Mie bhana nakumbuka ilikuwa 2003 nipo Darasa la Tano Kunduchi Dar.
Kisa kenyewe ilikuwa ni ugomvi baina yangu mm na mwanafunzi mwenzangu wa darasa la saba.
Sijui ni utoto au nini tukapanga tupigane baada ya muda wa masomo kuisha. Mie nilikuwa na kundi kubwa la wapambe asikwambie mtu ukiwa na wapambe unajiamini balaaa.
Mwenzangu yupo peke ake baada ya muda wa masomo kuisha tukaruhusiwa, Wana wakanipanga twende zetu na yule mpinzani wangu akatafutwa tukatokomea porini uko.
Nikavua Begi wapambe wakanishikia jamaa akasogea ngumi zikaanza Daah mie nina bonge la nyomi la wapambe Piga huyo!! Mng'oe Meno huyo!!
Bichwa likavimba Mbwembwe nyingi ,Basi mara Ngumi Mara Teke, Kwepa Tena Kwepa Nikampatia Moja Saafi ya Mdomo Akachanika Kidogo Damu Ikaanza Kutoka.
Daah kumbe ndo nimemjeruhi simba, Nilikula mbata za kutosha hadi nikaona kizunguzungu nikazirai.
Wana wote wakakimbia nililala pale sijitambui kwa nusu saa. Bahati kuna mzee alikuwa anapita akaniona nimelala uso umevimba Shati limechanika Daah
Ndo akanibeba kunipeleka shule uku sijitambui kuwaelezea walimu nikamwagiwa maji sijui ndo kunipeleka hospital Wakaitwa wazazi.
Daah Kesi ilikuwa kubwa mno, Wazazi wote wakaitwa.Nashukuru Mungu yaliisha ila nimekoma Kupewa Sifa za Kijinga Inaponza Watu.