Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

NILIOKOLEWA NA JIRANI NA WAZUNGU

Mimi ilikua siku nikiachwa mwenyewe nyumbn basi hio ndio siku ya kujaribu mengne yote ambayo nakatazwaga,
Siku moja hv wakubwa wote wakaenda shamba kuvuna mahindi nikaachwa mwenyewe, wakati wanaondoka Mama akaniambia "Leo usipotulia litakalo kupata utajisaidia mwenyewe maana kambini watu karbu wote leo wanaenda shamban kuvuna mahindi" (tulikua tunaish kwenye kambi za maliasili na utalii na ipo isolated na vijiji vingne) mtoto wa mamkubwa akacheka akasema "leo sijui tutakuta kituko gani?" maana wiki iliyopita nilikutwa nimelala kwenye maua baada ya kupanda juu ya bati na kujitia fundi wa antena nikashuka nayo, nilipo angukia ndo hapo hapo nilipokutwa nimejikunyata, wapita njia walikua wananiona ila hawakujua kama nimepattwa na tatzo maana hapo hapo mbuzi wakaja kujilaza kwa kunizunguka, jiran baada ya kuona mbuzi wameondoka wamekuja kuku mimi bado nipo ndo akapigwa na machale akaja kunibeba akanipeleka dispensary,

sasa basi, baada ya bimkubwa kunipa onyo wakasepa, nikanywa kwanza chai, wakati anaongea vile nilikua nasubr tu amalize lakn kichwan nishapanga leo lazima nijifunze baiskeri,
Nikaenda stoo nikachomoa mphoenix nikakokota mpk barabarani, mimi raha yangu nikokote mpk kwenye mteremko/kilele cha mlima halaf nipande inishushe then nikokote tena nirudie, nikaenda mara ya kwanza safi tu, mara ya pili niliumia matakoni baada ya kujibamiza kwenye ule mtalimbo unaounganisha sterring na kiti maana nilikua sikai kwenye kiti ili nifikie sterring na pedal vizuri(tulikua tunaita kuisimamia), Mara ya tatu ndo kimbembe sasa,
Kwa sbb nilishajihs kuweza mzee nikashuka kwa kasi huku nimekaa kwenye kiti, kitu kikaanza kuyumba, speed ikaongezeka zaid, break nikashndwa kushika maana siwez kutanua vidole nizifikie na nikilazimisha napoteza balance maana huku nyuma nako kiti nimekikalia pale kwenye ncha(pale wanaposema panawatoaga wanawake waendesha baisker bikra) huku nimeinamia sterring, ule mlima n mrefuu mpk ufke chini, chini ikawa inapanda gari ya watalii wanaenda kule kambini kuchukua kibali ofisini ili waingie porini huku wanachukua video, wakaniona nashuka kwa kasi sanaa ikabd wao ndo wanikwepe, sasa pale mwisho wa mlima pana kona kali, karavat, bwawa/mto na chaka la miba, kona nilijua niwazi kbsa sitaweza kukata, nikawaza kule mtoni kuna mawe na maporomoko=kifo, kwenye karavat pale nikijarb tu n kifo, maana ni kubwa na maji n meng, option ikabakia kwenye chaka la miba(miba flan hv mifupi imejikunja halaf inawasha sana ikikuchoma),
Nikalifakamia bwanaaaaa, niliingia mpk kati kati ya lile biwi kubwa la miba, huko ndani kulikua na vicheche, bundi, wanyama flani hv wananuka sana na wale wanaopenda kujisaidia sehem moja hata wakienda mbali watarud pale n.k wote walitoka nduki kila yule kwa mlio wake, nilibananishwa na miba ukijitikisa tu kdg inakuchoma,kumbe wale wazungu walipigwa na machale, walipaki gari wakarud kuniangalia, wakanikuta nimejaa damu, mmoja akaenda kwenye gari kuchukua vifaa wakatumia zaid ya masaa mawili kunitoa mule ndani ya lile biwi la miba bila kuniumiza zaidi, wakanipa huduma ya kwanza(walikua na vifaatiba ving), wakanipeleka ofisini, huko tukamkuta mzee na wafanyakaz wenzake, nimejaa ma bandage ofce nzima wakaanza kuitana "jaman njooni mmuone ..... Huku" baada ya kusununika watu hoi kwa vicheko, hapo naonekana tu kijimdomo na macho, wale wazungu wakawa marafk zangu kuanzia pale mpk wanaondoka, wakaniachia bonge ya Nokia na PC, niliwashwa siku tatu, kuanzia pale ikawa kuachwa nyumbn mwenyewe n mwiko.
Nimecheka sana
 
Bwana Yesu asifiwe kwa wale wenzangu na mimi. Wengine habari zenu?

Ninapoelekea kutimiza miongo kadhaa ya kuwepo hapa duniani nimejikuta natafakari maisha yangu tangu pale nilipoanza kupata akili hadi leo hii nimejikuta natabasamu na kumshukuru sana Mungu maana nimekutana na mengi mazuri, mabaya, ya kukatisha tamaa ila katika yeye anitiaye nguvu nimeyaweza yote na nitaendelea kuyaweza yote.

Nimejikuta nakumbuka tukio moja la huko nyuma nikiwa na miaka sita hivi au saba (sikumbuki exactly ilikuwa mwaka gani). Mimi bwana nilikuwa naishi na sister tangu nikiwa mdogo sana na mpaka leo ukisikia nasema naenda nyumbani maana yake naenda kwa sister (naonekana kituko si eti eeh?)..tuachane na hayo kwanza.

My sister miaka hiyo alikuwaga mwalimu vijiji vya ndani kabisa huko, akiwa anaenda kuchukua mshahara anatumia siku tatu..siku ya kwanza kwenda, siku ya pili anaitumia kuchukua mshahara na kufanya mambo yake na hakukuwa ATM miaka hiyo kwa hiyo unaweza kupata picha na siku ya tatu anaitumia kurudi na wakati mwingine alikuwa anaweza kutumia hata siku nne.

Siku hiyo kabla hajasafiri alinunua kumbikumbi (wenyeji wa mikoa ya nyanda za juu kusini mtakuwa mnazijua, nilikuwa nazipenda sana) basi nilizifakamia zile ndude kama ugomvi, nilizikula kama lita moja hivi. Asubuhi ameamka zake hana hili wala lile akaondoka, mimi mida ya saa moja asubuhi nikaanza kuendesha, baadae nikaanza kutapika matapishi ya njano (mnaitaga nyongo sijui).

Kwa hiyo ikawa ni mwendo wa kuharisha na kutapika, sijui dawa yoyote na hata akili ya kwamba niende kwa jirani nikamwambie hali yangu nikawa sina sijui ndio utoto? Inafika mida ya saa nne mtoto nimechoka nikalala kwenye mkeka nje siwezi tena kusimama nikawa natapika hapohapo sina hata nguvu ya kusimama tena yaani nikawa nikifumbua macho hivi naona kila kilichopo mbele yangu kinazunguka. Ni miaka mingi imepita lakini picha ya siku ile haijawahi kunitoka.

Bahati nzuri akaja rafiki yake sister alikuwa hajui kama kasafiri ndio kunikuta katika hali hiyo akanibeba kunipeleka kwake maana kile kijiji hakikuwa hata na dispensary hadi kijiji cha jirani ... yule dada alikuwa anaitwa Fausta (RIP). Ndio ikawa pona yangu na sister alirudi baada ya siku tatu. Huwa najaribu kutafakari hivi asingekuwa yule dada kuja pale sister angenikuta niko hai kweli?

Tangu siku hiyo hakuwahi kuniacha peke yangu akisafiri maana siku zote nilikuwa najifanya konki siogopi kulala peke yangu. Tena wale wadudu niliwachukia jumla jumla sijawahi kuwala tenaa.

Kama na wewe mdau ulishawahi kupitia ugonjwa au hali yoyote ukaona kifo hiki hapa karibu tushee
very sorry babe
 
Umenikumbusha nikiwa mtoto bwana nililia kumbikumbi acha zidakwe nikaangiwe Nile, acha nianze kutapika had nikaishiwa nguvu kabisa, tangu siku hyo sipendi kumbi kumbi, kisa kingine nilikuwaga mtundu niliye kubuhu acha nitumbukie kisimani nikiwa mtoto sijui hili wala lile nikaja kuokolewa na wenzangu. Aisee kikubwa mimi nimepitia mengi na kunusurika kifo mara nyingi sana. Namshukuru Mungu dunia hii siji kuondoka had niwe mbibi na mkongojo
Same to me. ...
 
@demi kafanyaje tena!!

Nalijua, kimbo, tanbond, nk ni makopo tulitumia sana zamani rafiki.

Swali langu ni lita moja ya kumbikumbi? Unakunywa maji kilo moja... hahahaha!!!
Sasa lile kopo la lita moja huwa tunatumia kupima vitu kama hivyo,maharage, mahindi, n.k kwa hiyo vipimo vinaenda hivyo hata mashine ukienda huku utaona bei zimewekwa kwa mfumo wa kg ila kule kwetu zinawekwa kwa mfumo wa lita. Demi alishangaa kwamba kumbikumbi wanapimwaje kwenye lita
 
Sasa lile kopo la lita moja huwa tunatumia kupima vitu kama hivyo,maharage, mahindi, n.k kwa hiyo vipimo vinaenda hivyo hata mashine ukienda huku utaona bei zimewekwa kwa mfumo wa kg ila kule kwetu zinawekwa kwa mfumo wa lita. Demi alishangaa kwamba kumbikumbi wanapimwaje kwenye lita
Ulitakiwa unieleweshe hivyo siku ya Kwanza ningekuelewa.
 
Sasa lile kopo la lita moja huwa tunatumia kupima vitu kama hivyo,maharage, mahindi, n.k kwa hiyo vipimo vinaenda hivyo hata mashine ukienda huku utaona bei zimewekwa kwa mfumo wa kg ila kule kwetu zinawekwa kwa mfumo wa lita. Demi alishangaa kwamba kumbikumbi wanapimwaje kwenye lita
Sijui kwenu, ila kwetu tunasema ni "kopo" au "debe" na sio lita. Actually huwa watu wanadhani kopo moja ni sawa na kilo moja kwa vitu vingi, which is wrong.

Kuhusu bei, tunaandikiwa kopo ni shs. 200 na sio lita, huwezi kusema lita ya mahindi..

Sorry, labda nyie mna terminologies tofauti.
 
Sijui kwenu, ila kwetu tunasema ni "kopo" au "debe" na sio lita. Actually huwa watu wanadhani kopo moja ni sawa na kilo moja kwa vitu vingi, which is wrong.

Kuhusu bei, tunaandikiwa kopo ni shs. 200 na sio lita, huwezi kusema lita ya mahindi..

Sorry, labda nyie mna terminologies tofauti.
Asante kwa kunisaidia maana nilishambuliwa hatari. Ila Sasa nimemuelewa
 
Nakumbuka henzi za utoto nilikua mtundu balaa,kuna siku tulienda porin kusanya kuni tumefika mm nikawambia wenzangu kuni zilizodondoka chini sishiki nataka zilizopo juu ya miti tu(matawi yaliokauka)


Baada ya kupanda miti kadhaa nikakutana na miti miwili mirefu balaa imeachana kama mita2 iv alafu yote juu ina matawi makavu ila yapo mbali,sikujali hlo mm nikapanda mti wa kwanza nikakata yale matawi...sasa ili nikate ya mti wa pili lazima nishuke nikaanze upya kupanada..

Kucheki chini ni mbali mpaka nishuke nikapande tena sio leo,si nikaona bora nijirushe kama nyani nirukie kwenye mti wa pili..nikaweka panga vizuri na nikatarget tawi la kudaka upande wa pili..si nikajirusha nikashindwa kulifikia lile tawi..kilichofuata nikuporomoka kwenda chini huku nikijibamiza kwenye matawi ya chini..

Nilivyotua nilikaa pale chini kama dakk1 siwezi kujigusa wala kutoa sauti alafu wenzangu wapo machakani hawajui kinachoendelea..baada ya mda sauti ikarudi nikapiga bonge la yowe wenzangu wakaja..
Kuja kuninyanyua mguu umetenguka ilibidi nibebwe mpaka nyumban nimefika nikapokelewa na kichapo ndio uduma zingine zikaendelea.
 
Nynigine Kuna Siku tukatoroka shulen kwenda mtoni kuogelea huo mto kuna sehemu umetengeneza kama bawa ivi na kuna maporomoko tumefika wenzangu wanajitupa kwenye maji mimi kuogelea sijui..

Kila navyo angalia jamaa wanavyoenjoy ndivyo na mm nazidi kutaman kuingia majini si nikatupa nguo kule nikajitosa ila kwa kuibia ibia kwenye maji mafupi..kidogo si nikajitosa kwenye kina kirefu acha ninywe maji nimekuja kutoka huko tumbo limejaa maji kama chura maana mm nilijizamisha bila kujua kuna kubana pumzi.
 
Sijui kwenu, ila kwetu tunasema ni "kopo" au "debe" na sio lita. Actually huwa watu wanadhani kopo moja ni sawa na kilo moja kwa vitu vingi, which is wrong.

Kuhusu bei, tunaandikiwa kopo ni shs. 200 na sio lita, huwezi kusema lita ya mahindi..

Sorry, labda nyie mna terminologies tofauti.
Ni kweli tuko tofauti sisi huwa tunaita hivyo hivyo lita
 
Back
Top Bottom