Uchaguzi Mkuu wa CCM Mwaka 2007

Kama CCM wanaruhusu msuguano wa mawazo hiyo ni positive kwao; tatizo ni pale msuguano huo utakapoleta uasi, lakini kama hautaleta then ndio wanajiimarusha....
 
Nadhani hiyo ni dalili ya demokrasia ndani ya CCM, haya yangetokea miaka ya '80 ungesikia watu wanafukuzwa uanachama! siku hizi hilo haliwezekani kwani ukimfukuza mtu anakimbilia upinzani na kuendeleza mapambano.
 
Lakini, mbona hatujiulizi hawa wanaotuhumiwa kufuja mali wana hali gani sasa? Tunaweza kutazama mambo mawili hapa, what they had few years back and what they are owning recently. Tukipata taarifa, itatusaidia kujua kuwa wanaweza kwa wabadhilifu au la! Naomba kutoa hoja.
 
Nafikiri wanatakiwa kuacha malumbano na kuendeleza kampeni za uchaguzi na kuwafanya wakose muda wa kuhudumia wananchi sisi tunahitaji kupata huduma nzuri na hicho ndio kilio chetu.

Tunahitaji viongozi wajue wajibu wao wakutuhudumia na si kuendeleza malumbano.
 
KWELI mtandas wamekamata chama ..hatimaye mwenyekiti wa jumuia ya wazazi ambaye wakati wa muchakatoo wa urais alitangaza hadharani kumuunga mkono FREDERICK SUMYE...amevuliwa madaraka yote chamani..pia mwingine aliyevuliwa ni aliyewahi kuwa mbunge wa bukoba na sasa katibu wa chama bukoba mh kataraia....wote wanadaiwa kuwa wabadhirifu..na zaidi kataraia anadaiwa kusaidia upinzani..

vipi wadau naona ccm imeanza kuadhibu wabadhirifu kwa kuanza na hao ..tusubiri wengine nao..au isijekuwa ndio mtandao wameanza kufanya usafi...
This is interesting ...

Malegesi na Kataraiya ni jamaa wa karibu sana na lile syndicate la 'mafia' wa BoT, kwa yeyote anyewafahamu hawa jamaa, hili linaweza kuunganishwa na kuwaumiza watu wengine kisiasa!

Yetu macho,...
 
Hivi gurudumu la maendeleo limerudi nyuma miaka mingapi chini ya hawa wazee?? Je tukiendelea nao tutafika??
 
jamani hii ndio sanaa hasa inaanza kazi.JK na EL ni wasanii wetu,sasa hii ndo sijui nini.ebu tazameni:maregesi alimuunga mkono sumaye,mara sumaye karudi toka chuoni na kuchukua fomu ngome yake inaanza kuvunjwa,in maana ubadhirifu wa maregesi umejulikana jana tu?na je yeye ndo mbadhirifu kuliko EL,malecela,JK n.k?

hii ndo sanaa halisi na Boyz II Men ndo wameanza,hadi kufikia 2010 nadhani nchi hii na CCM kwa ujumla watakuwa wamejua maana ya hotuba ya Nyerere ile ya mwaka 1995 wakati alipowakataa hwa B II M.
 
Hivi mvutano wa power struggle CCM kati ya wazee na vijana unaoendelea Dodoma una faida kwa nchi au ni kwa ajili ya ubinafsi wa baadhi ya viongozi wetu? Kuna viongozi wengi wenye uwezo mkubwa ambao wamekuwa kwenye madaraka makubwa kwa muda mrefu. Wengine wamefanya mambo makubwa kwa taifa na wengine wametumia nafasi hiyo kujinufaisha wao binafsi. Sasa kuna hili kundi la vijana ambao hatujui uwezo wao wa kifkira wala wa kiuongozi lakini wanataka wachukuwe madaraka kutoka kwa wazee. Je, kweli tunaweza kuwaamini hawa vijana au tuendelee na wazee wetu???? Naomba maoni yenu!!
 
jamani hii ndio sanaa hasa inaanza kazi.JK na EL ni wasanii wetu,sasa hii ndo sijui nini.ebu tazameni:maregesi alimuunga mkono sumaye,mara sumaye karudi toka chuoni na kuchukua fomu ngome yake inaanza kuvunjwa,in maana ubadhirifu wa maregesi umejulikana jana tu?na je yeye ndo mbadhirifu kuliko EL,malecela,JK n.k?

hii ndo sanaa halisi na Boyz II Men ndo wameanza,hadi kufikia 2010 nadhani nchi hii na CCM kwa ujumla watakuwa wamejua maana ya hotuba ya Nyerere ile ya mwaka 1995 wakati alipowakataa hwa B II M.

ibambasi,

Naomba nitofautiane na wewe lawaka kuzipeleka kwa boyz II men; kuna mambo mawili hapa:-

1. Unamaanisha wajumbe wengine wote (33) ni Bendera hufuata upepo kwa maana ni wajinga kabisa.hawawezi kukataa chochote boyz II men watakachosema kama kweli wanafanya hivyo.

2. Unalazimisha hisia zako watu wazichukue juu juu na haya ndio wanasiasa wengi wamewalazimisha wananchi wetu kuamini mambo yasiyokuwepo.

Hongera kwa majungu!!!!
 
1) Kwanza lazima watu wafahamu kwamba Maregesi, si mtu wa kuaminika. Ni mtu wa kukurupuka ndio maana aliamua kujitangaza kuwa anamuunga mkono Sumaye na Sumaye ndiye atakua Rais. Sumaye kwa udhaifu wake, alishindwa kumdhibiti na habari zinasema aliendelea kufanya mambo ya aibu na ambayo kwa kiasi kikubwa pamoja na matatizo ya Sumaye, MAregesi alichangia kutia chumvi katika kidonda. kwa hiyo suala la kua ni mchafu halina ubishi.

2) Pili hapa kumeibuka mjadala wa mtandao kuanza kazi ya kuandaa timu yao kuelekea chaguzi zijazo, na kutawala bila kubanwa.. hilo nalo halina ubishi. Hii ni siasa, hakuna mtu atakayeacha kutumia silaha alizonazo eti kuogopa kelele zenu kuwa oooh, taifa litagawanyika, oooh, sijui CCM itamegeka, hayo yote wanayajua na jinsi ya kuyakabili wamekwishajiandaa pia.

3)Ama kuhusu ni jinsi gani wataweza kutawala wajumbe wa vikao vya Kamati Kuu, hilo halina ubishi kwani wajumbe wengi ni wale walioteuliwa na JK kuunda sekretarieti ya CCM akiwamo Rostam Aziz na EL ambao hukaa pamoja katika vikao hivyo.

4) Kataraiya naye pamoja na kuwa alikua na misimamo yake, hoja yake inabebwa na maana nyingi, ikiwamo mapambano ya kisiasa mkoani Mwanza na zaidi kanda nzima ya ziwa. Kwa walio Mwanza wanajua maana yake nini.

5) Taarifa zote za magazeti ya jana ambazo zimekanushwa leo na CCM ziinaonyesha kutoka katika chanzo kimoja, na sina shaka chanzo hicho ni hao hao akina EL ambao wanapima upepo kuona umma utapokeaje, na hivyo kuwaandaa kisaikolojia kabla ya kufanya vitu vyao... Sawa na mtu ambaye amekufa, anaambiwa kavumishiwa kifo na kwamba anapumua kwa mashine na baada ya siku ama saa kadhaa unaambiwa AMEKWISHAFARIKI DUNIA... Hapana shaka Maregesi na Kataraia si wa kupona, na kama watapona kikao cha sasa basi wajue hawataendelea na nyadhifa zao baada ya uchaguzi ujao wa chama.

TAARIFA ZINASEMA WAZEE WANAOTA
 
Samahani sehemu ya mwisho inayosomeka WAZEE WANAOTA.... nilitaka kuandika hivi, WAZEE WANAOTAJWA KUWA WANATAKA KUKATWA MAJINA WAMEPITISHWA AKIWAMO SUMAYE AMBAYE ANAWAKERA SANA WATU, WANASEMA,
"KWANINI HAONDOKI, ALISHAKULA WAKATI WAKE SASA ATUACHE NA SISI TULE"
 
MAREGESI Kafukuzwa rasmi pamoja na Thomas Nyimbo, naye kazuiwa kushiriki ktk chaguzi kwa kukiuka maadili, CC pia wamewavua madiwani wake pamoja na mwenyekiti wao wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru
 
Halisi,
Hii mindset ya kula ndiyo inayotupeleka pabaya. Siku hizi hakuna cha "niifanyie nini nchi yangu," bali ni zamu yetu pia kula.
 
NILISEMA, CCM wana mambo, wamesema "BADO HAJAFA" wakipima upepo, sasa wametangaza rasmi, Maregesi ameng'olewa Uenyekiti wa WAZAZI maana yeke ni kwamba si mjumbe wa KAMATI KUU TENA
 
1. Unamaanisha wajumbe wengine wote (33) ni Bendera hufuata upepo kwa maana ni wajinga kabisa.hawawezi kukataa chochote boyz II men watakachosema kama kweli wanafanya hivyo.

2. Unalazimisha hisia zako watu wazichukue juu juu na haya ndio wanasiasa wengi wamewalazimisha wananchi wetu kuamini mambo yasiyokuwepo.

Hongera kwa majungu!!!!

Kama EL anaweza kuwafanya wabunge zaidi ya mia mbili kufuata upepo na wakaacha kujadili masuala ya maana atashindwa vipi kwa watu 33 pekee?
 
MBUNGE wa zamani wa Njombe Mashariki, Thomas Nyimbo,
amepigwa STOP na KAMATI KUU YA CCM kuwania nafasi ya uongozi ndani ya Chama hicho.

MBALI YA NYIMBO CCM pia imewavua uanachama madiwani wake watano akiwami Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Tunduru mkoani Ruvuma, Burhan Makonjekwa madai ya utovu wa nidhamu.
 
Mr. Zero,

Tunaweza kufika bila kujua au kutofika popote kwa kuwa hatujui tunaenda wapi?

Kama unajua tunapoenda tafadhali nihabarishe!!!
 
Mambo yako sawa ndani ya CCM, ila hayako sawa kwetu walalahoi, CCM are doing just fine, hata siku moja hawatakuja kugombana kwa faida ya sisi wananchi at large, ila wao hugombana kwa faida zao binafsi tu,

Kwa mfano kabla ya uchaguzi wa rais uliopita Muungwana na Mwandosya, walikuwa hawaongei kabisaaa, leo Mwandosya ni waziri kwenye serikali ya Muungwana! Kumbuka mchezo wa rais Mwinyi, nitaacha! nitaacha! nitaacha! mpaka akamaliza term mbili!

Do not believe the hype my brother!, hizo hadithi za abunuwas ni njama tu za kuendelea kututawala milele!
 
Back
Top Bottom