Tusio na kazi tukutane hapa

Tusio na kazi tukutane hapa

Ndugu zangu huu uzi wangu niliuandika mwaka jana, ila mpaka sasa sijapata kazi yeyote, naombeni mnisaidie
[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]

Naomba msaada wako ndugu yangu


Habarini za muda huu mpendwa

Pole na miangaiko ya hapa na pale, ya kuhakikisha tunajenga familia zetu vyema na taifa letu la Tanzania kwa ujumla.

Kwa wale wagonjwa/wanaouguza poleni sana na mwenyezi mungu mwigi la lekhema awape nguvu mpya na kuwaponya kabisa ili mrejee kwenye majukumu yenu ya awali.

Niende kwenye maada moja kwa moja

Ndugu yangu Mimi ni mtanzania mwenzako ninapitia wakati mgumu sana nahisi kuchanganyikiwa maana umri pia unasonga sana na sina chochote.

Kwanza kabisa nikili mbele zenu napenda sana kuja kuwa "Mfanya biashara" kwanini sikufanikiwa uko

Nilipomaliza Elimu yangu ya Diploma (diploma in computer science )

Nilipenda nipate mtaji ili nifanye biashara, kwanza kabisa ilinilazimu kutafuta kazi ili nipate mtaji na pa kuanzia...

niliangaika sana na kutafuta kazi yapata mwaka mzima pasipo kuambulia chochote...

Note: aliyenisomesha diploma ni ante yangu, pesa yake alipenda kuitoa kwa kunisomesha tuu na sio vinginevyo (ndio msimamo wake ulikuwa ivyo)...

Nilisha jaribu kumshawishi kwa namna moja ama nyingine anisaidie mtaji wa kiasi fulani ili baada ya mzunguko wa biashara nitairejesha pesa yake yote, alikataa alisema "kama unataka kuendelea na shule ntakulipia ada ila sio mambo ya biashara"

Baada ya kuona mambo si shwali ilinilazimu kurudi tena chuoni kwa ngazi ya "bachelor degree "

Nilisoma na kumaliza, alijitahidi kunilipia sehemu ya ada yangu yote... (mwenyezi mungu ambariki sana)

Ndugu yangu nimeangaika sana kutafuta sehemu ya kujishikiza pasipo mafanikio yeyote yale, kila siku nimekuwa mtu wa kuamini uwenda bahati yangu yaja....ila giza kwangu naona linanizonga sasa..

Ndugu yangu poleni kwa maelezo marefu sana hapo juu

Naombeni msaada wenu wa kazi yeyote halali nipo tayari kuifanya kwa ajili ya kuhakikisha kampuni/taasisi/au mtu binafsi, usika inakuwa na kufikia kilele cha mafanikio tarajiwa

Mungu awabariki sana nyote

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana, ukiona giza linazidi usihofu jua kwamba kuna karibia kupambazuka.
Nichukue fursa hii kukuombea upate kazi unayohitaji.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
shortly kupata ajira n kaz sana,maana kazi ukiitaka mda wowote unaipata mfano unaweza ukaamua uchimbe tu shimo hyo n kaz ila hutolipwa,ajira inaambatana na malipo
nami n mhanga wa ajira,kfup inachanganya akili unaweza ukaenda kujisaidia haja ndogo ukachutama kwa mtoto wa kiume,maana unaanza na kuisahau hta jinsia yako kwa msongo wa mawazo,jero tu kwako lnakuwa utata,najiombea na sijakata tamaa nam niwe ktk ajira maana hata kujiajir kama huna capital hauwez
 
Nimejikuta nawaza tu, kwanini tusiwe na jukwaa la watu tusiokuwa na kazi rasmi za kufanya.

Wengine tumetumbuliwa hivi karibuni, wengine wamemaliza vyuo bado wanatafuta na wengine wana kazi lakini siyo ya maana ili mladi tuu siku ziende.

Hata mwenye job vacancies anaweza akatupata humu tukasaidiana maana hali hii siyo kabisa.

Vyuma vimekaza kila kona. Tujipigishe zetu story humu tujuzane ilikuwaje ukajikuta huna kazi.

Karibuni wadau.
kama kweli mtu hana kazi aje tulime wote mshahara utakua 200 baada ya mavuno ila awe mvumilivu sana atajifunza mengi atakula atalala

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom