Mbeya: Uzembe wa Hospitali ya Rufaa Kanda umesababisha kifo cha binti huyu

Mwanongwa

Senior Member
Feb 15, 2023
169
198
Mwanajamii fuatilia huu mkasa kwa kina.

Kuna binti anaitwa Belith Adamu Mwangoka ambaye kwasasa ni Marehemu na amefariki leo hii majira ya saa kumi jioni katika hospitali ya Rufaa ya Kanda mkoani Mbeya.

FUATILIA KISA CHAKE HAPA HADI UMAUTI ULIPOMFIKA

Marehemu alifika Kituo cha afya Ruanda Mwanjelwa alikuja kufungua kadi ya mimba lakini hali aliyokuja nayo haikuwa nzuri akapewa barua kwenda Hospitali ya Rufaa ya Mkoa maarufu kama Mkoani.

Akawa hana uwezo wa kulipia gharama za matibabu nikamwambia mimi nitakusaidia hata ukilazwa nitakuletea chakula, mgonjwa akakubali tukachukua gari la wagonjwa tulipofika Mkoani alianza matibabu.

Nikaomba kibali cha kutibiwa kwa sosho walinipa lakini hakikusaidia kitu baada ya hapo nikaambiwa amepewa ya kitanda tu nikaanza kununua dawa wakamuanzishia uchungu akajifungua mtoto Njiti maana miezi ilikuwa haijatimia, lakini hali ilikuwa mbaya sana wakaniambia damu yake ni B Negative tutoe hela inatakiwa chupa mbili nikatoa wakamwongeza baada ya hapo wakamruhusu kutoka hospitali.

Nikawambia mbona hali bado analalamika kifua na tumbo limejaa wakamruhusu hivyohivyo akawa anatembea kwa shida sana tukarudi nyumbani kwangu.
ae69217a-7506-4e31-a530-272ba58967d5.jpg

Marehemu Belith Adamu Mwangoka
Nilivyokaa naye siku 3 ya 4 nikarudi naye tena Kituo cha Afya Ruanda Mwanjelwa, nilipofika wakatupa tena barua ilikuwa usiku tukafika mkoani wakaniuliza mmekuja na usafiri gani nikawaambia Bajaj walishangaa maana mgonjwa alikuwa hawezi hata kutembea.

Basi Mkoani wakatupa huduma siku ya tatu wakatupa barua tukaenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda kukawa hakuna huduma yoyote, nikiwafuata wananiambia mbona hamjamchukua vipimo wananiambia "kesho", jamani mgonjwa kazidiwa mtundikieni hata maji na tayari nilikuwa nimelipia wakawa wanamwangalia tu mpaka jana nikaenda huyu mgonjwa hali yake ilikuwa mbaya na sukari ilikuwa imeshuka mpaka 1 .

Mgonjwa mwenyewe akaniambia mama hawa wananiua tu ndio wakamtundikia maji moja, naenda jioni nikakuta wamemtoa nikawauliza mbona maji hayajaisha wakasema huoni sasa sasa hivi kafumbua macho.

Hospitali sasa hivi wanangalia mtu mwenye hela, kifo cha Belith wamechangia sana sio Mkoani sio Rufaa walikuwa wanamwambia maneno magumu sana ambayo yalikuwa yanampa wakati mgumu sana.

Hiyo ni simulizi ya mtoa huduma katika Kituo cha Afya cha Ruanda Mwanjelwa.

Marehemu alikuwa ameolewa na mwanaume mmoja ambaye kabila lake ni Msukuma na wakifanikiwa kupata mtoto mmoja ambapo jamaa alivyoona mkewe kabeba tena mimba ya pili akaamua kutoroka na mtoto wake mkubwa.

MTOTO ANAHITAJI MSAADA WA MAZIWA NA MAHITAJI MENGINE
e39da40a-4f5b-4ba6-9a26-fe1c36374ae2.jpg
 
Mwanajamii fuatilia huu mkasa kwa kina.

Kuna binti anaitwa Belith Adamu Mwangoka ambaye kwasasa ni Marehemu na amefariki leo hii majira ya saa kumi jioni katika hospital ya Rufaa ya Kanda mkoani Mbeya.

FUATILIA KISA CHAKE HAPA HADI UMAUTI ULIPOMFIKA

"marehemu alifika kituo Cha afya Ruanda Mwanjelwa alikuja kufungua kadi ya mimba lakini hali aliyokujanayo haikuwa nzuri akapewa barua kwenda hospital ya Rufaa ya mkoa maarufu kama mkoani.

Akawa hanauwezo wa kulipia gharama za matibabu nikamwambia mimi nitakusaidia hata ukilazwa nitakuletea chakula, mgonjwa akakubali tukachukua Gari la wagonjwa tulipofika mkoani alianza matibabu.

Nikaomba kibali Cha kitibiwa kwa sosho walinipa lakina hakikusaidia kitu baada ya hapo nikaambiwa amepewa ya kitanda tu nikaanza kununua dawa wakamuanzishia uchungu akajifungua mtoto Njiti maana miezi ilikuwa haijatimia,lakini hali ilikua mbaya Sana wakaniambia dam yake ni B negative tutoe hela inatakiwa Chupa mbili nikatoa wakamwongeza baada ya hapo wakamruhusu kutoka hospital.

Nikawambia mbona hali bado analalamika kifua natumbo limejaa wakamruhusu hivyo hivyo akawa anatembe kwa shida Sana tukarudi nyumbani kwangu nilivyokaa nae siku 3 ya 4 nikarudi naye tena kituo cha Afya Ruanda wwanjelwa nilipofika wakatupa tena barua ilikua usiku tukafika mkoani wakaniuliza mmekuja na usafiri gani nikawambia bajaji walishangaa maana mgonjwa alikua hawezi hata kutembea,

Basi mkoani wakatupa huduma siku ya tatu wakatupa barua tukaenda hospital ya Rufaa ya kanda kukawa hakuna huduma yoyote, nikiwafuata wananiambia mbona hamjamchukua vipimo wananiambia kesho jamani mgonjwa kazidiwa mtundikieni hata maji na tayari nilikuwa nimelipia wakawa wanamwangalia tu mpaka jana nikaenda huyu mgonjwa Hali yake ilikuwa mbaya na sukari ilikuwa imeshuka mpaka 1 .

Mgonjwa mwenyewe akaniambia mama hawa wananiua tu ndio wakamtundikia maji moja naenda jioni nikakuta wamemtoa nikawauliza mbona maji hayajaisha wakasema huoni saizi kafumbua macho .

Hospitality saizi wanangalia mtu mwenye hela, kifo Cha Belith wamechangia Sana sio mkoani sio Rufaa walikua wanamwamia maneno magumu Sana ambayo yalikua yanampa wakati mgumu sana"

Hiyo ni simulizi ya mtoa huduma katika kituo cha Afya cha Ruanda Mwanjelwa.
Stori zingine zinatia uchungu sana aisee
 
Pole sn mkuu,apumzike kwa amani dada.

Nadhani Hospital ya Meta ndo kila kitu kwa Mbeya,ungejitahidi akafikishwa Meta mkuu.
 
Mwanajamii fuatilia huu mkasa kwa kina.

Kuna binti anaitwa Belith Adamu Mwangoka ambaye kwasasa ni Marehemu na amefariki leo hii majira ya saa kumi jioni katika hospital ya Rufaa ya Kanda mkoani Mbeya.

FUATILIA KISA CHAKE HAPA HADI UMAUTI ULIPOMFIKA

"marehemu alifika kituo Cha afya Ruanda Mwanjelwa alikuja kufungua kadi ya mimba lakini hali aliyokujanayo haikuwa nzuri akapewa barua kwenda hospital ya Rufaa ya mkoa maarufu kama mkoani.

Akawa hanauwezo wa kulipia gharama za matibabu nikamwambia mimi nitakusaidia hata ukilazwa nitakuletea chakula, mgonjwa akakubali tukachukua Gari la wagonjwa tulipofika mkoani alianza matibabu.

Nikaomba kibali Cha kitibiwa kwa sosho walinipa lakina hakikusaidia kitu baada ya hapo nikaambiwa amepewa ya kitanda tu nikaanza kununua dawa wakamuanzishia uchungu akajifungua mtoto Njiti maana miezi ilikuwa haijatimia,lakini hali ilikua mbaya Sana wakaniambia dam yake ni B negative tutoe hela inatakiwa Chupa mbili nikatoa wakamwongeza baada ya hapo wakamruhusu kutoka hospital.

Nikawambia mbona hali bado analalamika kifua natumbo limejaa wakamruhusu hivyo hivyo akawa anatembe kwa shida Sana tukarudi nyumbani kwangu nilivyokaa nae siku 3 ya 4 nikarudi naye tena kituo cha Afya Ruanda wwanjelwa nilipofika wakatupa tena barua ilikua usiku tukafika mkoani wakaniuliza mmekuja na usafiri gani nikawambia bajaji walishangaa maana mgonjwa alikua hawezi hata kutembea,

Basi mkoani wakatupa huduma siku ya tatu wakatupa barua tukaenda hospital ya Rufaa ya kanda kukawa hakuna huduma yoyote, nikiwafuata wananiambia mbona hamjamchukua vipimo wananiambia kesho jamani mgonjwa kazidiwa mtundikieni hata maji na tayari nilikuwa nimelipia wakawa wanamwangalia tu mpaka jana nikaenda huyu mgonjwa Hali yake ilikuwa mbaya na sukari ilikuwa imeshuka mpaka 1 .

Mgonjwa mwenyewe akaniambia mama hawa wananiua tu ndio wakamtundikia maji moja naenda jioni nikakuta wamemtoa nikawauliza mbona maji hayajaisha wakasema huoni saizi kafumbua macho .

Hospitality saizi wanangalia mtu mwenye hela, kifo Cha Belith wamechangia Sana sio mkoani sio Rufaa walikua wanamwamia maneno magumu Sana ambayo yalikua yanampa wakati mgumu sana"

Hiyo ni simulizi ya mtoa huduma katika kituo cha Afya cha Ruanda Mwanjelwa.


Marehemu alikuwa ameolewa na mwanaume mmoja ambaye kabila lake ni Msukuma na wakifanikiwa kupata mtoto mmoja ambapo jamaa alivyoona mkewe kabeba tena mimba ya pili akaamua kutoroka na mtoto wake mkubwa.

MTOTO ANAHITAJI MSAADA WA MAZIWA NA MAHITAJI MENGINE

0766127653 jina Lucy Mussa Samajengo.

View attachment 2711246View attachment 2711245
Nenda kwa Mwambukusi atakusaidia.
 
story iba leta uchungu.. Ila kuna haja ya kusikiliza na upande wa pili..

POLE SANA KWA YALIYOKUKUTA:


1. kwa hiyo mkoani na rufaa wote walikubaliana kuto muhudumia ndugu yako tu. Kwote hukutendewa haki.

2. Kuna wagonjwa wengine wana malalamiko kama yako
3. unasema huku hudumiwa hapo hapo unasema sukari ilikuwa moja... ulijuaje ? kama siyo uliambiwa na walio kuwa wana muhudimia

4. kwa nn ulitaka mgonjwa awekewe maji? we ni daktari pia? unajuaje mgonjwa anahitaj tiba maji?

5. ulifikisha malalamiko yako kwa uongozi, ukapewa maelezo na hukuridhika kabla ya kuja kulalamika humu..?
 
Huyu alienda Meta ile ya wazazi au alienda ile isiyokuwa ya wazazi!?
Alienda ile ambayo siyo ya wazazi sababu baada ya kujifungua aliruhusiwa kurudi home lakini baadae hali ikawa inabadilika ndiyo wakampa rufaa ya kwenda ile ya kanda
 
Back
Top Bottom