Tusiwaonee sana Polisi(Nijikite Ilula-Iringa)

Tusiwaonee sana Polisi(Nijikite Ilula-Iringa)

Mleta Mada Una Laana Inayokutesa Si Bure,mtu Na Akili Zake Timamu Hawezi Kuwatetea Policcm Kwa Matendo Huwezi Kumpangia Mtu Muda Wa Kufanya Starehe Wakati Yeye Si Mfungwa,laana Inayowatesa Policcm Ndo Inakutesa Na Wewe,umeandika Ujinga Mtupu,mavi Tupu,wala Hukuishughulisha Akili Yako Kufikiri,watu Wanakunywa Pombe Kwa Starehe Zao Mnaenda Kuwakamata Bila Sababu Halafu Ulivyo Mjinga Kama Baba Yako Alivyokuwaga Anaitetea Serikali Ya Kishenz Bungeni Eti Na Wewe Unaendeleza Ujinga Huohuo,kwanza Huna Aibu Wala Fikra,serikali Inawasaidia Nini Wananchi Wewe Kenge? Zaidi Ya Kuwapora Jasho Lao? Wanajitibu,wanajisomesha Na Hata Raslimali Za Nchi Nazo Hawazifaidi Zaidi Ya Kuliwa Na Kina Kikwete Na Genge Lao,wamefanya Kazi Kwa Jasho Lao Wakaona Angalau Wakajiburudishe,eti Wanakamatwa Kwa Kunywa Pombe Wakati Wa Kazi,kwani Ni Watumishi Wa Umma Hao Kwamba Eti Walitoroka Kazini? Huna Akili Kabisa Wewe Nyambaf,na Hili Ndo Anguko La ccm.

Na hapo ndipo ashki zenu zinapodhihirika ktk masuala ya msingi kama haya. Eti PoliCCM.

Good! Tuipatie ridhaa UKAWA ili waweke na vyuo vya waharifu na mambo yaende sawa sawia.

Fikra mgando kabisa. Natamani mngekuwa Raia at least wa Zimbabwe tu hapo mkaona namna Dola linavyofanya Raia (kama mnavyotaka iwe).

Mna mambo ya ovyo sana. Any ways, you are calling for a such a systems. Tuombe uzima. Mtaikimbuka hali hii siku za mbele (pale ambapo hakuna jiwe litakalokaa juu ya jiwe lingine).

Just go on with this.
 
Unaweza kuniambia ni kwa kifungu gani cha sheria Mwenye Baa haruhusiwi kufungua Baa yake asubuhi....Na unapozuia wanywaji wasiingie unatarajia yeye apate wapi Kodi..mishahara ya wafanyakazi wake...Tatu hizo kazi unazotaka wa kafanye ni zipi zaidi ya kujiliwaza kwenye pombe.kwani kuna mahali serikakli imekuonesha ilwapangia ajira waka kataa na kuendelea kung`ang`ania kunywa pombe..Kwani hawa wapuuzi waliotoa hilo agizo hawana taarifa kwamba wananchi hao mpaka leo mazao yao waliyo lima mwaka jana bado hayajanunuliwa ...alafu unawafukuza kwa kutumia Polisi ili wakalime mengine.

Hili lililofanyika linaweza kuungwa mkono na mtu ambaye akili yake inamatatizo kidogo.Hata hao waliokuwa wakitekeleza amri hiyo akili yao haiko sawa kabisa .Wanahitaji kupimwa .Mwendawazimu siyo lazima abebe makopo .Tatizo kubwa ni kwamba baadhi ya hawa tunaofikiri kuwa polisi ni GREEN GUARD ndiyo maana wanalidhalilisha Jeshi hili na kuendelea kutokomeza hata Kaheshima angalau kidogo kaliko baki.
 
huo ndio ukwel wengi wetu tunaongozwa na mihemko ya siasa zaid kuliko uhalisia....what next hata wakulalamika? Always sioni uzito wa makosa ya police tz tumezoea kulalamika tu pasipo kuchunguza kwa makini mambo

Umewagonga nyundo utosini. Bahati mbaya huu ni ukweli mchungu kwao.

Any ways, itafahamika tu.
 
UKIWA NA TOTO JINGA KAMA TUNTEMEKE SANGA Hakika Inabidi Ukafanye Maombi Ya Nguvu Ili Upate Mtoto Mwingine Mwenye Akili Timamu. TUNTEMEKE SANGA NI GALASA HAKUNA MTU PALE.

Teh! kwa taarifa yako niko imara. Wazazi,familia na ndugu zangu wote do feel proud of TUNTEMEKESANGA.

Labda hapo ume'reflect stastus uliyonayo hapo kwenu.
 
Uchumi gani huo kama mkulima ameiuzia serikali mahindi toka mwezi wa saba hadileo hajalipwa si bora watu wale pombe tu maani ni ujinga!
 
Hichi kitendo angefanyiwa mama yako hlf ukaja kuwatetea kwa pumba zako kama ulivyotumwa ningekupa pongezi ila naamin kwako inawezekana maana huna hata chembe ya utu

Ningehuzunika actually. Lakini moyoni bado ningebaki na ukweli huu kwamba sheria ilivunjwa.
 
Moja ya vitu amabvyo hujaviongelea ni malalamiko ya wananchi, jana pale Ilula ilikuwa kama "trigger" maanan walikuwa wakilalamika police kuwanyanyasa bodaboda sana, mfano bodaboda yupo kwenye mwendo police anakuja na gari anamuwekea kwa mbele, wanasema zaidi ya watu sita wamepata vilema kwa style hiyo na mmoja amekufa lakini hatua hazichukuliwi>
Swala la pili ni kwamba kwa mfumo wa uchumi ulivyombovu huwezi wapangia watu mda gani wafanye kazi na mda gani wapumzike, wananchi wengi vijijini ni wachapakazi sana, wanaamka saa 10 kulima kufika saa4-6 wanakuwa wamemaliza wanaenda kwenye urabu, ndo maana hausikii wamepewa chakula cha msaada zaidi ya kusikia mazao yao hayana soko.
Mwisho serikali ya kijiji inakusanya ushuru kila siku pale kilabuni, na operation kama zile huwa zinafanywa na sungusungu, kuna hisia kuwa police wanawakamata watu vilabuni makusudi na kuwepeleka kituoni alafu wanaweka sharti la kila kichwa kutoa 50000-200000 ili kutoka.

USHAURI
Police ikiimarish kitengo cha mahusiano (nadhani Mwema alijaribu na ilileta mafanikio kwa kiasi kidogo).
Serikamli ianzishe kitengo maalumu cha usuluhishi wa migogoro kwenye vituo vya police vya kikanda bila hivyo maafa makubwa yasubilia, mwishi police isiwe kwa watu waliofeli darasa.

Naomba nisikupe challenge yoyote ktk mchango wako huu(pamoja na kwamba kuna mambo nilipaswa kuyaweka sawa).

Ila, kwa umuhimu wa jumla wa comment yako hii, naiunga mkono. Mawazo mazuri sana haya.
Asante.
 
Pole sana Mkuu. Mimi sijatumwa. Lakini hii ndiyo demokrasia (freedom of speech). Jikaze kisabuni.

Wewe unaoba kama unawajenga polisi kumbe ndio unaibua hasira kwa ndugu wa marehemu,sifa nyingine hazifai
 
Kwa Kuwa Wamewachokoza Wananchi Wajue Wakitoka Kazini Wanaishi Mitaani Na Familia Zao Zipo Mitaani Hilo Lazima Walijue.

Mkuu; hiyo si dhana nzuri na endelevu. Ikumbukwe kuwa, hao ni Dola. Ni vyema kweli kuwakosoa kwa nguvu zote na kuwahimiza kuendenda kwa weledi.

Lakini namna ya mtazamo wako huo, hatuwezi kushindana nao. Chukua mfano wa Syria. Serkali ikiamua kufanya upumbafu, Raia hawez akawa salama.
 
Wakuu; heshima mbele!

Napenda kuwasihi sana Watanzania wenzangu kudumisha umoja,mshikamano na uzalendo. Hii nikutokana na mambo kadhaa yanayotokea nchini kwetu(hususan current Police v/s Citizens' Laments).

Nikijikita ktk suala la juzi pale Ilula-Iringa,nimeshuhudia baadhi ya Watanzania kadhaa ktk mitandao mbalimbali ya kijamii na hata mitaani kote wakiendelea kulilalamikia Jeshi la Polisi kuwa, ni watesaji wasiozingatia misingi ya Utu.

Mimi naomba nitofautiane na malalamishi hayo(nikirejea tukio hilo hapo juu).

Ni ukweli uliowazi kwamba, Polisi walikuwa wanakwenda kutekeleza Ilani,Sheria na Utaratibu wa Nchi na Utawala-Mahalia (By-Laws),ambao ni mpango wakusimamia mienendo na taratibu za Wananchi kuhakikisha wanalisukuma vyema gurudumu la maendeleo.

Haipingiki kwamba,kuna mambo mengi sana yasiyokuwa ya msingi yanawafanya watu/wananchi kulegea na kushindwa kujihusisha kwa bidii na umakini kufanya shughuli za maendeleo. UNYWAJI HOLELA WA POMBE au ULEVI WA AINA YOYOTE, ni miongoni mwa mambo hayo.

Ni jukumu la Mamlaka kutunga sheria na utaratibu kufanya "perpendicular & mutual monitoring" kwa Raia wake ili kutimiza malengo ya maendeleo. Hicho ndicho kitendo kilichokuwa kinafanyika pale Ilula.

Si busara wala hekma kumwacha mtu/watu kuenenda katika njia mbovu badala ya kujikita katika shughuli za maendeleo kwa wakati muafaka uliopangwa.

Yule mama aliyeanguka na kufariki (R.I.P), ni wazi kwamba,ilitokea bahati mbaya (kama inavyoweza kumtokea yeyote yule), na si kwamba alipigwa au kuteswa na Polisi.




Now; malalamiko yanayoendelea kutolewa na baadhi ya Watanzania juu ya tukio hilo(yakielekezwa kwa Polisi na Serikali), si sahihi hata kidogo. Mnyonge mnyongeni,lakini Hakhi yake mpeni.

Nchi kama CHINA,S.KOREA na RUSSIA,wako Serious mno kufuatilia nidhamu za Wananchi ktk uzalishaji mali na kujituma kwa Wananchi. Naamini that's why wako juu kiuchumi. **Sasa shida inakuja wapi kwa Serikali na Polisi wa Tanzania kusimamia Nidhamu ya kazi ya Raia wake?**

MY TAKE;
Watanzania tusihemke na kukengeuka bila sababu. Tuwe wawazi na Makini mbele za Mungu. Tusihamaki bila sababu za msingi. Tujitengenezee mazingira na Saikolojia yakutii sheria halali bila shuruti,kwa manufaa yetu binafsi,kizazi chetu na kwa Taifa letu Tanzania.

Nawasilisha.


ACHA KUTUMIKA
Kumbuka wale wanafanya biashara kuna mnunuaji na muuzaji wote wanatumia pesa. Unafikiri anakunywa bure huyo? Ina maana anatafuta na hapo ndio anakwenda kutumia. Pili sio wote wanafanya kazi ya kuingiza kipato asubuhi wengine mchana, usiku na hata alfajiri kwa hiyo sio sawa kuwazuia watu wasinywe pombe asubuhi wakati hotel za nyota tano watu wanakunywa asubuhi mpaka wanakesha tuache sheria za zamani za ujamaa zilifaa kipindi huicho cha mashamba ya ushirika na sio sasa.
Kuhusu Polisi unaonekana una conflict of interest otherwise hajitambui, Polisi wanakwenda kuchukua rushwa tu pale hamna lolote na kwa taarifa kutoka watu wa karibu ni siku kadhaa tu [polisi walikwenda kuchukua elf 20 hapo za faini.
Na si kweli huyo mama amekufa kwa kudondoka bali kwa kupigwa mtama na polisi leo kwao, kesho kwako uwe na utu.
Nitakupa mfano kwenye vurugu kati ya mechi ya Majimaji Songea vs Kurugunzi walipigwa watu wawili viongozi wa UVCCM mmoja alikuwa anawalinda wachezaji wa timu ya wanawake mkoa wa ruvuma na mwingine mchambuzi wa soka so kwa kufikiria wao ni viongozi wa UVCCM kwamba hawatapigwa wpai walipata mkong'oto wa polisi bila kuangalia kama ni viongozi wa timu na uvccm kwa hiyo kuwa makini hao plc huwa hawaaangalia mtu iko siku wata kusulubu ndio ujue kuwa wanakosea.
 
Kwa taarifa yako, kuna baadhi ya sectors huko hufanya kazi zaid ya masaa 8. Sometimes hadi usiku kucha(over working). Na of course muda wa kazi unafahamika (hususan kipindi cha kazi au msimu wa Kilimo kwa Bongo).

Sasa M-Tz anagusa ofisini saa moja then anachepuka bar jirani kunitundika! Au Baba anatelekeza kazi za shambani kwa mke na watoto then anashinda kutwa nzima,wiki & mwezi mzima Bar anakunywa wanzuki,mnazi, #Ulanzi na kadhalika. Unatarajia jamii & Taifa litasonga mbele?
Kwa nini hao Police wasianze na Officers Mess zao ambako bar inafunguliwa asubuhi na utawakuta wapo wanapata safari baridi na supu asubuhi, au ndiyo yale ya kunya anye kuku akinya bata kaharisha?
 
Unakandamizwa wewe!

Umemuona mpugususu huyo? Mambo mengine mtu inabidi ucheke sana tu! Eti alikuwa muuza chakula.

Na jamaa zetu hawa wamejikita ktk upuuzi na mihemko tu badala ya uhalisia. Sasa nadhani umeona wanavyotapika ovyo.

Tanzania bwana!!
 
Si kweli mkuu. Hapo utakuwa unataka kuniziba mdomo.

Tuntemeke mimi ni mtu muelewa sana na najua nini maana ya jukwaa kama hili,tukio la hayo maafa limetokea jana tu hata bado maiti haijazikwa wewe unaanza kuleta utetezi kama huu?unataka kutuambia kuwa jambo likifanywa na polisi sisi raia hatuna nafasi ya kulaani hilo tukio?
 
Mkuu, hakuna asiyejua uchungu huo. Hata Mama wa Jambazi(mfano) hulia pale mwanae anapouawa kwa tukio la uhalifu.

Wakati fulani, haiwezekani mtu kukiuka utaratibu halafu akaachwa hivihivi. Dhana ya Mamlaka na Utawala bora itakuwa imekufa asilani.

Tuwe tayari kuupokea ukweli. Bahati nzuri mama-muza hakuuawa kwa kipigo wala kuteswa.

Mama wa watu Muuza Pombe au Makongoro ya Miguu KIFO chake unalinganisha na Jambazi ...hongera wewe familia bora !!!!
 
Back
Top Bottom