Mwezi wa 2 mwaka huu home tulikula chakula chenye sumu(inasemekana ilikua samaki) asubuhi tumeamka ilkua siku ya j2, mke kaamka katoka nje baada dk 10 hv karudi mbio akasema watoto(wapo mapacha) pamoja na mdada wa kazi wanaharisha sana, wakati wanajiandaa kwenda hospitali mara kaja mlinzi aliekuja kumpokea mwenzake anadai mwenzie yupo hoi kaharisha usiku kucha hata kuinuka hawezi (alikua anakula home jioni) wakapigia ndugu zake wakaja na gari ya kampuni wakampeleka hospitali,
Nikapakia mke, dada na watoto nkawapeleka pale kwa hospital kwa mama ngoma, nkarudi home maana alibaki mtoto mdogo,
Baada ya kurudi na mimi nkanza trip mdogo ndogo hadi ikafika namwaga maji tu lkn najiskia poa wala siumwi popote kufika saa 6 nkaona hii hali sio ntaishiwa nguvu maana kila dk toi, nkaanza safari kwenda hospital nkaanza kuhisi nguvu zinaisha, sikuchukua gari nkaenda kupanda daladala niende hospital niliyoizoea ipo kkoo, nimetokea sinza mapambano kufika kwa remi hali ikawa mbaya sana, nkawa nachungulia vibao pembezoni nikionna cha hospital nishuke (sikutaka kwenda Palestina) kufika karibu na kijiweni nkaona kibao nkamwambia konda akanishusha, kufika hospital drip 3 za fastaa huku vipimo vinaendelea, hali ilizidi kua mbaya nilijiskia kufakufa nikawa napiga ule ukuta wa wodini makofi tu mara nkazima mazima kuja kushtuka saa 2 usiku niko vizuri kiasi...
Nashkuru Mungu hakuna aliedhurika zaidi....