jmapunda
JF-Expert Member
- Jul 9, 2015
- 731
- 2,924
Nashindwa kuelewa hii nyumba niliyofikia hawa wenyeji wangu wanapata vipi usingizi. Kunguni niliowaona baada ya kulinyanyua godoro ni wengi utadhani mchanga umemwagwa hapo kitandani!
Siwapendi kwa usumbufu wao lakini pia unaweza kuaibika mbele za watu unakuta dudu limeshiba halafu linatembea kwenye nguo zako tena shati jeupe. Naona noma hata kumwambia jamaa kwa jinsi anavyokuwa akijipaisha. Wasiwasi wangu nisije nikatoka na mbegu hapa.
Nifanyaje?
Siwapendi kwa usumbufu wao lakini pia unaweza kuaibika mbele za watu unakuta dudu limeshiba halafu linatembea kwenye nguo zako tena shati jeupe. Naona noma hata kumwambia jamaa kwa jinsi anavyokuwa akijipaisha. Wasiwasi wangu nisije nikatoka na mbegu hapa.
Nifanyaje?