Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Sababu imani yao yataka hivyo.

Ila huyu imani yake ni tofauti na kwa mujibu ya imani yake ya kikatoliki si kosa,mwisho wa siku atazikwa kwa misingi ya imani yake ya kiroho ya Roman Catholic.
Nafahamu imani inahusu. Ndio maana nikasema angekua mwislamu ingekuwa tofauti.
Kwa Catholic nadhani hata akizikwa baada ya miezi kadhaa poa tu.
 
Hapana @Jurjani usione ukweli wako kwa mtazamo wako ni ukweli wangu..
Ukweli una tabia moja ya ajabu sana, na juu yake haukaliwi na chochote. Ukweli ni kuwa kama kweli wewe ni mkweli na nafsi yako inashuhuduia,basi ungekiri hili na kuacha kujadili hili sababu liko wazi sana, na hili liko wazi na nilio uandika ni ukweli wa wazi kabisa, ndio maana kuna swali katika nukta moja wapo huko juu hujalijibu.

Pili, nilichokiandika hapa kimemili katika elimu na misingi yake, ndiyo maana nimegusa pande zote, upande wako wangu,wetu na upande ulio dhidi yako.

Tatu, ukweli hauna upande mzee, ndiyo maana huwa mchungu.

Nne, hizi ni falsafa dhaifu za kusema ya kuwa kuna ukweli wa namna unavyojitokeza kwa mtu, yaani wewe uwe na ukweli wako,mimi niwe na wangu tena katika jambo moja. Hapa walio leta hii nadharia walifeli na kuwadanganya watu, ukweli ni MMOJA.
Mimi ni mwadilifu na huwa nikikengeuka nakubali kurelebishwa kwakuwa si mkamilifu na huwa naomba na radhi pia
Kaka usiwe unapoteza muda katika jambo ambalo hata ukipewa miaka na mikaka huwezi kulipinga kielimu, na hapa unadhihirisha hilo. Wewe si muadilifu. Sasa hili iweje linakushinda kwamba umekosea ? Kwanini usikiri hilo ?

Ni wachache sana huwa wanawapa stahiki zao wale wanao wachukia au wale ambao ni maadui zao, hao ni wenye elimu na uchajimungu, sababu huwa wanafanya mambo kwa ajili ya kumridhisha Mola muumba na si kujifurahisha, au kutafuta sifa au mfano wake.
note hii kitu inaitwa ukweli usiegemee sana kwake kwakuwa ukweli hubadilika kulingana na mazingira, imani, hulka na mitazamo...
Kwanza ngoja nikufundishe jambo kuhusu tamko UKWELI, nilichokiona hujui maana ya tamko hili, ndiyo maana linakusumbua na kutoka nje ya mipaka yake.

UKWELI ni kauli au kitendo kinapo afikiana na hali halisi. Maana yake ukweli hauna egemeo, bali unasimama wenyewe popote pale. Ukweli haubadiliki sababu katika ukweli kuna hayo yoyote, yaani itifaki huzingatiwa.
Napenda uhalisia kwakuwa hauna rangi nyingi hivyo haubadiliki wala haubadilishwi
Sasa mbona huu uhalisia wa wewe kumili katika hisia zaidi hutaki kuukiri au kwa sababu uko dhidi yako...?

Waja wema na wenye elimu, walisisitiza sana kutokupendelea kumzungumzia sana yule usiyempenda kwa kuchelea ya kuwa ni rahisi sana kumdhulumu, kumtuhumu na kumfanyia mbaya mengine kisa tu humpendi au mfano wake.
 
Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...

Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk

Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.

Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali

Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Hakuna cha padiem wala sijui naiti! Hata bure waweke mikoa yote watu walidhike! Wale wasiopenda mnaweza mkahamia Somalia tu!
Rest in Power Mwamba!
 
Yani hadi Nyerere umempiga teke!,kweli wewe mataga og.
Muache mwendazake aagwe..
Kiukweli anapendwa...
Waacheni wananchi wapate fursa..
Kiu ni kubwa.....

Ukiacha mwalimu hatujawahi pata jemedari kama huyu...
 
Muache mwendazake aagwe..
Kiukweli anapendwa...
Waacheni wananchi wapate fursa..
Kiu ni kubwa.....

Ukiacha mwalimu hatujawahi pata jemedari kama huyu...
Ukiacha mwalimu ambaye wengi hatukupata nafasi ya kuona uwezo wake, Mwinyi pia wengine akili za kisiasa hazikuwepo, Ila huyu mwamba ni alikuwa njema sana, yaani ukisikia BOLD, the man was BOLD...dadeq, kupata watu wa calibre hii ni nadra sana, anayekuambia ukweli huku mnatazamana. Watanzania wengi hatuwezi hilo, ni majungu na unafiki tu, this man sijui tu!
 
Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...

Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk

Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.

Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali

Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Moja katika mambo mazuri katika dini ya Kiislamu ni hili la mazishi. Nawapa pongezi ndugu zangu waislamu katika hili
Leoo hii jpm angekuwa muislamu haya yote usingeyaina angeshazikwa na mambo mengine yangekuwa yanaendelea muda huu.
Hata yale inasemwa alikufa siku nyingi ila haikutangazwa mapema ingekuwa kwa ndugu zetu waislamu kamwe hilo lisingetokea
 
Nakuunga mkono sana! Tunajihangaisha zaidi na mwili-mfu kuliko mwili-hai. Mwili-mfu ni mavumbi tu, ni utupu. Mwenye nao kaondoka, hatuoni, hatusikii wala hahisi chochote!

Mwili-hai unabeba mtu halisi ambaye ni nafsi na roho yake. Huyo ndiye tumjali zaidi, na si mwili-mfu anaouacha.
Aisee!
 
Back
Top Bottom