Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Mie bhana nakumbuka ilikuwa 2003 nipo Darasa la Tano Kunduchi Dar.

Kisa kenyewe ilikuwa ni ugomvi baina yangu mm na mwanafunzi mwenzangu wa darasa la saba.

Sijui ni utoto au nini tukapanga tupigane baada ya muda wa masomo kuisha. Mie nilikuwa na kundi kubwa la wapambe asikwambie mtu ukiwa na wapambe unajiamini balaaa.

Mwenzangu yupo peke ake baada ya muda wa masomo kuisha tukaruhusiwa, Wana wakanipanga twende zetu na yule mpinzani wangu akatafutwa tukatokomea porini uko.

Nikavua Begi wapambe wakanishikia jamaa akasogea ngumi zikaanza Daah mie nina bonge la nyomi la wapambe Piga huyo!! Mng'oe Meno huyo!!

Bichwa likavimba Mbwembwe nyingi ,Basi mara Ngumi Mara Teke, Kwepa Tena Kwepa Nikampatia Moja Saafi ya Mdomo Akachanika Kidogo Damu Ikaanza Kutoka.

Daah kumbe ndo nimemjeruhi simba, Nilikula mbata za kutosha hadi nikaona kizunguzungu nikazirai.

Wana wote wakakimbia nililala pale sijitambui kwa nusu saa. Bahati kuna mzee alikuwa anapita akaniona nimelala uso umevimba Shati limechanika Daah

Ndo akanibeba kunipeleka shule uku sijitambui kuwaelezea walimu nikamwagiwa maji sijui ndo kunipeleka hospital Wakaitwa wazazi.

Daah Kesi ilikuwa kubwa mno, Wazazi wote wakaitwa.Nashukuru Mungu yaliisha ila nimekoma Kupewa Sifa za Kijinga Inaponza Watu.
 
Mie bhana nakumbuka ilikuwa 2003 nipo Darasa la Tano Kunduchi Dar.

Kisa kenyewe ilikuwa ni ugomvi baina yangu mm na mwanafunzi mwenzangu wa darasa la saba.

Sijui ni utoto au nini tukapanga tupigane baada ya muda wa masomo kuisha. Mie nilikuwa na kundi kubwa la wapambe asikwambie mtu ukiwa na wapambe unajiamini balaaa.

Mwenzangu yupo peke ake baada ya muda wa masomo kuisha tukaruhusiwa, Wana wakanipanga twende zetu na yule mpinzani wangu akatafutwa tukatokomea porini uko.

Nikavua Begi wapambe wakanishikia jamaa akasogea ngumi zikaanza Daah mie nina bonge la nyomi la wapambe Piga huyo!! Mng'oe Meno huyo!!

Bichwa likavimba Mbwembwe nyingi ,Basi mara Ngumi Mara Teke, Kwepa Tena Kwepa Nikampatia Moja Saafi ya Mdomo Akachanika Kidogo Damu Ikaanza Kutoka.

Daah kumbe ndo nimemjeruhi simba, Nilikula mbata za kutosha hadi nikaona kizunguzungu nikazirai.

Wana wote wakakimbia nililala pale sijitambui kwa nusu saa. Bahati kuna mzee alikuwa anapita akaniona nimelala uso umevimba Shati limechanika Daah

Ndo akanibeba kunipeleka shule uku sijitambui kuwaelezea walimu nikamwagiwa maji sijui ndo kunipeleka hospital Wakaitwa wazazi.

Daah Kesi ilikuwa kubwa mno, Wazazi wote wakaitwa.Nashukuru Mungu yaliisha ila nimekoma Kupewa Sifa za Kijinga Inaponza Watu.
Hahaha mambo ya shule bwana mimi nilikuwa nami napigana hatari
 
Poleee sana,

Kwa upande wangu, kuna simbilis moja almanusra inifanye nipak vitu vyangu niondoke duniani, shenzi sana, mapenzi haya


Anyway.. tuyaache hayo

miaka ya Nyuma kidogo hapo, nikiwa kama standard three hv au two, nikiwa kwa babu mzaa mama moshi vijijin huko, siku moja nimepanda juu ya mti wa mmerez, (kwa wanao ifahamu hii miti ukiwa umekomaa n mrefu sana) nilikua naupunyua matawi, bwana wee huku na huko nimekata tawi lina kama V hv, hiyo V si ikaja ikanivaa shingon kama tai hv... nilijaribu kulivua weee lakn wapi, huku na huko wapi (nilikua bado mdogo, chini ya miaka 10) so uamuz wa haraka ukanijia nijiachie tu nidondoke nalo, nikaachia panga likatangulia kwanza... Yaan ilitokea kama miujiza vile, ile nataka kujiachia tu likanivuka lenyewe, niko hoi bin taaban hapo, nguvu zenyewe zalisha anza kuisha, nikashuka nikaenda kulala
Umenifurahisha sn jins ulivisimulia yaan km natazama muvi...
# nkataka kjiachia nishuke nalo mara paap likachomoka shingoni, nikaenda lala hapohapo# [emoji38]
 
Ha ha ha ha ni kwel halafu hao ndio wanachukua mara tatu zaid ya utundu wetu sis Kaz ipo, But kuna muda nasema umesaidia sana kizaz chetu atlist kuwa creative kuliko hawa wa sasa
Kaazi kwelikweli na wazazi wa siku hizi mnavyojua 'kuwapenda' watoto wenu basi hamjui hata kitu inaitwa kiboko kazi ipo
 
Lake chala, hili ziwa lipo mpakani mwa kenya na tanzania, nimechungulia kifo mara 2, nikasema sitakaa niende tena huko

1. Nilinusurika kuzama, ziwa lina kina kirefu sana hatua moja kutoka ulipo inatosha kabisa kukuzamisha, nimejifanya mtaalamu nikasogea kidogo, nikahisi kama kuna kitu kimenishika miguu kunivuta chini, nikazama, nikarudi juu nikazama tuna kurud juu kwa kasi nikamvuta jamaa aliyekuwa karibu mimi nikatoka, bahati jamaa alijitahidi kurudi nchi kavu

2. Tulienda kwa mara ya pili nikasema siogelei, nikakaa pembeni nimevua tshirt yangu mpyaa kwa ajili ya siku hiyo, mda wa kuondoka nikawa nimeisahau ile tshirt pale chini (huwa ninajiuliza sababu) nimeambaa na mawe umbali wa kutosha nikakumbuka afu wenzangu wametangulia daah, nikarudi na kuichukua, hapo hapo nasikia kitu kinanipush kupita njia nyingine tofauti na na tuliyoshukia (ziwa lipo kwa chini) nipo mwenyewe nimeanza kumake step ninaona bonge moja la nyoka ananiangalia daah hizo mbio zake halafu kwenye mawe makubwa, nikateleze nikaingia kwenye maji nikajitajidi nikatoka na kufanikiwa kuwapita hata wale wliokuwa wameanza safari wa kwanza kabisa...sitasahau hii
 
Kaazi kwelikweli na wazazi wa siku hizi mnavyojua 'kuwapenda' watoto wenu basi hamjui hata kitu inaitwa kiboko kazi ipo
Hapo ndio tunakosea imagine wenzangu waliokuwepo walikua na akili ya kunivuta na kuntoa kwenye maji bila msaada wa watu wazima i had to re write notes za masomo yote nkachukua kiatu cha mshua cha zamani nkakipiga rang nyeusi fresh nkaenda shule nawaza hawa watoto wa siku hzi do they even dare au ndio kusubir spider man na hanah montana cartoons
 
Story yangu inaanza kama ifuatavyo baada ya kumaliza shughuli zangu za kuuza chipsi usiku napita karbu na nyumba ya jiran namsikia bwana mifugo akimwambia jiran yangu ambae ngombe wake alkuwa kasha dead amzike Mara moja kwani alkuwa ana anthrax basi nikaendelea kupeleleza nkaona alpomzka walipomaliza walivyoondoka nikaenda mfukua skuwa na gloves nikavaa mifuko ya Rambo maana nlsikia akisema ugonjwa ni hatar unaambukzwa na bacteria aina ya bacillus anthrax sjui kama nimepatia spelling au laa ila hayanihusu basi tuendelee na story basi bwana nikamuosha nikamkatakata vipande kesho nikamuuze mishkak vipande vilivyobakia nikampa mshkaj aweke kwenye freezer lake maana anatuchaj per day bwana nikauza wee mara watu wakaanza kuanguka baada ya kula wengne kutapika na kuhara palepale RAIA waliponishtukia wakaanza nikimbiza na mapanga wengine magongo sauti zilisikika zikisema "lazma tukukate vipandevipande" kwa bahat nzur kulikuwa kuna fuso sjui Lori hata skumbuk vzr lilikuwa linaanza kuondoka sjui lilikuwa linaenda WAP bas bwana nikalidandia baada ya masaa mawil mule ndan ya fuso simu yangu inaita mama mwenye nyumba anasema upo WAP mbona kuna polis wanakutafuta hapa nikakata Sm mara tena simu inaitaa kapiga RFK take yule mshkaj anatuifadhia nyama akasema nyama yako ina nn jamaa alikuibia kdogo kaenda itumia gheto sahiv ninavyokwambia tumemuwahisha hospital nikakata Sm .gar likiwa linaenda ktk kukaguakagua mule ndan nikakuta magunia kuyacheck ndani naona bangi pia kulikuwa na madawa mengne syajui kumbe skudandia fuso nilidandia kifo Mara gar likasimama kumbe hlo eneo kulikuwa na police patrol nkasikia shuken wote tukague gari
😀😀😀 Malizia mkuu.
 
Aisee nimecheka sana maana tukio kama hili lilinitokea nikiwa nakata majani juu ya mti unaoitwa "mhesi" kule Rombo, kumbe nilikuwa nimeshikilia kimti kikavu kikakatika nikashuka kwa kichwa hadi chini phuuh!.
Nilijaribu kuinuka nikae lakini nikashindwa na sauti ya kulia nayo ikawa haitoki. Nikatulia kama dakika moja nguvu zikanijia lakini shingo sidhubutu kuigeuza maana ilikuwa inauma balaa.
Niliposimama nikageuka kumbe pale chini palibakibaki na nywele za kichwani kutokana na kile kishindo nilichoanguka nacho [emoji23][emoji23]
Siku nyingine tena nilitoka shule nikawahi fasta kwenda kupanda juu ya mwembe kujisevia kama ilivyo kawaida yangu, baada ya kula na kushiba hukohuko juu ikawa ni wakati wa kushuka sasa.
Nilikuwa na tabia ya kushuka kwa kutumia matawi ya huo mwembe,, sasa wakati natumia tawi kushuka si likaachia kule juu/likakwanyuka kwa kuzidiwa na uzito! Nilitangulia chini nikiwa nabembea na ule mti hadi chini alafu matawi yake yakanifunika nikalala palepale usingizi mzito hadi usiku wa saa 2 kasoro ndio nilizinduka
Hahahhahaha dah, pole sana ila kwakweli nimecheka mno.
 
Nimekumbuka nyingine niligongwa na gari,

Hii ilinikuta mtoni pale himo, tulikuwa tumeenda kuogelea, wakati tunarudi askari nao wakawa wametoka kupeleka farasi wao, kuna farasi ambaye nilikuwa nimemzoea uncle wangu alikuwa anakuja nae home(kikosi cha farasi) alivyoniona akawa ananifuata mwenzake wanamfuata daah nkaingia uoga nilijikuta ninakimbia nikagongwa na gari, nakumbuka nilijikuta niko hospital naletewa mtori
 
Lake chala, hili ziwa lipo mpakani mwa kenya na tanzania, nimechungulia kifo mara 2, nikasema sitakaa niende tena huko

1. Nilinusurika kuzama, ziwa lina kina kirefu sana hatua moja kutoka ulipo inatosha kabisa kukuzamisha, nimejifanya mtaalamu nikasogea kidogo, nikahisi kama kuna kitu kimenishika miguu kunivuta chini, nikazama, nikarudi juu nikazama tuna kurud juu kwa kasi nikamvuta jamaa aliyekuwa karibu mimi nikatoka, bahati jamaa alijitahidi kurudi nchi kavu

2. Tulienda kwa mara ya pili nikasema siogelei, nikakaa pembeni nimevua tshirt yangu mpyaa kwa ajili ya siku hiyo, mda wa kuondoka nikawa nimeisahau ile tshirt pale chini (huwa ninajiuliza sababu) nimeambaa na mawe umbali wa kutosha nikakumbuka afu wenzangu wametangulia daah, nikarudi na kuichukua, hapo hapo nasikia kitu kinanipush kupita njia nyingine tofauti na na tuliyoshukia (ziwa lipo kwa chini) nipo mwenyewe nimeanza kumake step ninaona bonge moja la nyoka ananiangalia daah hizo mbio zake halafu kwenye mawe makubwa, nikateleze nikaingia kwenye maji nikajitajidi nikatoka na kufanikiwa kuwapita hata wale wliokuwa wameanza safari wa kwanza kabisa...sitasahau hii
Haha kama nakuona mkuu
 
Nimekumbuka nyingine niligongwa na gari,

Hii ilinikuta mtoni pale himo, tulikuwa tumeenda kuogelea, wakati tunarudi askari nao wakawa wametoka kupeleka farasi wao, kuna farasi ambaye nilikuwa nimemzoea uncle wangu alikuwa anakuja nae home(kikosi cha farasi) alivyoniona akawa ananifuata mwenzake wanamfuata daah nkaingia uoga nilijikuta ninakimbia nikagongwa na gari, nakumbuka nilijikuta niko hospital naletewa mtori
OMG pole mkuu
 
Moshi town kukatwa na sime

Hii nayo ingenisababisha niage dunia, mshkaji wangu kabisa tulikorofishana, aliiba kitu home kwetu nikawa ninamwambi arudishe ugomvi ukaanzia hapo, iyo siku amerudisha nipo home nikamwambia mwanzo na mwisho kukanyaga home, ghetto nilikuwa nina sime ya kimasai jamaa aliivuta kaniletea shingoni nikahepa kidogo ikanichubua mpaka leo nina alama, ilienda kutua kwenye ukuta kwa namna ilivyo chimba ukuta isingeniacha salama
 
Dodoma kipigo cha mbwa koko

2010, dodoma kulikuwa kuna bash royal village dogo wangu akanitunuku rafiki zake wawili niende nao, walikuwa wamevaa ovyo, party ikaisha mda wa kuondoka tunatoka nje tunaelekea kweny gari mob ikaanza kuwavuta wale mademu, ikabidi nikimbie fasta kuchukua gari mademu nimewaacha na mshkaji wangu wamezongwa zongwa, kurudi pale wademu wameingia mmoja seat ya mbele mwingine kakaa nyuma na mchizi, kufumba na kufumbua mob imezingira gari wanataka mademu, mara kioo kimevunjwa mlango umefungulia mademu wanavutwa wamebebwa juu juu ndio kushuka na mimi kwenda kuwaokoa, ebanaeeee nilichezea kichapo siyo cha nchi hii, nilichoropoka nikarudi hotelini, gari la aunt yangu nyang’a nyang’a, demu mmoja aliokolewa na mabaunsa mwingine aliliwa mtungo vichakani
 
Moshi town kukatwa na sime

Hii nayo ingenisababisha niage dunia, mshkaji wangu kabisa tulikorofishana, aliiba kitu home kwetu nikawa ninamwambi arudishe ugomvi ukaanzia hapo, iyo siku amerudisha nipo home nikamwambia mwanzo na mwisho kukanyaga home, ghetto nilikuwa nina sime ya kimasai jamaa aliivuta kaniletea shingoni nikahepa kidogo ikanichubua mpaka leo nina alama, ilienda kutua kwenye ukuta kwa namna ilivyo chimba ukuta isingeniacha salama
Duuuh, hatarii jamaa vipi huku mshughulikia?
 
Back
Top Bottom