Uhamiaji Musoma, huyu mama kutoka Burundi angefariki damu yake ingewalilia

Dialysis

JF-Expert Member
Sep 22, 2021
325
674
Mama mjamzito ametoka Burundi kwenda Kwa mume wake Kenya Juzi tarehe 25/02/2022. Alivyofika Musoma alikamatwa na uhamiaji sehemu ainayoutwa Kurumuli (Barrier) . Alijitetea kwa uchungu Sana mpaka tulio kuwa kwenye gari lile tulipata huruma.

Mama alijitetea kuwa anaenda Kenya kujifungulia huko kwa mchumba aliyempa ujauzito, asingeweza kujifungulia kwao maana hana msaada na hata hivyo hajapata chakula tangu aanze Safari akitokea Burundi Kupita mpaka wa BURUNDI na NGARA na hata hivyo alijitetea kwenye mpaka huo na akasikilizwa.

Afisa wa uhamiaji Musoma hakutaka kabisa kusikiliza na hakujali hali ya mama yule. Alishikiliwa mpaka akapata labour pain (Uchungu) akakimbizwa Kituo cha AFYA NYASHO .

Mama hakuwa na chochote hata nguo hana, kibaya zaidi alipaswa kufanyiwa upasuaji kwa sababu alipata uchungu pingamizi.

Maafisa uhamiaji waliomleta wakatokomea na hata walipotafutwa hawakuwa na msaada, maana kituo hawakuwa na vifaa vya kama surgical gloves, Dawa za baada na kabla ya upasuaji, drip n.k

Watumishi wa kituo hiki walichanga pesa wakamsaidia. Leo yuko wodini hata chakula anapewa na wagonjwa wenzie. Hana nguo anatumia mashuka ya Kituo.

"Hivi uhamiaji pamoja na Sheria za nchi kwa Hali kama hiyo hawakuwa na chakufanya kuanzia kwenye ukamataji"?
 
Imekuwa kadhia siku hizi eti nchini kwako ni lazima usafiri ukiwa na nyaraka zinazothibitisha wewe ni raia; tulisimamishwa Chalinze pale na hao makonstebo wakaomba kila mtu atoe kitambulisho cha taifa... ilikuwa fujo kwenye gari wengi hawana ufahamu kwamba ni lazima uwe na utambulisho safarini, sielewi kwanini hawajapeleka elimu kwanza kwenye jamii.

Pole sana kwa huyo Mama; by birth kijana ni mtanzania sasa 👏😁
 
Nadhani huyo dogo wa immigration anasoma huu uzi na hii reply ni yake kama ifuatavyo...

Nasema "hii dunia ni moja, haya mataifa yametokana na dhambi zilizosababishwa na wewe, hiyo nafasi hapo uhamiaji ni cheo cha muda, hawa binadamu wapo na hawataisha, tunakuja na kuondoka, kesho anaota/birth mwingine as huyo kijana uliyesababisha akazaliwa nchi uliyotaka wewe"...

Kumbuka, ... "lolote unalomfanyia mwenzako hujirudi kwa njia nyingine na kukuadhibu ukiwa umesahau matendo uliyomfanyia mwenzako. Tabia kama hiyo ya kukomalia jambo ambalo kwa elimu ya darasani kwenye mambo ya uhamiaji sidhani kama uliwahi fundishwa kukomaa na mtu mwenye hujauzito"...

Na ... "baada ya tukio la kumsababishia hali ile ukakimbia ila nafsi yako najua inavyokusumbua na huna la kufanya although unajipa moyo ulikiwa kazini ukitekeleza wajibu, wajibu gani ambao unaona kabisa kuna hali ya hatari?."

Haya ni maisha mdogo wangu afisa uhamiaji na hizi ni nchi za Afrika Mashariki mnazojipambanua kuwa na ushirikiano wa jumuiya, mwisho "hata wewe unajiita kidume ukiwa mkoa nje ya Mara au nje ya Tanzania huwa unaparamia mabinti wa watu, siku unaondoka hujui kama ulipandikiza mbegu"


Asante.
 
Nadhani huyo dogo wa immigration anasoma huu uzi na hii reply ni yake kama ifuatavyo...

Nasema "hii dunia ni moja, haya mataifa yametokana na dhambi zilizosababishwa na wewe, hiyo nafasi hapo uhamiaji ni cheo cha muda, hawa binadamu wapo na hawataisha, tunakuja na kuondoka, kesho anaota/birth mwingine as huyo kijana uliyesababisha akazaliwa nchi uliyotaka wewe"...

Kumbuka, ... "lolote unalomfanyia mwenzako hujirudi kwa njia nyingine na kukuadhibu ukiwa umesahau matendo uliyomfanyia mwenzako. Tabia kama hiyo ya kukomalia jambo ambalo kwa elimu ya darasani kwenye mambo ya uhamiaji sidhani kama uliwahi fundishwa kukomaa na mtu mwenye hujauzito"...

Na ... "baada ya tukio la kumsababishia hali ile ukakimbia ila nafsi yako najua inavyokusumbua na huna la kufanya although unajipa moyo ulikiwa kazini ukitekeleza wajibu, wajibu gani ambao unaona kabisa kuna hali ya hatari?."

Haya ni maisha mdogo wangu afisa uhamiaji na hizi ni nchi za Afrika Mashariki mnazojipambanua kuwa na ushirikiano wa jumuiya, mwisho "hata wewe unajiita kidume ukiwa mkoa nje ya Mara au nje ya Tanzania huwa unaparamia mabinti wa watu, siku unaondoka hujui kama ulipandikiza mbegu"


Asante.
Salute mkuu, hawa vijana wa dot.com sijui nani kawapa roho za kishetani, mtu yupo transit why uhangaike naye?na Hana illegal substances zozote why umsumbue?hii laana itaishi naye maisha yake yote, mpumbavu mkubwa
 
Kuna ofisi moja ya uhamiaji wakiwakamata watu wa namna hiyo (wasio raia) huwapiga sana na kuwanyang'anya fedha zao wanazokuwa wamezipata katika kufanya kazi aidha wakiwa wanarudi nchini kwao au wakiwa wameingia nchini kwetu katika utafutaji.

Sasa ninapofanyia kazi ni karibu na ofisi hiyo Sasa wakiwa wanawapiga wanatoa kilio cha uchungu sana utakuta mtu anapigwa zaidi ya masaa matatu roho yangu huwa inaugua sana kwa kusikia vilio vile.

Baada ya kuwapiga huwapora fedha zao na kuwaachia warudi nchini kwao huku hawana nauli wala hela ya chakula, uhamiaji fuateni taratibu zenu za kazi tafadhari
 
Kuna ofisi moja ya uhamiaji wakiwakamata watu wa namna hiyo (wasio raia) huwapiga sana na kuwanyang'anya fedha zao wanazokuwa wamezipata katika kufanya kazi aidha wakiwa wanarudi nchini kwao au wakiwa wameingia nchini kwetu katika utafutaji.
Sasa ninapofanyia kazi ni karibu na ofisi hiyo Sasa wakiwa wanawapiga wanatoa kilio cha uchungu sana utakuta mtu anapigwa zaidi ya masaa matatu roho yangu huwa inaugua sana kwa kusikia vilio vile.
Baada ya kuwapiga huwapora fedha zao na kuwaachia warudi nchini kwao huku hawana nauli wala hela ya chakula, uhamiaji fuateni taratibu zenu za kazi tafadhari
Mkuu kwa heshima na taadhima naomba utaje hiyo ofisi, maana Sabaya keshakula 30 kwa unyang'anyi ili nao wapate fundisho.
 
Imekuwa kadhia siku hizi eti nchini kwako ni lazima usafiri ukiwa na nyaraka zinazothibitisha wewe ni raia; tulisimamishwa Chalinze pale na hao makonstebo wakaomba kila mtu atoe kitambulisho cha taifa...ilikuwa fujo kwenye gari wengi hawana ufahamu kwamba ni lazima uwe na utambulisho safarini, sielewi kwanini hawajapeleka elimu kwanza kwenye jamii!!. Pole sana kwa huyo Mama; by birth kijana ni mtanzania sasa 👏😁

mngewaacha wawakamate, halafu wawaambie kwenu wapi....then unakwenda kwa cowboy pale msasani kuomba asylum nchi yako haikutaki...
 
Mh kheri amejifungulia hapa Tz, ktk ile nchi ya Kenya sidhani kama angeambulia kitu
 
Mama mjamzito ametoka Burundi kwenda Kwa mume wake Kenya Juzi tarehe 25/02/2022.Alivyofika Musoma alikamatwa na uhamiaji sehemu ainayoutwa Kurumuli(Barrier) .Alijitetea kwa uchungu Sana mpaka tulio kuwa kwenye gari lile tulipata huruma.

Mama alijitetea kuwa anaenda Kenya kujifungulia huko kwa mchumba aliyempa ujauzito ,asingeweza kujifungulia kwao maana hana msaada na hata hivyo hajapata chakula tangu aanze Safari akitokea Burundi Kupita mpaka wa BURUNDI na NGARA na hata hivyo alijitetea kwenye mpaka huo na akasikilizwa.

Afisa wa uhamiaji Musoma hakutaka kabisa kusikiliza na hakujali hali ya mama yule.Alishikiliwa mpaka akapata labour pain(Uchungu) akakimbizwa Kituo cha AFYA NYASHO .

Mama hakuwa na chochote hata nguo hana ,kibaya zaidi alipaswa kufanyiwa upasuaji kwa sababu alipata uchungu pingamizi.

Maafisa uhamiaji waliomleta wakatokomea na hata walipotafutwa hawakuwa na msaada ,maana kituo hawakuwa na vifaa vya kama surgical gloves,Dawa za baada na kabla ya upasuaji,drip n.k

Watumishi wa kituo hiki walichanga pesa wakamsaidia.Leo yuko wodini hata chakula anapewa na wagonjwa wenzie.Hana nguo anatumia mashuka ya Kituo.

"Hivi uhamiaji pamoja na Sheria za nchi kwa Hali kama hiyo hawakuwa na chakufanya kuanzia kwenye ukamataji"???
mkuu wewe ilikuwaje ukasafiri na huyo mama, ukaenda kuona anavyozaa na kutelekezwa na pia unaona anavyonyanyasika wodini?
 
mkuu wewe ilikuwaje ukasafiri na huyo mama,ukaenda kuona anavyozaa na kutelekezwa na pia unaona anavyonyanyasika wodini?
clinician Mimi nilikuwa nasafiri nikitokea Mwanza kwenda TARIME alivyosushwa kwenye gari abilia tulipatwa hasira zilizo changanyika na huruma.

Kesho yake nilikuwa naenda MUSOMA MJINI huko nilipata full story ya mama huyo.

Nilifika mpaka kituo cha Afya Nyasho kumuona anatia huruma sana hata Kiswahili hajui vizuri
 
Mama mjamzito ametoka Burundi kwenda Kwa mume wake Kenya Juzi tarehe 25/02/2022.Alivyofika Musoma alikamatwa na uhamiaji sehemu ainayoutwa Kurumuli(Barrier) .Alijitetea kwa uchungu Sana mpaka tulio kuwa kwenye gari lile tulipata huruma.

Mama alijitetea kuwa anaenda Kenya kujifungulia huko kwa mchumba aliyempa ujauzito ,asingeweza kujifungulia kwao maana hana msaada na hata hivyo hajapata chakula tangu aanze Safari akitokea Burundi Kupita mpaka wa BURUNDI na NGARA na hata hivyo alijitetea kwenye mpaka huo na akasikilizwa.

Afisa wa uhamiaji Musoma hakutaka kabisa kusikiliza na hakujali hali ya mama yule.Alishikiliwa mpaka akapata labour pain(Uchungu) akakimbizwa Kituo cha AFYA NYASHO .

Mama hakuwa na chochote hata nguo hana ,kibaya zaidi alipaswa kufanyiwa upasuaji kwa sababu alipata uchungu pingamizi.

Maafisa uhamiaji waliomleta wakatokomea na hata walipotafutwa hawakuwa na msaada ,maana kituo hawakuwa na vifaa vya kama surgical gloves,Dawa za baada na kabla ya upasuaji,drip n.k

Watumishi wa kituo hiki walichanga pesa wakamsaidia.Leo yuko wodini hata chakula anapewa na wagonjwa wenzie.Hana nguo anatumia mashuka ya Kituo.

"Hivi uhamiaji pamoja na Sheria za nchi kwa Hali kama hiyo hawakuwa na chakufanya kuanzia kwenye ukamataji"???
Mimi naona uhamiaji inalaumiwa bure. Je, huyo mama alikuwa na passport ya Africa Mashariki akakataliwa kuendelea na safari?

Tukitunga sheria lazima tuzifuate. Hatuwezi kuchagua sheria ipi ifuatwe na ipi isifuatwe. Huyu mama angekuwa na makaratasi yanayotakiwa angeendelea na safari.

Kwanza unajuaje ni kweli anaenda Kenya. Unajuaje ni Mrundi. Kwa nini hakuwa na passport? Je huko Kenya angeingiaje bila passport?

Si angeisha kurudishwa mpakani. Kama alipata uchungu na kwenda Nyasho Clinic, si ni afadhali kuliko kupatia uchungu ndani ya gari ambapo huduma ya ukunga hakuna?
 
Kuna ofisi moja ya uhamiaji wakiwakamata watu wa namna hiyo (wasio raia) huwapiga sana na kuwanyang'anya fedha zao wanazokuwa wamezipata katika kufanya kazi aidha wakiwa wanarudi nchini kwao au wakiwa wameingia nchini kwetu katika utafutaji.
Sasa ninapofanyia kazi ni karibu na ofisi hiyo Sasa wakiwa wanawapiga wanatoa kilio cha uchungu sana utakuta mtu anapigwa zaidi ya masaa matatu roho yangu huwa inaugua sana kwa kusikia vilio vile.
Baada ya kuwapiga huwapora fedha zao na kuwaachia warudi nchini kwao huku hawana nauli wala hela ya chakula, uhamiaji fuateni taratibu zenu za kazi tafadhari
Ukisika uongo ndiyo huu. Nafikiri wewe ni CHADEMA.
 
Back
Top Bottom