JF ya sasa uwezo wa kujadili hoja umepungua sana... Hoja hujibiwa kwa hoja..kinyume cha hapo ni mahoka
Kwasasa kwenye hoja nyingi kinzani, malumbano hutoka kwenye hoja na kuhamia kwenye vioja, vijembe na kejeli ama la kumjadili mtoa hoja....!!!
Usipate shida kushughulika na maneno hayo mawili,sababu moja halikai bila ya mwenzake. Ukweli ndiyo uhalisia wenyewe, ndiyo maana kwenye maana ya Ukweli unakuta ni kuafikiana na hali halisi, uhalisia huanza.Asante kwa bandiko refu lenye ufafanuzi wa yale niliyoandika.. Hitimisho ndio limetoa muktadha wa yote uliyoandika
Bado tunapushana kwenye ukweli na uhalisia... Nitakapopata muda nitakuja na mada inayojitegemea kuhusu ukweli na kuhusu uhalisia..
Alisharudi kwani umechelewa kudandia treni?Ewaaaaa adi Yesu atakapo rudi
Duh kwaiyo ni wana nchi wanyonge wame nunua hayo maua sio?TUNAONA MKISUTWA NA ROHO ZENU WENYEWE KWA JINSI WANANCHI WANAVYOONYESHA HISIA ZAO.
KULIKUWA HAKUNA WIZI WA KURA BALI WAPINZANI MLIKATALIWA LIVE!View attachment 1730829View attachment 1730830
Kwa akili yako hapa treni ipo wapi?Alisharudi kwani umechelewa kudandia treni?
Inaonekana hujaelewa nilichokiandika, maelezo yangu yamejikita kwa Maiti, ambaye kiiamani nimeelezea ya kuwa maisha yanaendelea na yapo ambayo yanaendelea muda huu sisi hatuyaoni.Kwasasa hatuongelei tena mtu hai... Bali mwili wa mwendazake ... Sasa kinachotokea hapa ni vitu viwili tofauti kabisa ....Mwili wa marehemu na marehemu! Ukweli ni upi? Uhalisia ni upi? Hapo ndio tunaachana njiapanda
Imeshaenda nbinguni na YesuKwa akili yako hapa treni ipo wapi?
Maraisi wote ni wazanzibar kwahiyo issue yakupeleka Mwili wa JPM ZNZ imekua simple tuKuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...
Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk
Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.
Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali
Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Hao adui zako watakuja kujipiga 🤳, hawa 👇 unafikiri ndio sampuli hiyo?Kujaza watu msibani haina maana unapendwa, kuna wabaya wako wanakuja kuhakikisha kweli umekufa au ni maneno ya watu.
All in all Rais wetu amefariki tumuombee huko aendako akapumzike salama
Nani kamwombea kifo? Kifo cha mtu hupangwa na Mungu tu. Hayo mengine ni majibu ya shombo tu.Hao adui zako watakuja kujipiga [emoji1702], hawa [emoji116] unafikiri ndio sampuli hiyo?
Na yeye kachelewa sioImeshaenda nbinguni na Yesu
Wapi nimempiga teke? Soma kwa kutulia.Yani hadi Nyerere umempiga teke!,kweli wewe mataga og.
Haha amani blaza ... Tz yetu sote... acha tuendelee na konyagi maana hata sielewi maongezi yanavyoendaNa yeye kachelewa sio
Ndio JF yetu tuliyo nayo sasa..hakuna namna ngoja twende nayo hivyo hivyoWengi wamepotoka sana! Aidha, wengi wanashindwa kuheshimu mawazo tofauti na kushambuliana badala ya kuchambua hoja mbadala. Tunaacha kujadili maudhui na muktadha wa hoja, tunamjadili au kumwelezea mtoa hoja
[emoji1545][emoji1545][emoji1545]Asante kwa mjadala mzuri nimejifunza mengi kwako ...BARIKIWA....!!!Usipate shida kushughulika na maneno hayo mawili,sababu moja halikai bila ya mwenzake. Ukweli ndiyo uhalisia wenyewe, ndiyo maana kwenye maana ya Ukweli unakuta ni kuafikiana na hali halisi, uhalisia huanza.
Baadaye sana ndio unge elewa!Haha amani blaza ... Tz yetu sote... acha tuendelee na konyagi maana hata sielewi maongezi yanavyoenda