Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

DEPRESSION NA STRESS...aisee kuna siku niliamini wanaojiua sio wajinga.. pia kukaa na kitu moyoni ni hatari sana unaweza chukua maamuzi mabaya kumbe ungeweza kupata solution..!! OMBA USHAURI...ONGEA inasaidia sana.
Mkuu tusimulie kidogo basi
 
Nakumbuka henzi za utoto nilikua mtundu balaa,kuna siku tulienda porin kusanya kuni tumefika mm nikawambia wenzangu kuni zilizodondoka chini sishiki nataka zilizopo juu ya miti tu(matawi yaliokauka)


Baada ya kupanda miti kadhaa nikakutana na miti miwili mirefu balaa imeachana kama mita2 iv alafu yote juu ina matawi makavu ila yapo mbali,sikujali hlo mm nikapanda mti wa kwanza nikakata yale matawi...sasa ili nikate ya mti wa pili lazima nishuke nikaanze upya kupanada..

Kucheki chini ni mbali mpaka nishuke nikapande tena sio leo,si nikaona bora nijirushe kama nyani nirukie kwenye mti wa pili..nikaweka panga vizuri na nikatarget tawi la kudaka upande wa pili..si nikajirusha nikashindwa kulifikia lile tawi..kilichofuata nikuporomoka kwenda chini huku nikijibamiza kwenye matawi ya chini..

Nilivyotua nilikaa pale chini kama dakk1 siwezi kujigusa wala kutoa sauti alafu wenzangu wapo machakani hawajui kinachoendelea..baada ya mda sauti ikarudi nikapiga bonge la yowe wenzangu wakaja..
Kuja kuninyanyua mguu umetenguka ilibidi nibebwe mpaka nyumban nimefika nikapokelewa na kichapo ndio uduma zingine zikaendelea.
Hahaha African parents bwana daah yaani mtoto ameumia ye anashusha kichapo ndio maana zamani tulikuwaga tunaficha vidonda anakuja kushtuka baadae kidonda kina hali mbaya kwa sababu ya mambo yao ya kupenda kuchapachapa
 
Nynigine Kuna Siku tukatoroka shulen kwenda mtoni kuogelea huo mto kuna sehemu umetengeneza kama bawa ivi na kuna maporomoko tumefika wenzangu wanajitupa kwenye maji mimi kuogelea sijui..

Kila navyo angalia jamaa wanavyoenjoy ndivyo na mm nazidi kutaman kuingia majini si nikatupa nguo kule nikajitosa ila kwa kuibia ibia kwenye maji mafupi..kidogo si nikajitosa kwenye kina kirefu acha ninywe maji nimekuja kutoka huko tumbo limejaa maji kama chura maana mm nilijizamisha bila kujua kuna kubana pumzi.
Duuh pole mkuu
 
Mkuu tusimulie kidogo basi
Acha tu mkuu...niliona mwisho wangu umefika kabisaa! Enzi hizo nipo chuo kuna ishu ilitokea ilibdi nidisco kabisa aiseee...ilee siku niliwazaa mpaka daah..! Acha tu mkuu story ndefu kwa hali iliyokuwepo death niliona ndo only option sema nashukuru Mungu kuna mtu mzima flani aisee alinisaidia sana...
 
Bwana bwanaaaaa

Ilikuwa 2014 mbeya,msimu wakulima wanavuna maharagwe,basi mimi na mwanangu alikuwaga na gari aina ya pikup tukawa tunapiga dili za kuwasomba wamama waliotoka vunatoka shamba huko maeneo ya inyala imezu n.k tunawapeleka uyole

Siku hiyo mishale kama ya saa nne usiku tutakwafumania bhana wako kama saba hivi na magunia yao ya maharagwe,tukaingiwa tamaa ya kuwabeba wote na wao wakakubali lakini sasa gari haitoshi...ikabidi mimi ninitoe muhanga kupanda nyuma kule juu kabisaaaa ya magunia ya maharagwe....sasa tukatoka imhezu freshi tu.

Ule mzigo ulikuwa unayumba lakini muuni kibishi nikawa nakomaa tu tunaenda kitata.

Mwanzoni jamaa alikuwa anaendesha kistaarabu akijua juu kuna mtu,alivyoona silalamika akaanza kunogewa,kufika eneo la kilimo pale jamaa akakanyaga moto bhanaaaa,mara pappp mbele gari iko site yetu...ikawa anaenda kuivaa waziwazi akafanya manuva kuichengesha kuikwepa....bwana wweeee mimi huku juu naona kifo hiki hapa na nishajikojolea kwa hofu.

Kushtuka niko chini bahati nzuri sana niliangulia juu ya magunia ya maharagwe na tukafanikiwa kupishana lakini mimi niko chini.

Kusema ukweli ile siku nilitoa haja kubwa
 
Bwana bwanaaaaa

Ilikuwa 2014 mbeya,msimu wakulima wanavuna maharagwe,basi mimi na mwanangu alikuwaga na gari aina ya pikup tukawa tunapiga dili za kuwasomba wamama waliotoka vunatoka shamba huko maeneo ya inyala imezu n.k tunawapeleka uyole

Siku hiyo mishale kama ya saa nne usiku tutakwafumania bhana wako kama saba hivi na magunia yao ya maharagwe,tukaingiwa tamaa ya kuwabeba wote na wao wakakubali lakini sasa gari haitoshi...ikabidi mimi ninitoe muhanga kupanda nyuma kule juu kabisaaaa ya magunia ya maharagwe....sasa tukatoka imhezu freshi tu.

Ule mzigo ulikuwa unayumba lakini muuni kibishi nikawa nakomaa tu tunaenda kitata.

Mwanzoni jamaa alikuwa anaendesha kistaarabu akijua juu kuna mtu,alivyoona silalamika akaanza kunogewa,kufika eneo la kilimo pale jamaa akakanyaga moto bhanaaaa,mara pappp mbele gari iko site yetu...ikawa anaenda kuivaa waziwazi akafanya manuva kuichengesha kuikwepa....bwana wweeee mimi huku juu naona kifo hiki hapa na nishajikojolea kwa hofu.

Kushtuka niko chini bahati nzuri sana niliangulia juu ya magunia ya maharagwe na tukafanikiwa kupishana lakini mimi niko chini.

Kusema ukweli ile siku nilitoa haja kubwa
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sitasahau siku nilipopoteza fahamu kwa sababu ya pressure. Nilianzaa mazoezi kama mwendawazimu mpaka nikapungua uzito.
Haha pole mkuu ikabidi uanze kupungua kwa lazima maana ukaona kaburi linakuita
 
Acha tu mkuu...niliona mwisho wangu umefika kabisaa! Enzi hizo nipo chuo kuna ishu ilitokea ilibdi nidisco kabisa aiseee...ilee siku niliwazaa mpaka daah..! Acha tu mkuu story ndefu kwa hali iliyokuwepo death niliona ndo only option sema nashukuru Mungu kuna mtu mzima flani aisee alinisaidia sana...
Pole sana boss
 
Bwana bwanaaaaa

Ilikuwa 2014 mbeya,msimu wakulima wanavuna maharagwe,basi mimi na mwanangu alikuwaga na gari aina ya pikup tukawa tunapiga dili za kuwasomba wamama waliotoka vunatoka shamba huko maeneo ya inyala imezu n.k tunawapeleka uyole

Siku hiyo mishale kama ya saa nne usiku tutakwafumania bhana wako kama saba hivi na magunia yao ya maharagwe,tukaingiwa tamaa ya kuwabeba wote na wao wakakubali lakini sasa gari haitoshi...ikabidi mimi ninitoe muhanga kupanda nyuma kule juu kabisaaaa ya magunia ya maharagwe....sasa tukatoka imhezu freshi tu.

Ule mzigo ulikuwa unayumba lakini muuni kibishi nikawa nakomaa tu tunaenda kitata.

Mwanzoni jamaa alikuwa anaendesha kistaarabu akijua juu kuna mtu,alivyoona silalamika akaanza kunogewa,kufika eneo la kilimo pale jamaa akakanyaga moto bhanaaaa,mara pappp mbele gari iko site yetu...ikawa anaenda kuivaa waziwazi akafanya manuva kuichengesha kuikwepa....bwana wweeee mimi huku juu naona kifo hiki hapa na nishajikojolea kwa hofu.

Kushtuka niko chini bahati nzuri sana niliangulia juu ya magunia ya maharagwe na tukafanikiwa kupishana lakini mimi niko chini.

Kusema ukweli ile siku nilitoa haja kubwa
Duuh pole sana
 
Mimi na pikipiki tu😀😀😀

1. Kuna siku nilikuwa nachota maji kwa pikipiki, sasa kuna mshkaji wangu akaja nyumbani akanikuta ndo nafunga ndoo za maji kwenye pikipiki ili niende kisimani. Kumbe mshkaji alikuwa anataka kuendesha pikipiki sema akawa anamgwaya mshua, sasa tulipo toka nyumbani tukiwa njiani jamaa akaanza kuomba nimpe naye aendeshe, ila nikawa nakataa kwa kuwa nilikuwa namjua jamaa ni mpenda sifa sana na kwa kuwa njia ilikuwa inapita hadi mtaani nilijua wazi angetaka kuonyesha kuwa yeye ni mtabe wa kukimbiza na usalama wetu ungekuwa mdogo. Ila akazidi kunisumbua nikaona isiwe tabu nikamwachia ila nikamsisitizia awe makini.
Bwana bwana, jamaa akapanda mimi nikapanda nyuma, akang'oa chuma. Nikawa naona jamaa anapandisha gia tu kila baada ya mita chache. Ndani ya dakika chache jamaa akawa ameshaikamata gia namba 5 huku spidi ikiwa ni kali sana. Mimi nikaanza kutoka na kijasho nimsihi jamaa apunguze mwendo lakini wapi.
Sasa tukafika sehemu kuna kona kali sana, na ukinyooka kwa mbele bila kukata hiyo kona kuna ka bonde halafu unakutana na reli iliyoinuliwa na kokoto. Sasa jamaa alivyoona kuwa hawezi kupiga kona ikabidi anyooke. Kwanza pikipiki iliruka na tukapita katikati ya miti ya vichaka vichaka, ilipokwenda kutua jamaa bado alikuwa na wenge akazidi kuvuta mafuta, nikaona tunaanza kupanda mlima wa kokoto za relini ikabidi niruke na kamaa akaenda kumamia juu ya makokoto. Cha kushukuru hatukuumia sana, ila pikipiki ilikuwa nyang'anyang'a.

2. Mimi na mshua tulikuwa tunatoka kwa bibi kuwasalimia, tukawa tunarudi nyumbani kila mmoja anaendesha pikipiki yake tukiwa tunapita kwa ile barabara ya dom-singida. Sasa mshua akawa anaendesha slow, nikaambua kumuacha mimi nikatangulia. Sasa likaja semi kwa nyuma likanipita nikasema wewe sikuachi, nikaanza kulifukuzia kwa nyuma ili nami nilipite. Tukaenda wee, baadayr nikasema sasa huu ndo muda wa kuovatake na nikaamua kuovateke kwa kushoto. Bwana wee, ile nakaribia kulipita nikaanza kuona semi linakuja kuande wangu kwa kasi, sijui ndo dereva alikuwa ananifanyia kusudi. Ikabidi nitoke barabarani nikaingia machakani huku nikijitahidi nisidondoke maana nilikuwa kasi sana. Kwa hofu iliyonikumba nikawana naendesha huku nalia kwa kupiga mayowe. Nikaenda kusimama kwa mbele kabisa nikiwa nimechubukachubuka. Niliwatukana sana wale jamaa.
3. Nikiwa na pikipiki yangu ile ile nikiwa nimetoka misele narudi nyumbani nikakuta mto umejaa maji japo hayakuwa mengi sana kiasi cha kutisha, nikasema hapa ntapita tu.
Mzee baba nikajitosa, kufika katikati ya mto ngoma ikazima. Ilipozima maji yakaingia kwenye dude la kutolea moshi, kwa hiyo hapo pikipiki kuwaka tena ni mtihani. Nikiwa sijui nifanyeje nikaona naanza nasombwa mimi na pikipiki yangu. Ikabidi nitoke nikaicha pikipiki ikaanza kubebwa baadaye nikawaza nikiiacha inaweza kwenda mbali na ikaharibika, ikabidi nijitose mtoni ili niitoe. Maji yaone kwenye glasi tu, shughuli iliyonipata pale mtoni nilianza kuwaona akina eskarioti na washkaji zake.
 
Mimi nilihitaji ufafanuzi nikashushuliwa.
Itakuwa muanzisha uzi ni mtu wa iringa...nilienda kutembea huko mwaka huu nikashangaa kichombo/kipimio kikiitwa Lita, wanakitumia kupima vitu vya uzito kama njegere, maharagwe...ukitumia akili ya shule unaweza usielewe maana mambo ya lita ni kwenye vi/kimiminiko tu
 
Mimi na pikipiki tu[emoji3][emoji3][emoji3]

1. Kuna siku nilikuwa nachota maji kwa pikipiki, sasa kuna mshkaji wangu akaja nyumbani akanikuta ndo nafunga ndoo za maji kwenye pikipiki ili niende kisimani. Kumbe mshkaji alikuwa anataka kuendesha pikipiki sema akawa anamgwaya mshua, sasa tulipo toka nyumbani tukiwa njiani jamaa akaanza kuomba nimpe naye aendeshe, ila nikawa nakataa kwa kuwa nilikuwa namjua jamaa ni mpenda sifa sana na kwa kuwa njia ilikuwa inapita hadi mtaani nilijua wazi angetaka kuonyesha kuwa yeye ni mtabe wa kukimbiza na usalama wetu ungekuwa mdogo. Ila akazidi kunisumbua nikaona isiwe tabu nikamwachia ila nikamsisitizia awe makini.
Bwana bwana, jamaa akapanda mimi nikapanda nyuma, akang'oa chuma. Nikawa naona jamaa anapandisha gia tu kila baada ya mita chache. Ndani ya dakika chache jamaa akawa ameshaikamata gia namba 5 huku spidi ikiwa ni kali sana. Mimi nikaanza kutoka na kijasho nimsihi jamaa apunguze mwendo lakini wapi.
Sasa tukafika sehemu kuna kona kali sana, na ukinyooka kwa mbele bila kukata hiyo kona kuna ka bonde halafu unakutana na reli iliyoinuliwa na kokoto. Sasa jamaa alivyoona kuwa hawezi kupiga kona ikabidi anyooke. Kwanza pikipiki iliruka na tukapita katikati ya miti ya vichaka vichaka, ilipokwenda kutua jamaa bado alikuwa na wenge akazidi kuvuta mafuta, nikaona tunaanza kupanda mlima wa kokoto za relini ikabidi niruke na kamaa akaenda kumamia juu ya makokoto. Cha kushukuru hatukuumia sana, ila pikipiki ilikuwa nyang'anyang'a.

2. Mimi na mshua tulikuwa tunatoka kwa bibi kuwasalimia, tukawa tunarudi nyumbani kila mmoja anaendesha pikipiki yake tukiwa tunapita kwa ile barabara ya dom-singida. Sasa mshua akawa anaendesha slow, nikaambua kumuacha mimi nikatangulia. Sasa likaja semi kwa nyuma likanipita nikasema wewe sikuachi, nikaanza kulifukuzia kwa nyuma ili nami nilipite. Tukaenda wee, baadayr nikasema sasa huu ndo muda wa kuovatake na nikaamua kuovateke kwa kushoto. Bwana wee, ile nakaribia kulipita nikaanza kuona semi linakuja kuande wangu kwa kasi, sijui ndo dereva alikuwa ananifanyia kusudi. Ikabidi nitoke barabarani nikaingia machakani huku nikijitahidi nisidondoke maana nilikuwa kasi sana. Kwa hofu iliyonikumba nikawana naendesha huku nalia kwa kupiga mayowe. Nikaenda kusimama kwa mbele kabisa nikiwa nimechubukachubuka. Niliwatukana sana wale jamaa.
3. Nikiwa na pikipiki yangu ile ile nikiwa nimetoka misele narudi nyumbani nikakuta mto umejaa maji japo hayakuwa mengi sana kiasi cha kutisha, nikasema hapa ntapita tu.
Mzee baba nikajitosa, kufika katikati ya mto ngoma ikazima. Ilipozima maji yakaingia kwenye dude la kutolea moshi, kwa hiyo hapo pikipiki kuwaka tena ni mtihani. Nikiwa sijui nifanyeje nikaona naanza nasombwa mimi na pikipiki yangu. Ikabidi nitoke nikaicha pikipiki ikaanza kubebwa baadaye nikawaza nikiiacha inaweza kwenda mbali na ikaharibika, ikabidi nijitose mtoni ili niitoe. Maji yaone kwenye glasi tu, shughuli iliyonipata pale mtoni nilianza kuwaona akina eskarioti na washkaji zake.
Hahaha hiyo pikipiki ulivyobaki nyang'anyang'a mshua wenu mlienda kumweleza nini sasa manake sipati picha, waendesha pikipiki wengi huwa wanapata ajali kwa sababu ya sifa za kutaka kushindana na magari..mkubwa atabaki kuwa mkubwa tu. Nimecheka eti ukaanza kuwaona akina eskariot na washikaji zake
 
Itakuwa muanzisha uzi ni mtu wa iringa...nilienda kutembea huko mwaka huu nikashangaa kichombo/kipimio kikiitwa Lita, wanakitumia kupima vitu vya uzito kama njegere, maharagwe...ukitumia akili ya shule unaweza usielewe maana mambo ya lita ni kwenye vi/kimiminiko tu
Hujakosea mkuu wangu mimi ni wa ukanda huo na tukiona unashangaa kipimo cha lita sisi pia tunakushangas vilevile haha
 
Hahaha hiyo pikipiki ulivyobaki nyang'anyang'a mshua wenu mlienda kumweleza nini sasa manake sipati picha, waendesha pikipiki wengi huwa wanapata ajali kwa sababu ya sifa za kutaka kushindana na magari..mkubwa atabaki kuwa mkubwa tu. Nimecheka eti ukaanza kuwaona akina eskariot na washikaji zake
Mshua wangu hanaga noma sema mimi ndo nilikuwa nahofia. Tuliikokota hadi kwa fundi then ndo nikamwambia kuwa tumepata ajali, akauliza pikipiki ni nzima? Nikamwambia, sisi ndo wazima ila pikipiki haitamaniki. Akaja pale kwa fundi akaulizia tu ilikuwaje then akalipia gharama za matengenezo.
 
Bwana bwanaaaaa

Ilikuwa 2014 mbeya,msimu wakulima wanavuna maharagwe,basi mimi na mwanangu alikuwaga na gari aina ya pikup tukawa tunapiga dili za kuwasomba wamama waliotoka vunatoka shamba huko maeneo ya inyala imezu n.k tunawapeleka uyole

Siku hiyo mishale kama ya saa nne usiku tutakwafumania bhana wako kama saba hivi na magunia yao ya maharagwe,tukaingiwa tamaa ya kuwabeba wote na wao wakakubali lakini sasa gari haitoshi...ikabidi mimi ninitoe muhanga kupanda nyuma kule juu kabisaaaa ya magunia ya maharagwe....sasa tukatoka imhezu freshi tu.

Ule mzigo ulikuwa unayumba lakini muuni kibishi nikawa nakomaa tu tunaenda kitata.

Mwanzoni jamaa alikuwa anaendesha kistaarabu akijua juu kuna mtu,alivyoona silalamika akaanza kunogewa,kufika eneo la kilimo pale jamaa akakanyaga moto bhanaaaa,mara pappp mbele gari iko site yetu...ikawa anaenda kuivaa waziwazi akafanya manuva kuichengesha kuikwepa....bwana wweeee mimi huku juu naona kifo hiki hapa na nishajikojolea kwa hofu.

Kushtuka niko chini bahati nzuri sana niliangulia juu ya magunia ya maharagwe na tukafanikiwa kupishana lakini mimi niko chini.

Kusema ukweli ile siku nilitoa haja kubwa
[emoji3] [emoji3] [emoji3] [emoji3] , dah pole mkuu
 
I want to say something but am holding back. Ni wapi nimesema hawajui kutofautisha kilo na lita? Someone help me...hivi ni kweli hakuna sehemu amnayo wanapima mahindi, maharagwe viazi n.k kwenye lita? Hivi mtu wa kijijini ametoka shambani na njegere zake au huyo muokota kumbikumbi ametoka zake huko kuziokota hiyo kilo ya kupimia akaichukulie wapi? Madam why must we argue over something so insignificant? Hivi hata hapa Dar ukipita barabarani humo watu wanauza njegere mbichi kwenye lita moja au nne au mwenzetu mitaa ya huku uswahilini hujawahi kupita we wapitaga tu masaki?
Nimefuatilia majibizano yenu nyie wadada kuna jambo hamuelewani ila mpo upande mmoja. demi hiyo lita anayosema mdada hapo ni kipimo kama kipimo cha kawaida ulivyozoea huku mjini na ukae ukifahamu kila kijiji au sehemu zina lugha zao za utambulisho wa vitu.
 
Nimefuatilia majibizano yenu nyie wadada kuna jambo hamuelewani ila mpo upande mmoja. demi hiyo lita anayosema mdada hapo ni kipimo kama kipimo cha kawaida ulivyozoea huku mjini na ukae ukifahamu kila kijiji au sehemu zina lugha zao za utambulisho wa vitu.
Tumeshaelewana tumemaliza boss
 
Back
Top Bottom