Buyaka
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 1,781
- 2,077
Commentators wengi wa Uislam wanasema uislam kwa asilia unafundisha extremism. Kwa experience yangu, waislam wengi niliokutana nao ambao nimehisi wana elements za extremism unakuta hawana elimu sana. Kwa hiyo nadhani muislam ambae amesoma decently ni vigumu kuchotwa na extremism hata kama Quran ina strong elements za extremism.Dini zingine hata uwe umesoma kiasi gani, ule mtazamo uliokaa ki-udini unakuwa hautoki.
Kuna muislam mmoja nimeongea nae akanambia wanae ni bora wazingatie zaidi madrassa na elimu ya uislamu kuliko shule ya kawaida. Nikamwambia huoni kwamba wewe kutosoma vya kutosha ndio sababu ya kusukuma mikokoteni juani mchana kutwa, akadai ni kweli lakini maisha yetu baada ya kifo ndo muhimu zaidi ya haya duniani. Sasa nadhani mtazamo kama huo kwa mtu mwelewa, msomi, ambae amefaidika na elimu, hawezi kuwa nao, sidhani kama Muislam msomi anaweza kukubali mwanae asende shule aende madrasa. Na ambae anaona maisha ya hapa dunia si chochote mbele ya dini ni rahisi zaidi kukubali kujilipua kwa ajili ya Uislam.
Inawezekana nakosea sana.