Ugenini kuna kunguni, sijui nifanye nini!

Ugenini kuna kunguni, sijui nifanye nini!

Rudi kwenu
Nashindwa kuelewa hii nyumba niliyofikia hawa wenyeji wangu wanapata vipi usingizi. Kunguni niliowaona baada ya kulinyanyua godoro ni wengi utadhani mchanga umemwagwa hapo kitandani!

Siwapendi kwa usumbufu wao lakini pia unaweza kuaibika mbele za watu unakuta dudu limeshiba halafu linatembea kwenye nguo zako tena shati jeupe. Naona noma hata kumwambia jamaa kwa jinsi anavyokuwa akijipaisha. Wasiwasi wangu nisije nikatoka na mbegu hapa.

Nifanyaje?
 
kuna mtu aliwahisema kuna aina fulani ya vyandarua zinaleta kunguni sikuamini nikaamua kutafuta aina hiyo ya chandarua nikaifunga chumba kitupu na haki lali mtu.baada ya wiki nikaona vitu vyeupe nikatoa chandarua nikaifua baada ya wiki 2 mazee hao mifugo ni wengi kona zote za chandarua! hata nilipo piga sumu wadudu hawa waliendelea kuwepo hadi nilipo itoa ile net nikaichoma moto nasikupiga dawa bali niliacha madirisha ya chumba hiko wazi ndo wakapotea mazima.hivyo kuna vyandarua vinaleta wadudu hao haya upige dawa hasikii watapotea kwa muda na hurudi kwa kasi
Mkuu chandarua gani ni pm ni kijue jina maana walinisumbua sana zamani
 
Sasa ndugu yangu, akilala uchi ataongeza kiwango cha kufyonzwa.

Pia baadhi ya wadudu wanaweza kupenya kwenye uwazi wa nyuma kujitafutia makazi zaidi.

Au wewe humuonei huruma nduguyo kwa kumshauri alale uchi?.
Kwa akili yangu leo mmeniacha mbali sana1
 
Nashindwa kuelewa hii nyumba niliyofikia hawa wenyeji wangu wanapata vipi usingizi. Kunguni niliowaona baada ya kulinyanyua godoro ni wengi utadhani mchanga umemwagwa hapo kitandani!

Siwapendi kwa usumbufu wao lakini pia unaweza kuaibika mbele za watu unakuta dudu limeshiba halafu linatembea kwenye nguo zako tena shati jeupe. Naona noma hata kumwambia jamaa kwa jinsi anavyokuwa akijipaisha. Wasiwasi wangu nisije nikatoka na mbegu hapa.

Nifanyaje?
rudi kwako...

miaka hii na kunguni khaaaaaaaaaa ni wapi huko
halafu kunguni ni uchafu
kama ikiwezekana fanya kuwamwagia maji moto toa godoro nje ikibidi na kitanda
 
wanateketeaje hao wadudu mbona kwangu nimepambana nao huu mwezi wa 3 lkn hawaishi naomba msaada
 
Kunakipindi madereva wa daladala tuligoma tukakamatwa na kuwekwa sero mkoa furani, nadhani siku hiyo kunguni kama walinyonya kidogo ni damu Lita mbili.
 
Waite watu wa fumigation ili wawapulizie dawa na kuwaua hao kunguni, utakuwa umemsaidia sana mwenyeji wako lakini pia na wewe utapata nafasi ya kufanya kazi iliyokupeleka huko
Kunguni ni mgumu kufa kwa dawa..dawa yake ni moto tu
Ndio wadudu siwapendi siku nikimkuta kitandani nachoma godoro na kitanda
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom