Tupeane makavu: Kama pombe ni dawa ya kulevya yenye madhara makubwa kuzidi bangi ni kwanini bangi isiruhusiwe?

NetMaster

JF-Expert Member
Sep 12, 2022
1,454
4,853
elon-musk-security-clearance.jpg



Madhara ya sigara:

Ocean road pale hospitali ya cancer wapo wagonjwa wengi wenye kansa ya mapafu, fizi, koo, n.k. kwasababu ya matumizi ya muda mrefu ya sigara. Cancer inaharibu koo kiasi kwamba wengine wamechomolewa makoo wanaongea kwa kuwekewa mashine, sauti inatoka kwenye spika

Watu zaidi ya elfu moja wanakufa kwasababu ya sigara kila siku

Madhara ya Pombe.

Hii ndio ina madhara makubwa zaidi, takribani watu milioni 3 hufa kwa jili ya pombe kila mwaka aidha kwa magonjwa inayosababisha, ajali, n.k.
  • Huchochea uzinzi (huwa inashuka chini)
  • Ugomvi - hupunguza uwezo wa kucontroll hasira.
  • Kutukana matusi - Mdomo utasema unachotaka
  • addiction / uraibu
  • imefanya wengi kufukuzwa kazini hadi mawaziri
  • Kuzima
  • Kutembea kwa kupepesuka bila balance
  • kujisaidia hadharani
  • Maumivu ya kichwa

Bangi:

-Haisababishi kansa yoyote, Inatibu kansa.
-Haitoi umakini wa kazi kama ilivyo kwa Pombe mtu akiitumia anavuruga kazi hata iwe ya kuhutubia tu.
-Ina addiction ndogo na ni rahisi kuacha ukitaka kuacha, sio kama pombe na sigara,
- Hakuna vifo vinavyosababishwa na bangi kwa magonjwa


Ni kwanini baadhi ya watumiaji wa Bangi wa Tanzania wanapatwa na madhara kiakili tofauti na nchi zingine, kwanini iwe Tanzania na sio kwengine ?

Elimu ndio ufunguo wa kuweza kuyaishi haya maisha, ukitumia kitu bila kuwa na elimu nacho utapatwa na madhara, nikiri wazi kwamba watumiaji wengi wa kilevi hiki wanakurupuka kukitumia bila kujua chochote zaidi ya kuiga na matokeo yake Bangi huonekana mbaya.

- Watu hutumia bangi ambayo maua yake bado hayajakomaa vizuri na wao hawajui kutambua.
-Kinachovutwa ni maua tu, watu huvuta mpaka majani, vijiti na mbegu na kupata madhara zaidi.
-matumiz ya bangi iliyovunwa ikiwa bado mbichi
-Matumizi ya bangi ambayo baada ya kuvunwa haijaoshwa wala kukaushwa vizuri
-Bangi za mtaani kwa kiasi kikubwa zimechanganywa na sumu za panya na madawa ya kulevya.
 
Bangi ni dawa aibu viongozi wetu wanaotumia matako kufanya maamuzi ndio wanaizuia.
Hata elimu yetu naona haina msaada wowote tunaposhindwa kujinasua katika sheria za kikoloni bila ya sisi kujiongeza kuona kipi hakikuwa sawa, ajabu ni kwamba mapolisi wenye F za biology ndio wanasikilizwa bada ya kuwaachia jukumu hilo wanasayansi
 
Nasema Hivi...Tumechoka Kunyanyaswa,Kudharauliwa,Kuzingiziwa,Kuaibishwa,Kufungwa,Kulazimishwa Na Kuonekana Wabaya Kisa Mtazamo Hasi Wa Serikali...

Bangi Imewatajirisha Mapusha,Watasha Na Wakulima...

Bangi Inawapa Faraja,Starehe,Amani,Utulivu,Stimu,Akili,Ujasiri Kwa Wavutaji...

Ni Muda Wa Serikali Kuchukua Mapato Kwenye Bangi Ili Kwa Pamoja Tusaidiane Kuinua Uchumi Wetu...

Sasa Kinachosikitisha Serikali Imekalia Unoko,Majungu,Umbeya,Unafiki,Uchawi,Wivu,Fitina na Ushambenga Eti Bangi Ni Madawa Ya Kulevya!!!!

Madawa Ya Kulevya Ya nyoko.
 
kuna vijana walikula bangi wakawa wanaogopa kukanyaga changarawe mwengine akawa akikanyaga changarawe anacheka niliwacha pale njiani sijui kama walifika wanako ishi
 
Bangi ni chanzo cha magonjwa sugu ya akili (ukichaa) ikifuatiwa na ugumu au changamoto za maisha. Wakati sigara ikiua mapafu, bangi uua akili na kuudhoofisha mwili.

Elekezeni juhudi zenu hizi za uanaharakati wa uvutaji bangi katika kuhamasisha "kilimo-biashara salama na chenye mipaka" cha zao la bangi, Kwa kuwa ni zao la kiuchumi na lina manufaa japo lina madhara makubwa pia kwa watu wetu.

Serikali ihakikishe kilimo hiki kinasimamiwa na chombo maalumu, uzalishaji ufanyike katika maeneo maalumu kwa uwekezaji mkubwa na kitaalamu zaidi na asiruhusiwe mwananchi yeyote kufanya kilimo hiki kiholela.

Suala la udhibiti liwe ni kipaumbele kama ilivyo sasa maana tukiteleza kidogo tu tumeangamiza kizazi, na utumikaji wake huwe wa kimanufaa tu viwandani huko kwa ajili ya wakemia kutengeneza madawa ya kuponya watu na siyo uvutaji.
 
Bangi ikirusiwa watu watapunguza kuvuta sigara na kunywa pombe, mapato ya Kodi ya nchi nyingi yatashuka
 
Nasema Hivi...Tumechoka Kunyanyaswa,Kudharauliwa,Kuzingiziwa,Kuaibishwa,Kufungwa,Kulazimishwa Na Kuonekana Wabaya Kisa Mtazamo Hasi Wa Serikali...

Bangi Imewatajirisha Mapusha,Watasha Na Wakulima...

Bangi Inawapa Faraja,Starehe,Amani,Utulivu,Stimu,Akili,Ujasiri Kwa Wavutaji...

Ni Muda Wa Serikali Kuchukua Mapato Kwenye Bangi Ili Kwa Pamoja Tusaidiane Kuinua Uchumi Wetu...

Sasa Kinachosikitisha Serikali Imekalia Unoko,Majungu,Umbeya,Unafiki,Uchawi,Wivu,Fitina na Ushambenga Eti Bangi Ni Madawa Ya Kulevya!!!!

Madawa Ya Kulevya Ya nyoko.
naziona hisia zako Askari wangu
 
Back
Top Bottom