Tuliwazuia kufanya Kongamano, wameamua kuelekea kwenye nyumba za ibada ambayo ni haki ya kikatiba pia

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Kwenda kanisani kufanya Ibada Ni haki ya kikataba ndani ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania. Wanaotaka katiba wamenyimwa kufanya makongamano, bila kuathiri Hali ya usalama wameamua siku ya ibada wavae t-shirt zao za kutaka katiba mpya. Naamu waumini wameamua kufanya t-shirt za katiba mpya kuwa nguo ya kuendea sokoni na kanisani.

Je, dola itazuia haki ya kuabudu? Itatunga sheria kwamba kuvaa tshirt ya katiba mpya ni dhambi? Sidhan Kama dola itqvunja katiba kwa kusukumwa na mavazi, tutaelewana tu kwamba tatizo siyo t-shirt, tatizo siyo mabango na Wala tatizo siyo Mbowe. Tatizo nikukosekana kwa haki.

Tunapoelekea tshirt nyekundu ya katiba mpya itakuwa Ni vazi la Taifa maana naona hata CCM wananunua nakwenda nalo kwenye TV.

Tukutane ibadani, Gwajima akipiga mwingi huko Ubungo sisi tupige mwingi kwenye nyumba zetu za ibada. Wachungaji na wasimamizi wa kanisa sidhani Kama watatii dola wakaacha kumtii Mungu aliesema njooni kwangu nyote msumbukao na kulemewa na dhambi maana ntawapumzisha.

Naamini kuwa na wataka katiba wanaokwenda kwenye nyumba za ibada ni Bora kuliko kuwa na wataka katiba wanaokwenda msituni. Kushuhudia waumini wakitaka mabadiliko ni Bora kuliko kushuhudia makundi ya uasi yakitaka mabadiliko. Tujivunie aina hii ya wanadamu kwenye ardhi yetu.
 
Nimeipenda hii, wameibukia kanisani. T-shirt za katiba zimeadimika mjini watu wanavyozisaka kuzinunua. Yaani maisha ya mwanadamu ni kujinyambulisha.

Hongereni mliojiongeza bila kuvuruga amani wala kuvunja Katiba.

Haki ya kuabudu ipo wazi na t-shirt hazina nembo za chama zina Hitaji la Katiba so hata makanisa kuzuia watu kuzivaa awqtakuwa na hoja.
 
Kwenda kanisani kufanya Ibada Ni haki ya kikataba ndani ya Jamuhuri ya Muungano ya Tanzania. Wanaotaka katiba wamenyimwa kufanya makongamano, bila kuathiri Hali ya usalama wameamua siku ya ibada wavae t-shirt zao za kutaka katiba mpya. Naamu waumini wameamua kufanya t-shirt za katiba mpya kuwa nguo ya kuendea sokoni na kanisani.

Je, dola itazuia haki ya kuabudu? Itatunga sheria kwamba kuvaa tshirt ya katiba mpya ni dhambi? Sidhan Kama dola itqvunja katiba kwa kusukumwa na mavazi, tutaelewana tu kwamba tatizo siyo t-shirt, tatizo siyo mabango na Wala tatizo siyo Mbowe. Tatizo nikukosekana kwa haki.

Tunapoelekea tshirt nyekundu ya katiba mpya itakuwa Ni vazi la Taifa maana naona hata CCM wananunua nakwenda nalo kwenye TV.

Tukutane ibadani, Gwajima akipiga mwingi huko Ubungo sisi tupige mwingi kwenye nyumba zetu za ibada. Wachungaji na wasimamizi wa kanisa sidhani Kama watatii dola wakaacha kumtii Mungu aliesema njooni kwangu nyote msumbukao na kulemewa na dhambi maana ntawapumzisha.

Naamini kuwa na wataka katiba wanaokwenda kwenye nyumba za ibada ni Bora kuliko kuwa na wataka katiba wanaokwenda msituni. Kushuhudia waumini wakitaka mabadiliko ni Bora kuliko kushuhudia makundi ya uasi yakitaka mabadiliko. Tujivunie aina hii ya wanadamu kwenye ardhi yetu.
Kilichofanyika ktk kanisa la KKKT Makongoro Mwanza hapo jana si kitendo cha kiungwana, kanisa si ofisi ya vyama vya siasa, kanisa ni nyumba takatifu kwa ajili ya maombi, tukio la jana limewakwaza waumini wengi maana kila mtu anayo itikadi yake ya chama tofauti. Naiomba Serikali isifumbue macho jambo hili, ni hatari kwa afya ya taifa. Na kama itaachwa hivi basi tuwe tunatangaziwa jumapili hii Chadema watasali kanisa fulani ili tuwaachie wakafanye mambo yao ya siasa mshenzi sisi tutafute maeneo mengine ya kusali
 
Back
Top Bottom