Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Hakika
Shetani yupo kazini
MUNGU pia yupo,halali wala hasinzii kwa ajili ya maisha ya kwetu

Na hii kitu niliwahi onyeshwa(huwa naota na napata mafunuo kwa njia ya mawazo)
Lakini kwa umri niliokuwa nao sikuelewa,pengine kwa sababu ya utoto na imani yangu ilikuwa ndogo nadhani.
Ila Mungu yupo, Mungu wetu ni Mungu wa vita...ana nguvu.
God heals everything
All the pains i passed through yet He was there for me




Kuna wakati anafanya pasi na kumuomba..
Huwa nashangaa Sana kuna watu huwa hawaoni sababu ya kumshukuru Mungu,wameelekeza sana malalamiko kwa Mungu kuliko shukrani,hawajui wao kumaliza siku wakawa wazima wa afya,wanakula,wanaona,wanatembea,wanaongea ni sababu tosha za kumshukuru Mungu.
I hope now unajua jinsi ya kufanya iwapo umeonyeshwa mabaya yaliyo mbele yako
 
Wakati niko mdogo nilipitia mateso mengi sana...

1.mpaka nafikia kati ya miaka mitano mpaka sita.. nilikuwa sijawahi kumuona mzazi wangu (mama)/wazazi

Nilkuwa nasikia tu kwamba kaenda mjini na baba kutafuta maisha...na hiyo nilkuja kujua baadae muda wa kuanza shule.. lakini muda wote huo nilijua shangazi ndie mama yangu.

siku moja niko kwenye kijumba ambacho kilikuwa ni jiko..kwa wale waliokaa vijijini wanaeza elewa.
Hiyo ilkuwa ni baada ya kumaliza kuogeshwa na shangazi yangu..

Basi nikaenda kuota moto kwenye kile kijumba cha nyasi chenye jiko la mafiga ndani.. wakati huo mtoto wa shangazi akimaliziwa kuogeshwa.

Wakati niko naota moto kanga niliofungwa... kwa mtindo wa lubega kama sikosei,

Sijui nini kilitokea ila nadhan njaa ilinifanya nikasinzia....ndani ya dakika chache tu ile kanga ilishika moto, na ule moto ulishika paa la kile kijumba na kufanya nizungukwe na moto kila upande.

Moto ulikuwa mkubwa.. nilipiga kelele sana, kanga yote iliungua ikiwa mwilini na baada ya kupata msaada kutoka kwa majiran na shangazi kuzima moto.
Nilitolewa nikiwa uchi

Kila mtu alishangaa hakuna sehemu yoyote nilioungua zaidi ya mkononi kwa juu kuelekea begani..tena ngozi ilitoka kwa ukubwa wa shilingi tu
wakati huo kanga na jiko zima limeteketea kwa moto.

Mungu ni mwema... kila wakati.
####################

Nikipata muda nitawaambia kuhusu... kupatwa na uvimbe kichwani uliotaka kutoa uhai wangu kijijini... nikiwa mtoto ambae nina muongoza bibi yangu aliekuwa kipofu nadhani mna wafaham watoto wa namna hiyo.

Tusimsahau m/mungu...
wazazi ulionana nao?
 
Dodoma kipigo cha mbwa koko

2010, dodoma kulikuwa kuna bash royal village dogo wangu akanitunuku rafiki zake wawili niende nao, walikuwa wamevaa ovyo, party ikaisha mda wa kuondoka tunatoka nje tunaelekea kweny gari mob ikaanza kuwavuta wale mademu, ikabidi nikimbie fasta kuchukua gari mademu nimewaacha na mshkaji wangu wamezongwa zongwa, kurudi pale wademu wameingia mmoja seat ya mbele mwingine kakaa nyuma na mchizi, kufumba na kufumbua mob imezingira gari wanataka mademu, mara kioo kimevunjwa mlango umefungulia mademu wanavutwa wamebebwa juu juu ndio kushuka na mimi kwenda kuwaokoa, ebanaeeee nilichezea kichapo siyo cha nchi hii, nilichoropoka nikarudi hotelini, gari la aunt yangu nyang’a nyang’a, demu mmoja aliokolewa na mabaunsa mwingine aliliwa mtungo vichakani
Au ndo huyo demu mwenye HIV anaye trend tik tok maan naye alibakwa dodoma huko
 
Back
Top Bottom