoa ambayo ilikuwa imeachwa nyuma kutokana na sera za mkoloni. Katika mikoa hii alama za ufaulu zilikuwa chini kidogo kulingana na Mikoa iliyokuwa na wasomi wengi kama Kilimanjaro, Mbeya na Kagera. Tena ni vizuri kukumbuka mwanafunzi aliyepasi alipangwa shule nje ya mkoa aliyosoma- hii ilikuwa sera mahususi ambayo imejenga utaifa wetu tunaojivunia.

Sasa kama Mheshimiwa alisoma huko Musoma (ambapo ilikuwa katika ile mikoa iliyofaidika na upendeleo maalumu kwa kuwa na alama za ufaulu chini ya zile za mikoa iliyotajwa hapa juu) basi huyu ama kweli ni kama Maskini akipata.... Na inaweza ikawa ndio kielelezo cha kiburi chake - arrogance.

Wapo maprofesa wengi wa miaka ya 70 na 80 ambao kwa sababu mbalimbali licha ya kufanya vizuri sekondari walichagua kutoendelea chuo kikuu ili waweze kuanza kazi mapema na kusaidia familia. Hawa walikwenda moja kwa moja kufundisha shule za msingi na baadae walirudi kusoma vyuo vikuu na kuendelea kutesa. Kwa wale wa UDSM watamkumbuka Mzee Prof Masenge - wa Hisabati, Prof Kimambo wa Historia- au Prof Phile Mushi wa Elimu na wengi wengine ambao utaona CV zao ni walimu wa Msingi, Sekondari halafu wahadhiri Chuo Kikuu. Hawa walikuwa hodari sekondari -walipata alama za juu shule za awali lakini walikatiza masomo- na waliporudi na hata kuupata uprofesa, huwasikii wakijivuna hata mara moja
 
huu utakuwa ushauri wa mke wake

Definetely kwa sababu enzi hizo si ajabu hata yeye si Reginald....alirudia. Huko nyuma kurudia ili kuwa ni kawaida though ilikuwa kosa la jinai. Wengi walio serikalini na rika la mengi ni ma-repeaters wa darasa la saba.

it is also a foolish and childish accussation
 
Tutamkumbuka kwa T2014ESCROW...

Muhongo kama angekuwa na akili kama anavyojisifu angetoboa mtihani wa std vii mara moja tu na sio kufoji Mara nne. Nakumbuka Enzi hizo tulikuwa tunayaita majitu yaliyofoji kama Muhongo "maiti"

Nadhani inafaa apongezwe kama ni kweli alirudia std vii mara 3 na sasa profesa.Maana huyo anayekejeri pamoja na kufaulu hilo darasa la saba(kama ni sahihi kuitwa hivyo)ameishia kupewa udaktari wa heshima
 
Kama ni ukweli utabaki ukwel.
C majungu wala fitna.

Walio gush wapo weng sn. Urasimu ndio unawasaidia.
Pole tanzania.
 
Definetely kwa sababu enzi hizo si ajabu hata yeye si Reginald....alirudia. Huko nyuma kurudia ili kuwa ni kawaida though ilikuwa kosa la jinai. Wengi walio serikalini na rika la mengi ni ma-repeaters wa darasa la saba.

it is also a foolish and childish accussation

umeona eeeeh! Nasikia pia hata Mwalimu Nyerere alirudia darasa ingawa sijajua ni darasa lipi
 
Lakini huenda kuna jambo liko nyuma ya pazia kuhusiana na Prof Muhongo. kuna jamaa mmoja alinijuza kuwa hebu nenda kwenye maktaba za vyou vikuu ukatafute maandiko yaliyofanywa na Prof yanayoendana na kupata elimu yake aliniambia anzia hapa Tanzania kwenye Vyuo vikuu vyetu kasha nenda nje ya nchi akaenda mbali aasema huenda ni mmojawapo ya wasomi waliofoji shule
 
Kumbe ndio maana tunashangaa mambo anayofanya muhongo kilaza huyu la saba mara tatu ndio maana haishi kujisifu kuwa ni msomi
.
 
MENGI anafikiri hii ni hoja ya kumng'oa Muhongo kweli? ama kweli u aweza kuwa umesoma lakini usielimike. Hoja ya kijinga kwa mwaka huu.
 
Jana Mr Reginald Mengi alipost kwenye Istagram yake kwamba kuna Mtu aliwahi kurudia la Saba mara tau na leo ni Le Porofeseri bila shaka akimaanisha Sospeter Muhongo

Je ana hoja>?
Ndiyo, anayo hoja. Usikate tamaa katika kila lengo unalotaka kufikia.
 
Ingawa najua Muhungo ni mropokaji na mara nyingi amekuwa si makini lakini kama kweli Mengi amesema maneno haya kumkejeli kwamba alirudia shule amekosea sana.

Naomba tuweke rekodi sawa kuhusu suala la kurudia shule. Miaka ya 1997 kurudi nyuma suala la kurudia shule lilikuwa changamoto kwa watu wengi. Wengi waliokuwa wasomi wa leo hata kushika nyadhifa kubwa serikalini wamerudia shule. HUWEZI KUWALAUMU ila kulaumu mfumo hafifu wa elimu Enzi hizo ambako hakukuwa na shule za sekondari za kutosha hivyo ni watu wachache tu pengine asilimia 5 ya watu waliofaulu mitihani yao walioweza kuchaguliwa kujiunga na shule. Huu mfumo umeanza toka ukoloni mpaka hivi majuzi tu ambapo shule za sekondari zimejengwa nyingi kuwasajili wanafunzi wengi wanaofaulu. Enzi hizo mtu angepata alama 90 na asipate nafasi ya kuingia sekondari. Issue ya pili inayokuja lazima itakuwa kwamba wale waliokuwa na nafasi serikalini walitumia mwanya huo kupitisha watu wao. Hivyo watu wa vijijini waliachiwa nafasi chache kugombania. Ungekuta kata nzima hakuna shule iliyofaulisha mwanafunzi licha ya kwambamba kwenye mitihani ya majaribio wapo waliokuwa wanapata alama A wengi.
Kwa kuwa hakukuwa na nafasi ndio maana unaweza kuona kuwa mtu kama Prof Muhongo aliyekuwa na uwezo mkubwa (Ni kweli licha flaws zake nyingi katika mawasiliano, kitaaluma Muhongo ni moto wa kuotea mbali) alishindwa kwenda sekondari, akarudia, akarudia na kurudia. Wapo wengi wanaofanana na Muhongo laiti kungekuwa na nafasi kubwa ya elimu ya sekondari enzi hizo wengi leo wasingekuwa kama walivyo leo.
Kosa kubwa aliyofanya Mwalimu Nyerere ilikuwa katika sekta ya elimu. Sera ya serikali kugharamia elimu peke yake ilikuwa na gharama kubwa na inaigharimu serikali hadi leo. Ni kwamba sera hii ilisababisha sehemu ndogo tu ya gharama iliyogharimiwa na serikali kufanya kazi hivyo shule zikajengwa chache na vyuo vichache. Njia muafaka ingekuwa serikali kugharamia elimu lakini wazazi pia kugharamia ili kuweka wigo mpana. Matokeo yake wengi wamekosa kuendelea na masomi si kwamba hawakuwa na uwezo lakini kwa kuwa nafasi zilikuwa chache.
Ifike mahali serikali ikubali kuwa ilifanya makosa hivyo wale waliorudia shule Enzi hizo wahalalilishwe kwa kuwa ni mfumo mbovu wa elimu uliowafanya warudie shule licha ya kuwa na uwezo mkubwa kitaaluma. Ni kosa la serikali na taifa kwa ujumla, si kosa la warudiaji.
 
Ila mengi na wewe kiboko umeenda kumpekua kwenye mafaili mpaka umempata ngoja tusubifri nae atajibu nini hii vita bado inaendelea.
 
Back
Top Bottom