Ndugu wanaForum , nianze kusema Kidumu Chama Cha Mapinduzi!!! Kama siyo CCM niseme Habari Yako!!
Chama Cha Mapinduzi {CCM} kitaanza Uchaguzi wa Viongozi wake kutoka Ngazi ya Shina hadi Halmashauri Kuu ya Taifa kwanzia tarehe 20 Mwezi huu.. Kuelekea huko lazima kuwe na matukio au taarifa mbalimbali. Naam tuanze basi leo kwa habari ifuatayo nayo ni :-
Kutoka Gazeti ; Mwananchi
Ally Sonda, Kutoka Moshi Anasema
BAADHI ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro, wameanza utekelezaji wa agizo la kutowachagua viongozi ndumilakuwili katika uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika hivi karibuni.
Agizo hilo lilitolewa hivi karibuni na Mlezi wa Chama hicho mkoani humo, ambaye pia ni Waziri Mkuu, Edward Lowassa .
Mwananchi limebaini kuwa, utekelezwaji wa agizo hilo , unafuatia kuundwa kwa makundi maarufu kama kambi ya kampeni za baadhi ya wanachama wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.
Kambi hizo tayari zimeanza kazi ya kuwanadi wagombea wao na wakati huo huo, zikiwatangaza wagombea wengine vibaya.
Mwanakambi mmoja wa mgombea (jina la nafasi linahifadhiwa) ameliambia Mwananchi jana kuwa, makambi mengi yaliyoundwa ni ya kuwanadi baadhi ya wagombea wa nafasi za uongozi ngazi za wilaya na mkoa.
Amezitaja baadhi ya nafasi ambazo tayari wagombea wake wameunda makambi ya kampeni kuwa ni ya uenyekiti wa mkoa, uwakilishi wa halmashauri kuu ya taifa kutoka Kilimanjaro , ukatibu uenezi na uweka hazina wa mkoa.
" Sasa hivi ndugu yangu wanaume na wanawake ngangari wapo kazini, kampeni hazijaanza lakini pitapita imeanza, ni lazima tutekeleze agizo la Lowasa.... wale ndumilakuwili lazima tuwajue mapema na tuwang'o, " alisema mwanakambi mwingine.
WanaCCM hao, walisema kuwa baadhi ya viongozi waliokisaliti chama hicho mwaka juzi kwenye uchaguzi Mkuu hususan Jimbo la Moshi Mjini, wana uwezo wa kujieleza kisiasa, hali ambayo imekuwa ikiwawezesha kurejeshwa tena kwenye uongozi.
" Hawa viongozi wetu wanaotoaga siri za mikakati ya Chama kupata ushindi na kuipeleka upande wa upinzani wana uwezo mkubwa wa kujieleza jukwaani wakati wakiomba kura..baadhi yao siasa wanaijua, lakini mwaka huu tunawangofoa, kauli ya Lowassa ni nzito lazima ifanyiwe kazi kwa faida ya Chama.
Mwananchi ilipomuhoji jana kwa njia ya Simu, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kiliamnjaro, Vicky Nsilo Swai endapo ameunda kambi, alisema yeye hana haja ya kuunda kambi wala kikundi cha kampeni kwa madai kuwa wapiga kampeni wake ni wanachama wote.
" Wewe unataka niwe na kambi au unaniuliza kama nina kambi mimi sina kambi ya kampeni, kambi yangu ni wanaCCM wa Mkoa wa Kilimanjaro, wanajua nimewafanyia nini kwa miaka mitano sasa," alisema Vicky na kukata simu yake.
Baadhi ya wanachama wamebainisha kuwa kiongozi yeyote wa CCM kuanzia ngazi za mashina hadi mkoa aliyetimiza wajibu wake baada ya kuchaguliwa mwaka 2002, atarejeshwa tena kwenye uongozi, endapo atawania tena, mwaka huu.
Akiwa mjini Moshi mwanzoni mwa mwezi huu Lowassa ambaye pia ni Mlezi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, aliagiza wale wote waliokihujumu chama wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka juzi, wasichaguliwe tena kwenye uchaguzi wa chama mwaka huu.
Hapo Hapo
Kutoka Gazeti la Mwananchi
Mussa Juma, Kutoka Arusha Anasema
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Arusha kimeingilia kati mgogoro ulioibuka kati ya wakazi wa Muriet Kata ya Sokoni 1 na Manispaa ya Arusha baada ya kutakiwa kuvunja nyumba zao kupisha mradi wa upimaji viwanja.
Habari kutoka ndani ya CCM ambazo zilithibitishwa na Katibu wa Wilaya, Ngang'aso Ndekubali na viongozi wa CCM wa Kata hiyo na Murieti, zimeeleza hatua hiyo kuingilia kati mgogoro huo imekuja baada ya kubaini kuna mapungufu katika utekelezaji agizo la manispaa.
Viongozi wa juu ya chama hicho, juzi walipanga kufanya mkutano wa hadhara na wakazi hao, lakini walishindwa baada ya kuzuiwa na mvua iliyokuwa ikinyesha.
" Ni kweli tulikuwa tupite pale lakini tulikuwa na mambo mengine pia ikiwepo huu ugonjwa wa homa ya bonde la ufa, " alisema Ndekubali.
Hata hivyo, alisema kitendo cha wakazi hao kufungua kesi kinaweza kuwazuia kushughulikia suala hilo.
Kata ya Sokoni 1 kilipo kitongoji cha Muriet inaongozwa na Diwani wa Tanzania Labour Party (TLP), Michael Kivuyo na habari za uhakika zinaeleza kuwa kama manispaa hiyo, itavunja nyumba hizo Serikali ya CCM itaendelea kupingwa katika kata hiyo.
Kwa zaidi ya miezi miwili sasa kumeibuka mgororo mzito katika eneo hilo hasa baada ya Manispaa hiyo kuwapa notisi wakazi hao ya kuvunja nyumba zao, ndani ya siku saba, la sivyo itazivunja.
Notisi hiyo ilimalizika mapema wiki iliyopita, lakini hata hivyo, kabla ya manispaa hiyo kuanza kutekeleza amri hiyo, wakazi hao wamefungua kesi na kupinga kuporwa eneo lao.
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Job Laizer amekuwa akidai eneo hilo ni mali yao ambalo walikabidhiwa na Shirika la Mifugo la TLMP miaka 20 iliyopita, wakati wakazi hao, wanadai ni mali yao na kwamba eneo holo linamilikiwa kimila tangu enzi za ukoloni na ndiyo sababu iliyoifanya manispaa hiyo, mwaka 1999 kuomba ekali 60.
NB: Nitaendelea kutoa taarifa kutoka katika makao makuu ya chama au kutoka katika vyombo vya habari mbalimbali! nchini.
Kusoma habari zaidi kuhusu Chama Cha Mapinduzi tembelea tovuti yetu www.ccmtz.org
Hawa ndio wakuu wa CCM kwa sasa.

Chama Cha Mapinduzi {CCM} kitaanza Uchaguzi wa Viongozi wake kutoka Ngazi ya Shina hadi Halmashauri Kuu ya Taifa kwanzia tarehe 20 Mwezi huu.. Kuelekea huko lazima kuwe na matukio au taarifa mbalimbali. Naam tuanze basi leo kwa habari ifuatayo nayo ni :-
'Ndumilakuwili CCM' K'njaro matumbo moto
Kutoka Gazeti ; Mwananchi
Ally Sonda, Kutoka Moshi Anasema
BAADHI ya wanachama wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Kilimanjaro, wameanza utekelezaji wa agizo la kutowachagua viongozi ndumilakuwili katika uchaguzi mkuu wa chama hicho utakaofanyika hivi karibuni.
Agizo hilo lilitolewa hivi karibuni na Mlezi wa Chama hicho mkoani humo, ambaye pia ni Waziri Mkuu, Edward Lowassa .
Mwananchi limebaini kuwa, utekelezwaji wa agizo hilo , unafuatia kuundwa kwa makundi maarufu kama kambi ya kampeni za baadhi ya wanachama wanaowania nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya chama hicho.
Kambi hizo tayari zimeanza kazi ya kuwanadi wagombea wao na wakati huo huo, zikiwatangaza wagombea wengine vibaya.
Mwanakambi mmoja wa mgombea (jina la nafasi linahifadhiwa) ameliambia Mwananchi jana kuwa, makambi mengi yaliyoundwa ni ya kuwanadi baadhi ya wagombea wa nafasi za uongozi ngazi za wilaya na mkoa.
Amezitaja baadhi ya nafasi ambazo tayari wagombea wake wameunda makambi ya kampeni kuwa ni ya uenyekiti wa mkoa, uwakilishi wa halmashauri kuu ya taifa kutoka Kilimanjaro , ukatibu uenezi na uweka hazina wa mkoa.
" Sasa hivi ndugu yangu wanaume na wanawake ngangari wapo kazini, kampeni hazijaanza lakini pitapita imeanza, ni lazima tutekeleze agizo la Lowasa.... wale ndumilakuwili lazima tuwajue mapema na tuwang'o, " alisema mwanakambi mwingine.
WanaCCM hao, walisema kuwa baadhi ya viongozi waliokisaliti chama hicho mwaka juzi kwenye uchaguzi Mkuu hususan Jimbo la Moshi Mjini, wana uwezo wa kujieleza kisiasa, hali ambayo imekuwa ikiwawezesha kurejeshwa tena kwenye uongozi.
" Hawa viongozi wetu wanaotoaga siri za mikakati ya Chama kupata ushindi na kuipeleka upande wa upinzani wana uwezo mkubwa wa kujieleza jukwaani wakati wakiomba kura..baadhi yao siasa wanaijua, lakini mwaka huu tunawangofoa, kauli ya Lowassa ni nzito lazima ifanyiwe kazi kwa faida ya Chama.
Mwananchi ilipomuhoji jana kwa njia ya Simu, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kiliamnjaro, Vicky Nsilo Swai endapo ameunda kambi, alisema yeye hana haja ya kuunda kambi wala kikundi cha kampeni kwa madai kuwa wapiga kampeni wake ni wanachama wote.
" Wewe unataka niwe na kambi au unaniuliza kama nina kambi mimi sina kambi ya kampeni, kambi yangu ni wanaCCM wa Mkoa wa Kilimanjaro, wanajua nimewafanyia nini kwa miaka mitano sasa," alisema Vicky na kukata simu yake.
Baadhi ya wanachama wamebainisha kuwa kiongozi yeyote wa CCM kuanzia ngazi za mashina hadi mkoa aliyetimiza wajibu wake baada ya kuchaguliwa mwaka 2002, atarejeshwa tena kwenye uongozi, endapo atawania tena, mwaka huu.
Akiwa mjini Moshi mwanzoni mwa mwezi huu Lowassa ambaye pia ni Mlezi wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro, aliagiza wale wote waliokihujumu chama wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu mwaka juzi, wasichaguliwe tena kwenye uchaguzi wa chama mwaka huu.
Hapo Hapo
Kutoka Gazeti la Mwananchi
Mussa Juma, Kutoka Arusha Anasema
CCM waguswa mgogoro wa wananchi, manispaa
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Arusha kimeingilia kati mgogoro ulioibuka kati ya wakazi wa Muriet Kata ya Sokoni 1 na Manispaa ya Arusha baada ya kutakiwa kuvunja nyumba zao kupisha mradi wa upimaji viwanja.
Habari kutoka ndani ya CCM ambazo zilithibitishwa na Katibu wa Wilaya, Ngang'aso Ndekubali na viongozi wa CCM wa Kata hiyo na Murieti, zimeeleza hatua hiyo kuingilia kati mgogoro huo imekuja baada ya kubaini kuna mapungufu katika utekelezaji agizo la manispaa.
Viongozi wa juu ya chama hicho, juzi walipanga kufanya mkutano wa hadhara na wakazi hao, lakini walishindwa baada ya kuzuiwa na mvua iliyokuwa ikinyesha.
" Ni kweli tulikuwa tupite pale lakini tulikuwa na mambo mengine pia ikiwepo huu ugonjwa wa homa ya bonde la ufa, " alisema Ndekubali.
Hata hivyo, alisema kitendo cha wakazi hao kufungua kesi kinaweza kuwazuia kushughulikia suala hilo.
Kata ya Sokoni 1 kilipo kitongoji cha Muriet inaongozwa na Diwani wa Tanzania Labour Party (TLP), Michael Kivuyo na habari za uhakika zinaeleza kuwa kama manispaa hiyo, itavunja nyumba hizo Serikali ya CCM itaendelea kupingwa katika kata hiyo.
Kwa zaidi ya miezi miwili sasa kumeibuka mgororo mzito katika eneo hilo hasa baada ya Manispaa hiyo kuwapa notisi wakazi hao ya kuvunja nyumba zao, ndani ya siku saba, la sivyo itazivunja.
Notisi hiyo ilimalizika mapema wiki iliyopita, lakini hata hivyo, kabla ya manispaa hiyo kuanza kutekeleza amri hiyo, wakazi hao wamefungua kesi na kupinga kuporwa eneo lao.
Mkurugenzi wa Manispaa hiyo, Job Laizer amekuwa akidai eneo hilo ni mali yao ambalo walikabidhiwa na Shirika la Mifugo la TLMP miaka 20 iliyopita, wakati wakazi hao, wanadai ni mali yao na kwamba eneo holo linamilikiwa kimila tangu enzi za ukoloni na ndiyo sababu iliyoifanya manispaa hiyo, mwaka 1999 kuomba ekali 60.
NB: Nitaendelea kutoa taarifa kutoka katika makao makuu ya chama au kutoka katika vyombo vya habari mbalimbali! nchini.
Kusoma habari zaidi kuhusu Chama Cha Mapinduzi tembelea tovuti yetu www.ccmtz.org
CCM Oyeeeeeeeeeee!!!