Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

Tunautaabisha mwili kwa manufaa ya nani?

JF ya sasa uwezo wa kujadili hoja umepungua sana... Hoja hujibiwa kwa hoja..kinyume cha hapo ni mahoka
Kwasasa kwenye hoja nyingi kinzani, malumbano hutoka kwenye hoja na kuhamia kwenye vioja, vijembe na kejeli ama la kumjadili mtoa hoja....!!!
 
Ngoja tuwekane sawa katika jambo hili, na tuwe waadilifu.

Hapa nagusia nukta mbili au tatu na nukta ya mwisho itakuwa ni nasaha kwangu na kwenu.

1. Kiimani hasa kwetu sisi Waislamu jambo hili ni jambo baya na limekemewa vikali sana, na kiistilahi tunaita KUOMBOLEZA(Kuomboleza ni miongoni mwa mambo manne ya kijinga,ambayo hayataisha mpaka Kiyama kinasimama). Kiimani tunaamini ya kuwa Mtu ni wa aidha motoni au peponi,na akifa anatakiwa kuzikwa haraka ili akaanze kuishi maisha mapya kaburini, kama mtu wa kheri basi kaburi ni katika bustani miongoni mwa mabustani ya Peponi, na kaburi ni katika mashimo miongoni mwa mashimo ya motoni. Kwahiyo kitendo cha kumchelewesha maiti kumzika ni kuzidi kumpa dhiki na kumtesa kama ni wa motoni, na kama ni wa kheri basi mnamchelewesha kwenda kupata mazuri yake,kama alitoa usia mapema basi mzigo wa madhambi unakiwa ni juu yenu na si juu yake. Hitimisho ni kuwa,ni wajibu wetu na ni jambo jema kuwahisha kumzika maiti,tena huwa bora zaidi kutomsafirisha.

2. Wasia, ni jambo la dharura sana kwa mtu makini, tena ukiacha wasia mzuri juu ya maziko yako yaweje,huwa bora zaidi. Ila si kila wasia hufanyiwa kazi.

3. Hapa lazima tuelezane ukweli, mtoa mada nina hakika hali wa shani (Hii ni dhaa ya hakika kabisa, kwayo inahukumu hili sababu imevuka kiwango cja uzani wa asilimia Hamsini),umeandika uzi huu au haya kwa sababu ya chuki yako juu ya mwenda zake, lakini swali la msingi ni , Je angekuwa amekufa kipenzi chako tena katika wadhifa huo wa mwendazake ungeyaandika haya au na wewe ungekuwa katika kundi la hawa ambao wako dhidi yako na mlengo wako ambao wewe unawaita wapigaji ?

4. Hii ni nasaha ambayo kwayo,nimeigusia hapo awali ya kuwa baada ya kumaliza nukta mbili au tatu inayofata ni nasaha kwangu,kwako mtoa mada na kwa wale wasio kuwa mimi na wewe. Nasema hivi "Hutosha mtu kuwa MUONGO kusema au kuandika juu ua kila anachokiona au kukisikia". kiasili haya si maneno yangu.

Ziada : "Hajutii yule aliyekaa kimya kwenye fitina/fitna au kila wa kala."
umeandika uzi huu au haya kwa sababu ya chuki yako juu ya mwenda zake, lakini swali la msingi ni , Je angekuwa amekufa kipenzi chako tena katika wadhifa huo wa mwendazake ungeyaandika haya au na wewe ungekuwa katika kundi la hawa ambao wako dhidi yako na mlengo wako ambao wewe unawaita wapigaji ?[emoji848][emoji848][emoji848][emoji2827][emoji2827][emoji2827]
Ulikuwa na hoja nzuri lakini ikakatikia katikati na kupoteza mwelekeo baada ya kuacha hoja husika na kumjadili mtoa hoja kwa namna ulioona inakupendeza
 
Haina umuhimu upotezaji wa fedha za serikali na muda tu.
Usishangae baada ya haya tunayoandika hapa ratiba ikafupishwa ama kurefushwa tena.. Lakini most likely kufupishwa: kwa hali hizi za hewa tulizonazo kuuhangaisha mwili uharibikao kwenye maeneo tofauti kunataka kujipanga hasa mkikosea step moja tu mmetoa boko
 
kaka unamuonea WIVU MAREHEMU?[emoji53][emoji53][emoji53].
msije mkashangaa kusikia kwenye kaburi lake kuna harufu nzuri ya maua ya peponi.
 
Wewe ulishawahi kumuombea mtu akapona?..
Kifo ni ahadi na kimeshaandikwa.
Hakuna mtu anayeweza kumuombea mwenzie ASIFE mnaweza mkamuombea apone LAKINI SIO ASIFE.
kifo kipo Tu maana ni AHADI ambayo ni tayari umeweka na mungu wako hata kabla haujazaliwa.
Sasa namba zinabadilika. Tumetoka 1-3-5 odds red
Tunaingia even 2-4-6 BLACK.
gurudumu linazunguka.
Nyie na serikali yenu ndo mlitaka Afe kwa sbb mlificha ugonjwa wakati sisi watanzania tungemuombea
 
Kuna ratiba ndefu sana ya kuuaga mwili wa aliyekuwa rais wa Tanzania 2015-2021... Kwa ujumla wake ataagwa mara sita maeneo tofauti ya nchi ikiwemo Zanzibar iliyokuja kuchomekwa baadae kwa sababu za kisiasa
Msiba ni gharama kwa kila hatua na ni gharama zaidi kwa kila siku inayoongezeka kila siku ipitiyo bila kuzika...lakini zaidi kiimani ama kiroho si vema kuuhangaisha mwili uliokwisha tengana na roho labda tu iwe kwa maagizo ya mhusika
Safari ya kifo ni ndefu isiyo na kinyume ndio maana wafu hutolewa eneo alilofia, mochwari, nyumbani kisha kaburini... Ni safari ya njia moja... Ni kinyume cha mazoea kuutoa mwili mochwari na kuuanika siku nzima kisha kuurudisha mochwari tena na kuutoa tena na tena...

Watetezi wa hili wana hoja zao kama hizi
Dar kuaga ni mara mbili kutokana na wingi wa wakazi wake
Dodoma ni mji mkuu wa nchi alioupigania katika maisha yake hivyo si vizuri kuwaruka watu wa Dodoma
Mwanza ndio mkoa wa mji alikokulia
Geita na baadae Chato ndio nyumbani
Vipi kuhusu Zanzibar? Ni sehemu ya muungano , japo leo tayari kulikuwa na wawakilishi waliokuja kwa gharama za serikali
Kwa sasa ni matumizi , bajeti wanaijua wachache lakini huko mbeleni huu msiba unaweza kuja kuwa kashfa ya ufisadi
Kwa kila siku ya huu msiba kuna pesa inateketea
Per diem za viwango tofauti
Mafuta ya magari yanayohusika kwenye msiba
Malazi, chakula na vinywaji kwa waalikwa, wahudhuriaji, waombolezaji na wageni mbalimbali
Gharama za majukwaa mbalimbali, viti meza nk
Washereheshaji na watumbuizaji
Gharama za kuhifadhi mwili
Dharura nknk

Tunaweza kufanya mambo bila kujua mtazamo wake lakini isifike mahali tukakufuru kwa kuona kwamba hivi ndivyo inavyopaswa kuwa na zaidi kumbe kuna wapiga dili nyuma yake.

Hali ngumu ya maisha inawafanya baadhi kutumia misiba kama sehemu ya kujazia mashimo yao ya madeni, matumizi na mahitaji mbalimbali

Naweza kupigwa mawe kwenye hii post na wanufaikaji lakini huu... Wale wataosema msiba unabebwa na rambirambi za wapendwa wake. Na bajeti ya kitengo kwa nafasi yake kama mkuu wa nchi..lakini kuagwa mara sita sehemu tofauti za nchi kunaweza kuweka rekodi mpya.
Mbeya pia atakuja tumwage wala si shida maana yeye mwenyewe alijitoa sadaka kututumikia
 
Kitu nilicho notice sisi wa Tz Thinking capacity yetu ni ndogo kuliko punje ya haladali. Tunahis kuuzururisha mwili wa marehemu ndo kuonyesha kua tunampenda na kumjali hata tuki muaga mwaka mzima hakuna utofauti wowote tutakao ulete iwe kwa marehemu au kwa taifa zaid zaid ni gharama kuongezeka na maisha kuzi kuwa tight maana baada ya hilo zoezi bidhaa zinawez kupanda bei ili kufidia pesa iliyo tumika but who cares???
Ww ndo una thinking capacity ndogo, hili jambo lipo kiimani zaid. Imani ndo inaendesha maisha yako. Jiulize kuna jamii mtu akifa hazikwi had mtu flan either mtoto au mtu wa karib aje kumwona tu ndo azikwe. Hilo ndo naliona na kuna watu wangelalamika kuwa kwa nn hakupelekwa Zanzibar.
 
Usishangae baada ya haya tunayoandika hapa ratiba ikafupishwa ama kurefushwa tena.. Lakini most likely kufupishwa: kwa hali hizi za hewa tulizonazo kuuhangaisha mwili uharibikao kwenye maeneo tofauti kunataka kujipanga hasa mkikosea step moja tu mmetoa boko
Kuna sindano flan wakiipiga maiti ina kaa Mzee hata karibu mwezi mzima. Ndio waliopiga kwenye mwili wa hayati Daniel Arap Moi

Inamgandisha kabisa hata akifunuliwa hapo kwenye jeneza Mkuu, mwingine ni Princess Diana naye alipigwa hiyo.
 
Ulikuwa na hoja nzuri lakini ikakatikia katikati na kupoteza mwelekeo baada ya kuacha hoja husika na kumjadili mtoa hoja kwa namna ulioona inakupendeza
Maana yake ni kuwa nilichokiandika ni ukweli na huwezi kukipinga labda ujitoe ufahamu.

Watu makini na waadilifu huwa wakiambiwa ukweli, wanakiri kisha mengine yanaendelea.
 
kaka unamuonea WIVU MAREHEMU?[emoji53][emoji53][emoji53].
msije mkashangaa kusikia kwenye kaburi lake kuna harufu nzuri ya maua ya peponi.
Haya ndio majibu kwenye mjadala huu ambao swali hoja kwenye kichwa cha habari halijajibiwa
Iko hivi
Tanzania haijawahi kupata msiba wa kiongozi ngazi ya rais akiwa madarakani tangu uhuru, hivyo ukiachilia mwongozo wa katiba hakuna kingine tujuacho...kwahiyo kwa mara ya kwanza ile practice kwenye vfungu vya katiba ndio inafanyiwa kazi sasa

Hiki kitu kimetokea bila maandalizi ya kutosha(kawaida kifo hakina maandalizi) na hulka ya mwendazake aligeuza mfumo mzima kuufanya ni wake na ndio mwamuzi wa mwisho kwenye kila kitu.. Sasa hapa kuna mambo mengi sana ya kuyaweka sawa, kuna ya lazima na kuna ya muhimu lakini yote yanahitaji muda na muda uliopo hautoshi
Sasa hii ratiba ndefu ya kuaga mwili ni kwa maslahi ya nani? Jibu ni moja tuu... CCM...Ni wakati huu wananchi wakiwa busy na kuaga mwili kwa maelfu huko ndani nyuma ya pazia mambo yanaendelea tena kwa kasi kubwa lakini pia kwa umakini wa aina yake... Wana sacrifice kuuhangaisha mwili ili kudaivate attention ya jamii
CCM inajifahamu position iliyo nayo mbele ya macho ya jamii, IMESHAKATALIWA kitambo.. Uchaguzi huu kama sio wizi mkubwa wa kura ingekuwa Leo hii tunaongea mengine
Sasa ni muhimu sana kupanga timu za ushindi 2025.. Na wakati huo ni sasa, kipindi hiki cha maombolezo...ni katika hili ndio kila timu inajipanga kivyake na kufanya michakato kuwa migumu zaidi

Ni the race against time... Ni kwenye hii kundi lililokabidhiwa msiba linafanya yake pia.. Tutakuja kupeana mrejesho baadae
 
Mshana Jr ni kwamba unauonea huruma mwili wa mtu ambae ulionyesha kumchukia akiwa hai? Na inawezekana hujasononeshwa na kifo chake.

Tatizo ni kuuchosha mwili au gharama zinazotumika?
Tatizo ukiendekeza siasa na kama kichwa umewapa wana siasa na kubakia na kiwiliwili kila kitu utakichukulia kisiasa vitu ,mpaka sometimes wana twist vitu viendane na mitizamo yao ya kisiasa.

Lakini wanachofanya ktk msiba huu kwa mujibu wa imani ya RC si kosa,ila kwa kuwa siasa wanaziendekeza sometimes wanakuwa kama wendawazimu.

Manake mnasema tudiscuss kwa hoja haya.

Nakuuliza hili tukio limevunja katiba ya nchi?.

Limeenda kinyume na misingi ya Kanisa Katoliki? .

Sasa kwa nini ww uumie,kama humpendi sababu ya mitizamo yako ya kisiasa sawa,ila kaa ukijua kuna watu wanampenda wacha wamwage,wewe endelea kumchukia.Manake mnaleta siasa mpaka kwenye vifo.

RIP Magu.
 
Mshana Jr ni kwamba unauonea huruma mwili wa mtu ambae ulionyesha kumchukia akiwa hai? Na inawezekana hujasononeshwa na kifo chake.

Tatizo ni kuuchosha mwili au gharama zinazotumika?
Teh teh, eti mtu aliyeonyesha kumchukia katika uhai wake leo anahurumia mwili uliokwisha kufa...very strange!

Au anahurumia zile pesa wakuu watakazopiga katika zoezi zima.
 
Mshana Jr ni kwamba unauonea huruma mwili wa mtu ambae ulionyesha kumchukia akiwa hai? Na inawezekana hujasononeshwa na kifo chake.

Tatizo ni kuuchosha mwili au gharama zinazotumika?
Demi Nilikuona wazi kabisa hukufurahishwa na bandiko langu... Hata pamoja na hisia hizi kwamba nilimchukia marehemu ...lakini sasa hatumuongelei Magufuli tena, tunaongelea 'mwili wake' Mada yangu imejikita kwenye mwili uharibikao baada ya roho kuuacha
Nimefanya kazi mochwari mojawapo ya ethics za mochwari ni kuwatendea haki marehemu wote hata kama kati yao kuna adui yako mkubwa kwakuwa kilichopo pale si yeye tena bali ni jumba tupu liitwalo mwili
 
Kusema kweli hii kitu ni pointless kabisa. Uongozi uliobaki wamedhihirisha kuwa nao bado ni malimbukeni tu.

Haiwezekani kufanya mikusanyiko mikubwa namna hiyo bila kujali uhalisia wa janga la covid-19.

Watu tungeangalia shughuli kupitia kwenye TV na kusikiliza kwenye radio ingetosha. Hakukuwa na haja ya haya yote. Kwanza ni gharama kubwa tu zinatumika na zinaongeza mzigo kwenye kodi za wanaoitwa wanyonge.

Mimi kwangu haileti tofauti kuwa ameagwa na watu wengi au hajaagwa kabisa. Mtu akishakufa amekufa tu hata akiagwa na dunia nzima haimsaidii chochote.

Wangempumzisha tu tuendelee na maisha.

NB: In the end all the people you know (including you) will die.
We endelea na maisha hakuna aliekuzuia
 
Maana yake ni kuwa nilichokiandika ni ukweli na huwezi kukipinga labda ujitoe ufahamu.

Watu makini na waadilifu huwa wakiambiwa ukweli, wanakiri kisha mengine yanaendelea.
Hapana Jurjani usione ukweli wako kwa mtazamo wako ni ukweli wangu.. Mimi ni mwadilifu na huwa nikikengeuka nakubali kurelebishwa kwakuwa si mkamilifu na huwa naomba na radhi pia
Jurjani note hii kitu inaitwa ukweli usiegemee sana kwake kwakuwa ukweli hubadilika kulingana na mazingira, imani, hulka na mitazamo... Egema kwenye uhalisia...Napenda uhalisia kwakuwa hauna rangi nyingi hivyo haubadiliki wala haubadilishwi
 
Back
Top Bottom