Mpanda,Katavi kuna dhahabu za kutosha na pesa ipo but wamejaa wachina kote huko hata kupata vibali vya kuchimba kama Mzawa ni ngumu..
Wamejenga na Airport yao kabisa,wanasafirisha tani za kutosha za Gold..
SAMIA WHAT IS THIS
Britanicca
Wewe unatuongezea tu msongo wa akili; kana kwamba yaliyopo hayatoshi kuumiza roho za watu.
Sasa tueleze basi tuelewe unasema nini na ushahidi ulionao wewe; hata wa kimazingira tu.
Ni nani asiyejuwa wizi wa waChina, lakini sasa si wizi tena, ni kama wanazoa tu mali isiyokuwa na mwenyewe!
Tumeharibikiwa sana, lakini hasa sijui kwa nini wananchi nasi ni kama tumegandishwa akili kabisa ili tusistuke!
Kelele zote zile alizopiga Magufuli kuhusu mali zetu, hakuna hata moja iliyotuingia kichwani?
Na kwa wale wazee je, mafunzo yote ya Mwalimu Nyerere kuhusu raslimali za taifa hili, hata wao hawakumbuki kabisa lolote?
Tumebaki na akina Stphen Wassira na akina Kibudu Kalamaganda, wakiwa mstari wa mbele kunadi mali za waTanzania, kana kwamba hawakuwepo kabisa wakati wa mafunzo?
Sasa tufanyeje, nani ataliokoa taifa hili!