Ujumbe wa Mengi katika Twitter, kejeli kwa Prof. Muhongo?

Ujumbe wa Mengi katika Twitter, kejeli kwa Prof. Muhongo?

Definetely kwa sababu enzi hizo si ajabu hata yeye si Reginald....alirudia. Huko nyuma kurudia ili kuwa ni kawaida though ilikuwa kosa la jinai. Wengi walio serikalini na rika la mengi ni ma-repeaters wa darasa la saba.

it is also a foolish and childish accussation
Hivi alichofanya Mengi ni kumtuhumu Muhongo, au kueleza ukweli kwamba alirudia mara tatu! Muhongo amewahi kusema Sendeka alipata "0" A level, hiyo ilikuwa tuhuma, au fact!
 
Jana Mr Reginald Mengi alipost kwenye Istagram yake kwamba kuna Mtu aliwahi kurudia la Saba mara tau na leo ni Le Porofeseri bila shaka akimaanisha Sospeter Muhongo

Je ana hoja>?

Mzee Mengi amepotoka, kwa umri wake huo no utovu Wa hekima maana hiyo ni hoja dhaifu sana.

Mengi atueleze ubaya uko wapi? Kwamba kurudia la saba Mara tatu kunahusiana vipi Na tofauti zao? Kosa LA Prof. Muhongo hapo limo wapi? Kurudia Mara tatu hakumfanyi Prof. Muhongo kuwa duni, mafanikio ya Prof. Muhongo kitaaluma ni makubwa kuliko ya Mengi. Kama Mzee Mengi anajiona bora kwa yeye kutorudia darasa lolote basis atuwekee elimu take ili tuamue nano yuko juu.

Nashauri Prof. Muhongo asijibu upuuzi huo Wa Mzee Mengi.

Vv
 
......Daah! Mengi karusha jiwe moja ila kauwa ndege wengi mno. Utaona katika comment zitakazoandikwa hapa, wale wenye elimu za "welding" watakavyotoka povu. Ebu, nikae pembeni niangalie movie inavyoendelea.
 
Ndio maana yake!
Imagine kwa Tanzania ya leo nearly 42% wamedumaa kimwili probably kiakili!kipindi cha kina Muhongo si ndio ilikuwa balaa?

Tena kwa kurudia mara tatu yaonesha ukilaza wa kiwango cha juu.

Mimi binafsi sijawahi kurudia darasa hata baada ya Makweta kuleta kijimtihani cha darasa la 10 nilipasua vilevile.

Napenda ikumbukwe kwamba enzi zile akina Muhongo wanapiga primary school, shule za sekondari zilikuwa chache sana. Iliwezekana mtu mmoja kuzitaja zote maana katika mikoa mingi zilikuwa hazizidi shule 2 au 3 ukiondoa mikoa ya Kagera na Kilimanjaro. Kipindi kile wanafunzi walikuwa wanafaulu wengi lakini wachache walikuwa wanachaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari. Inawezekana Muhongo alifaulu mara mbili bila kuchaguliwa hatimaye mara ya 3 akachaguliwa. Isieleweke kwamba kurudia shule kipindi kile ni alama ya ukilaza.

Hongera Prof. Muhongo kwa kurudia mara tatu (kuhakikisha haki inatendeka) na leo wewe ni Profesa.
 
Kwahiyo uprofesa unapatikana darasa la tatu atafute sababu yenye mashiko ili tuwe nyuma yake kama alivyowazarau wazawa kuwa yao maji na juic ges za wazungi
 
sawasawa mjomba
Ingawa najua Muhungo ni mropokaji na mara nyingi amekuwa si makini lakini kama kweli Mengi amesema maneno haya kumkejeli kwamba alirudia shule amekosea sana.

Naomba tuweke rekodi sawa kuhusu suala la kurudia shule. Miaka ya 1997 kurudi nyuma suala la kurudia shule lilikuwa changamoto kwa watu wengi. Wengi waliokuwa wasomi wa leo hata kushika nyadhifa kubwa serikalini wamerudia shule. HUWEZI KUWALAUMU ila kulaumu mfumo hafifu wa elimu Enzi hizo ambako hakukuwa na shule za sekondari za kutosha hivyo ni watu wachache tu pengine asilimia 5 ya watu waliofaulu mitihani yao walioweza kuchaguliwa kujiunga na shule. Huu mfumo umeanza toka ukoloni mpaka hivi majuzi tu ambapo shule za sekondari zimejengwa nyingi kuwasajili wanafunzi wengi wanaofaulu. Enzi hizo mtu angepata alama 90 na asipate nafasi ya kuingia sekondari. Issue ya pili inayokuja lazima itakuwa kwamba wale waliokuwa na nafasi serikalini walitumia mwanya huo kupitisha watu wao. Hivyo watu wa vijijini waliachiwa nafasi chache kugombania. Ungekuta kata nzima hakuna shule iliyofaulisha mwanafunzi licha ya kwambamba kwenye mitihani ya majaribio wapo waliokuwa wanapata alama A wengi.
Kwa kuwa hakukuwa na nafasi ndio maana unaweza kuona kuwa mtu kama Prof Muhongo aliyekuwa na uwezo mkubwa (Ni kweli licha flaws zake nyingi katika mawasiliano, kitaaluma Muhongo ni moto wa kuotea mbali) alishindwa kwenda sekondari, akarudia, akarudia na kurudia. Wapo wengi wanaofanana na Muhongo laiti kungekuwa na nafasi kubwa ya elimu ya sekondari enzi hizo wengi leo wasingekuwa kama walivyo leo.
Kosa kubwa aliyofanya Mwalimu Nyerere ilikuwa katika sekta ya elimu. Sera ya serikali kugharamia elimu peke yake ilikuwa na gharama kubwa na inaigharimu serikali hadi leo. Ni kwamba sera hii ilisababisha sehemu ndogo tu ya gharama iliyogharimiwa na serikali kufanya kazi hivyo shule zikajengwa chache na vyuo vichache. Njia muafaka ingekuwa serikali kugharamia elimu lakini wazazi pia kugharamia ili kuweka wigo mpana. Matokeo yake wengi wamekosa kuendelea na masomi si kwamba hawakuwa na uwezo lakini kwa kuwa nafasi zilikuwa chache.
Ifike mahali serikali ikubali kuwa ilifanya makosa hivyo wale waliorudia shule Enzi hizo wahalalilishwe kwa kuwa ni mfumo mbovu wa elimu uliowafanya warudie shule licha ya kuwa na uwezo mkubwa kitaaluma. Ni kosa la serikali na taifa kwa ujumla, si kosa la warudiaji.
 
Ushahidi kuwa alirudia darasa la saba mara tatu uko wapi?

Na hata kama ni kweli bado Prof. Muhongo is an outstanding academician Na hakuna awezae kukanusha.

Nyakati zile nafasi za kufaulu darasa la saba hazikuwa wazi Na nyingi kama Leo, ili kufaulu darasa LA saba wakati ule ilikuwa lazima kijiji kizima kikubali kuwa uko vizuri kichwani tofauti Na sasa ambapo mwanafunzi hajui kusoma Na kuandika lkn bado anafaulu saba.

Vv
 
Kwahiyo uprofesa unapatikana darasa la tatu atafute sababu yenye mashiko ili tuwe nyuma yake kama alivyowazarau wazawa kuwa yao maji na juic ges za wazungi
naona pia kuna kaudaku kanajipenyeza kuashiria kufilisika
 
never ever give up in life
Na hata kama ni kweli bado Prof. Muhongo is an outstanding academician Na hakuna awezae kukanusha.

Nyakati zile nafasi za kufaulu darasa la saba hazikuwa wazi Na nyingi kama Leo, ili kufaulu darasa LA saba wakati ule ilikuwa lazima kijiji kizima kikubali kuwa uko vizuri kichwani tofauti Na sasa ambapo mwanafunzi hajui kusoma Na kuandika lkn bado anafaulu saba.

Vv
 
mtu kujituma na kutokata tamaa katika maisha imekuwa falsafa ya mengi siku zote labda kama leo hii anageuka kivuli chake mwenyewe
 
Hata kama alirudia, je ni prof wa ukweli au?

Huyo mzee Mengi aache udalali na arudishe pesa aliyoiba BENKI
 
Acheni Le Professor akamilishe kazi ya kusambaza umeme maana utawala wake kama Waziri umesababisha pale kijijini kwetu "MBALAMWEZI" iwake ndani.

Afterall Mkuu wa kaya keshasema PESA NI ZA WAWEKEZAJI kama le professor alivyosema bungeni... kosamlake nini tena...
 
Hivi alichofanya Mengi ni kumtuhumu Muhongo, au kueleza ukweli kwamba alirudia mara tatu! Muhongo amewahi kusema Sendeka alipata "0" A level, hiyo ilikuwa tuhuma, au fact!

hata Muhongo alifanya ujinga...huwezi kumtuhumu mtu kwa sababu amekupa changamoto ambayo inaonekana kuwa juu ya uwezo wako....kwa tz ya leo kurudia ndiyo fasheni na si kosa tena kama zamani...kwa hiyo mengi kuliibua suala hilo leo yeye ndiye anaonekana wa ajabu.
 
jamani jamani tuende mbele 2sisahau kurudi nyuma,,pro aliposema wafanya biashara wa tz biashara zao ni juisi tuu alipatia? tumeona na kusikia watu wamekuja na dola laki 3,,tuu,wamepewa mitambo ya ma bln, ..kumbe anaesema ivo alifeli mara 3,na jina kabadili.. hilo watanzania ha2lioni.mmwacheni mzee m aseme kama muongo alivoachwa akasema

Alikuwa anaitwa Mwijarubi Faru i wonder hilo la Sospeter alipotoa
 
Maana ya Mengi ni kwamba kujikwaa si kuanguka. Kwamba with wasikate Tamara. Ukifanya jambo likashindika endelea kujaribu kwa kusahihisha makosa.

Na pia ukishafanikiwa inakupasa kuwa Mnyenyekevu ili ufanikiwe zaidi
 
Back
Top Bottom