Uchaguzi Mkuu wa CCM Mwaka 2007

Tusiandikie mate.... kama ni kujisafisha huu ni mwanzo make wabadhirifu ni wengi twasubiri hilo fagio liendelee, Na twalikaribisha kwa mikono miwili. vinginevyo hawa watakuwa wametolewakafara!
 
Hebu angalieni rekodi ya CCM kuwajibishana na rekodi ya Mawaziri au marais kuwawajibisha walio chini yao. Nafikiri rekodi ya CC iko wazi!
 
Ubadhirifu unaoitafuna nchi hii sio ule unaotokea ndani ya CCM; ni ule uliopo serikali ambapo kodi zetu zinapita. Ujasiri wa CC ya CCM ningeuona kama wangeagiza kutimuliwa kwa Antony Diallo (kwa Richmond), Balali (BoT), Karamaga (kwa kutuingiza mkenge na mikataba fake), n.k. Hilo la akina Malegeresi leaves a lot to be desired ukizingatiwa hata nafasi ya kujitetea hawakupewa. Tukumbuke hawa wote waliotimuliwa hakuna hata moja ambaye ni kiongozi wa serikali na wala hawajawahi kuwa huko nyuma! Hakuna sababu ya kumshangilia mchawi kwa kumloga mchawi mwenzake!
 
vyovyote vile tunapaswa kuappreciate alau wameanza kuwashughulikia wabadhirifu, na tunapendekeza hii kasi isiishie kwa hawa izidi kusonga mbele kwa kila mbadhirifu.

sio ss kulaumu tu, hili right ila tukubaliane yako mengi na yanahitaji maamuzi mazito zaidi tunaomba CC muyaone
 
KM,
ulichosema ni kweli kabisa,hao wote hakuna hata mmoja ambaye ni big fish,hakuna cha kufurahia wala kuuzunika hapa.mpola mzee
 
Kilitime,
Tuwe wakweli hivi Mrema UNAWEZA KUMLINGANISHA NA AKINA "OJUKU NA ONYANGO" (Nimetumia wakenya kwa kuwa ndo wameivamia TZ kwa ujambazi na wako tayari kuua ili mradi tu wapate pesa)waliotia timu serikalini safari hii au unampiga madongo kwa kuwa yuko nje ya CC Majambazi.
 
Hakuna haja ya kuwaonea huruma walijipendekeza kuwa wana CCM iliiwe rahisi kwao kuiba.Sasa wamekutwa kuwa hili sio genge lao.Mijitu ya CCm inanidhamu ya kijinga kweli
 
Jamani Lugha iwe Kiswahili au Kiingereza kama Sheria yetu inavyodai,mbona Wakuu naona sasa tunakuja na Kipare!!!Mie nami nikishuka na Kidigo kweli tutaelewana!!!(Joke)
 
HABARI HAZIJADHIBITISHWA!!! MAY BE UDAKU MWINGINE NAJUKA KUSHABIKIA

Hata hivyo, CCM kimeshindwa kueleza maamuzi yaliyofanwa na kikao cha CC kilichoanza Jumamosi na kuendelea hadi jana, badala yake kikatoa taarifa inayovilaumu vyombo vya habari vilivyochapishwa habari kuhusu baadhi ya maamuzi yaliyofanyika.

Baadhi ya magazeti ya kila siku likiwemo gazeti hili, jana yaliripoti baadhi ya maamuzi yaliyofanywa na CC kuwa ni kuwasimamisha uongozi Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi, Abihudi Maregesi na Katibu wake, Cosmas Hinju na kumfukuza kazi Katibu wa CCM wa Mkoa wa Singida, Mujuni Kataraiya kwa tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za ofisi.

Duh haya!

Soma habari kamili hapa
 
nashindwa kuamini kama kweli cc haiwaoni mabadhirifu wanaolila taifa....kama kweli wamedhamiria tutaona kama wataendelea..kama ni adhabu kwa zambi za nyuma ..maana kumbukeni malegesi akiwa mkoani kilimanjaro march 2005,alitangaza rasmi kuwa yuko tayari kumpigia kampeni sumaye..kama dado wana kisasi naye haitakuwa vema...
na kama ni kweli wamewafukuza kwa chuki..nachukulia hilo kama onyo kwa sumaye kwamba anaweza kuangukia pua kwenye uchaguzi wa NEC mkashangaa..kama ndivyo BORA NAE ASTAFU SIASA KAMA SAS...
 
Mvutano mkubwa Kamati Kuu CCM

2007-07-31 10:44:42
Na Mary Edward, PST, Dodoma


Mvutano mkubwa umeibuka ndani ya kikao cha Kamati Kuu ya CCM iliyoanza kukutana mkoani Dodoma tangu Jumamosi iliyopita, hali ambayo imesababisha Kamati hiyo kuongeza siku moja zaidi.

Katika hali ya kawaida kamati hiyo hukutana kwa siku mbili, lakini mvutano huo umesababisha kuendelea kwa muda wa siku tatu.

Habari zilizopatikana kutoka ndani ya kamati hiyo zimesema kuwa kumeibuka makundi mawili, moja likitaka vijana wapewe nafasi nyingi zaidi, huku kundi lingine likitaka vigogo ambao wengi ni wazee ndani ya chama hicho wabakishwe.

Chanzo chetu cha habari kilisema jana kuwa mvutano huo umekuja baada ya mtandao unaowatetea vijana kutoa nafasi nyingi kwa kundi hilo na kusababisha vigogo wanaoshikilia nafasi hizo na ambao wanazitetea katika uchaguzi huo kuachwa.

``Hali hiyo imeibua hasira kutoka kwa baadhi ya wazee wa CCM na kusababisha kikao kushindwa kumalizika ndani ya siku mbili na hivyo kuendelea tena leo ambayo ni siku ya tatu,`` kilisema chanzo hicho cha habari.

Chanzo hicho kilisema kwa kuwa mtandao wa vijana ndio unaoonyesha kuwa na nguvu zaidi kwa upande mwingine matokeo yanaweza kuwa tofauti.

Chanzo kulitabiri kuwa mvutano huo unaweza kusababisha mpasuko mkubwa kwa kuwa vijana wengi hawajakomaa kisiasa.

``Kuna usemi unaosema kuwa uzee ni dawa ? Sasa endapo nafasi nyingi za wazee zitaondolewa, kunaweza kutokea mpasuko ndani ya chama,`` kilisema chanzo hicho.

Wakati hayo yakiendelea, Chama cha Mapinduzi kimevionya baadhi ya vyombo vya habari vinavyotoa taarifa juu ya kikao hicho, kwa madai kuwa baadhi ya taarifa si za kweli.

Taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na kusainiwa na Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya Itikadi na Uenezi, Bw. Aggrey Mwanri, iliwataka waandishi kusubiri taarifa rasmi itakayotolewa na chama hicho.

Wakati huo huo, Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama cha Mapinduzi (NEC) inakutana kwa kikao cha siku mbili mjini Dodoma kuanzia leo na kesho.

Mkutano huo utafanyika chini ya Mwenyekiti wake Rais Jakaya Kikwete.

Miongoni mwa ajenda zitakazojadiliwa ni pamoja na hali ya kisiasa nchini, kupokea taarifa ya ziara ya Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Zanzibar, Rais Aman Abeid Karume na kuteua wagombe uongozi wa CCM ngazi za Wilaya, Mikoa na Taifa.

Hata hivyo, hadi mwandishi wetu alipokuwa anaondoka nje ya viwanja vya mkutano jana saa mbili kasorobo usiku, mvutano katika mkutano huo ulikuwa haujamalizika.

SOURCE: Nipashe
 
Duu kaali kweli kweli!
Sii wawaondoe wazee wachache na kubalance na damu mpya kiasi ya vijana? Au hao wazee wanagoma kung'atuka?
Makubwa!
 
Back
Top Bottom