- Thread starter
- #21
Hapo Hapo!! Huko Kisulu nako kuna habari isemayo!!
Kutoka Gazeti 'letu' la Uhuru
Na Prosper Kwigize, Kasulu
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimeshindwa katika uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika wiki iliyopita katika kata ya Nyamidaho, wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.
Katika uchaguzi huo ulioshirikisha wagombea kutoka vyama vya CCM na CUF, mgombea wa Chama Cha Mapinduzi, Mustapha Mgereranya aliibuka mshindi dhidi ya Abel Nuhu wa CUF.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Msimamizi Msaidizi, Nicholaus Kimondo alisema wapiga kura 7,274 walijiandikisha na waliopiga kura walikuwa 2,746.
Kimondo alisema kati ya kura 2,746 zilizopigwa, halali zilikuwa 2,696, wakati nyingine zikiripotiwa kuharibika.
Nuhu alipata kura 1,047, wakati Magereranya alishinda kwa kupata kura 1,649.
Wakati huo huo, vinara wa CUF katika tarafa ya Makere, wilayani Kasulu wamekihama chama hicho na kujiunga na CCM kwa kile walichodai kuwa ndani ya chama chao hakuna demokrasia.
Waliojiunga na CCM ni Tumaini Sambilo na Henrico Kimorimori, ambaye alikuwa mgombea wa kiti cha udiwani wa kata ya Nyamidaho kwa tiketi ya CUF katika uchaguzi mkuu mwaka 2005.
Katibu wa CCM mkoa wa Kigoma, Said Hamad alisema kujiunga na Chama Cha Mapinduzi wanachama hao kunaonyesha kukomaa kwao kisiasa na kukubalika kwa Ilani na sera za Chama.
CUF Kasulu yabwagwa, yakimbiwa na wanachama
Kutoka Gazeti 'letu' la Uhuru
Na Prosper Kwigize, Kasulu
CHAMA cha Wananchi (CUF) kimeshindwa katika uchaguzi mdogo wa udiwani uliofanyika wiki iliyopita katika kata ya Nyamidaho, wilayani Kasulu, mkoani Kigoma.
Katika uchaguzi huo ulioshirikisha wagombea kutoka vyama vya CCM na CUF, mgombea wa Chama Cha Mapinduzi, Mustapha Mgereranya aliibuka mshindi dhidi ya Abel Nuhu wa CUF.
Akitangaza matokeo ya uchaguzi huo, Msimamizi Msaidizi, Nicholaus Kimondo alisema wapiga kura 7,274 walijiandikisha na waliopiga kura walikuwa 2,746.
Kimondo alisema kati ya kura 2,746 zilizopigwa, halali zilikuwa 2,696, wakati nyingine zikiripotiwa kuharibika.
Nuhu alipata kura 1,047, wakati Magereranya alishinda kwa kupata kura 1,649.
Wakati huo huo, vinara wa CUF katika tarafa ya Makere, wilayani Kasulu wamekihama chama hicho na kujiunga na CCM kwa kile walichodai kuwa ndani ya chama chao hakuna demokrasia.
Waliojiunga na CCM ni Tumaini Sambilo na Henrico Kimorimori, ambaye alikuwa mgombea wa kiti cha udiwani wa kata ya Nyamidaho kwa tiketi ya CUF katika uchaguzi mkuu mwaka 2005.
Katibu wa CCM mkoa wa Kigoma, Said Hamad alisema kujiunga na Chama Cha Mapinduzi wanachama hao kunaonyesha kukomaa kwao kisiasa na kukubalika kwa Ilani na sera za Chama.