Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Tuliowahi 'kuchungulia kaburi' tukutane hapa

Kuna pimbi moja ilikuwaga na papuchi tamu sana kidogo inipeleke akhera aisee.
Wayback miaka kadhaa nyuma kuna dem mmoja wa kizaramo alitugonganisha geto na msela alikuwa anasoma TEKU. Ilikuwa Mbeya maeneo ya Block T kilichotokea kutokana na ugomvi nilichomwa kisu mara mbili shingoni.

Ilikuwa ni balaa ndani ya sekunde chache nilianza kuona giza giza huku macho yakipoteza uwezo wa kuona, yaani kitu kama usingizi mzito na kupumua kwa kutumia nguvu kubwa.Mwili wote ulilegea ukiwa hauna nguvu kabisa.

Nilichokigundua ukielekea kufa huwa hakuna maumivu kabisa Ila huwa ni majuto ,hofu ya kufa na kutokuamini kama maisha ndio yanafikia mwisho. Ndani ya mda huo nilitamani ningerudisha mda nyuma hata kwa Siku kadhaa chache.

Anyway thanks God I'm still alive,baada ya kupoteza fahamu nilijikuta hospitali ya rufaa.
Ni kama habari yako nilisikiaga kumbe ndo ww
 
Kuna pimbi moja ilikuwaga na papuchi tamu sana kidogo inipeleke akhera aisee.
Wayback miaka kadhaa nyuma kuna dem mmoja wa kizaramo alitugonganisha geto na msela alikuwa anasoma TEKU. Ilikuwa Mbeya maeneo ya Block T kilichotokea kutokana na ugomvi nilichomwa kisu mara mbili shingoni.

Ilikuwa ni balaa ndani ya sekunde chache nilianza kuona giza giza huku macho yakipoteza uwezo wa kuona, yaani kitu kama usingizi mzito na kupumua kwa kutumia nguvu kubwa.Mwili wote ulilegea ukiwa hauna nguvu kabisa.

Nilichokigundua ukielekea kufa huwa hakuna maumivu kabisa Ila huwa ni majuto ,hofu ya kufa na kutokuamini kama maisha ndio yanafikia mwisho. Ndani ya mda huo nilitamani ningerudisha mda nyuma hata kwa Siku kadhaa chache.

Anyway thanks God I'm still alive,baada ya kupoteza fahamu nilijikuta hospitali ya rufaa.
Aisee pole sana boss hadi nimeogopa...
 
Namkumbuka miaka ya 90 mwishoni mwishoni huko kipindi nikiwa kijijini kwa babu huko migombani migombani moshi, kipindi hicho nikiwa kwenye level ya juu kabisa ya utundu na ukurofi, yaani nikiambiwa kitu mi nafanya kinyume chake, yaani chochote kilicho hatarishi mi ndo akili ilinituma nicheze nacho, sumu sumu za kahawa hizi zilishanifanyia booking kama mara 2 hivi Ila safari zikaahirishwa, nyuki nao hawana adabu kabisa, tena hawa nyuki wa kwenye mapango mapango ni washenzi sana . ila hii kupenda penda asali nayo bana daaaah!! alikufa ng'ombe mi nikapelekwa hospitali,
Sasa kuna siku moja bana, nakumbuka ilikuwa kipindi cha kiangazi nimerudi zangu kutoka skuli jua kali mbaya halafu nina njaa kama ya wiki hivi, nyumbani sioni mtu na hakuna dalili na jikoni pamenuna, nikaona isiwe tabu nikachukua zangu manati nikazama migombani. Kwenye pitapita zangu huko kwenye mikahawa na migomba nikaona kapapai kapo juuu kule karibia kabisa na izraeli mtoa roho anakoishi, shetani alivyo mwehu akaniambi "wewe ni mwanaume panda faster" nikavua chachacha zangu kiroho safi, nikaanza kupanda, daaaah! Kumbe kale kapapai kalikuwa mtego sijui ndo chambo bana! mpapai wenyewe ni ile mipapai sijui ni ya enzi gani maana imekaakaa kama ile minazi ilopandwa enzi za sultan Said sayeed kule zanzibar. Nikajitutumua mtoto wa kiume, shetani nae ananambia "pambana", nikajivuta mtoto wa kiume, shetani nae anakazia "Nenda..." nikafika katikati kuna matawi, nikakaa kwenye tawi nikapumzika, baada ya kama dk 5 safari ikaendelea, mtoto wa kiume nikapambana mzee, nikajikunja mwanaume, nikajivuta sana, shetani nae anakazia "twende tu" daaah, nikafika kwenye vitawi vya pili nikapumzika tena, shetani akanipa wazo, "hebu simama ujaribu kama utafikia, nikasima nikajinyooosha lakini wapi! Nikajivuta lakini wapi...!!
Nyie!!. Shetani mhuni sana, nikakumbatia mpapai nikaendelea na safari, nikajituma sana, nikajinyoosha sana tu, aisee!! Daaah nikafika! Daaaah nikaukumbatia mpapai kwa nguvu then nikakanyoosha mkono wa kushoto nichukue nilichofata, aisee nyie watu. Nakumbuka tu sauti ya kukatika Ule mti wa mpapai Ila baada ya hapo sijui nini kiliendelea. Hadi leo mapapai huwa sili.
Hahahhaaa mkuuu
 
Kuna pimbi moja ilikuwaga na papuchi tamu sana kidogo inipeleke akhera aisee.
Wayback miaka kadhaa nyuma kuna dem mmoja wa kizaramo alitugonganisha geto na msela alikuwa anasoma TEKU. Ilikuwa Mbeya maeneo ya Block T kilichotokea kutokana na ugomvi nilichomwa kisu mara mbili shingoni.

Ilikuwa ni balaa ndani ya sekunde chache nilianza kuona giza giza huku macho yakipoteza uwezo wa kuona, yaani kitu kama usingizi mzito na kupumua kwa kutumia nguvu kubwa.Mwili wote ulilegea ukiwa hauna nguvu kabisa.

Nilichokigundua ukielekea kufa huwa hakuna maumivu kabisa Ila huwa ni majuto ,hofu ya kufa na kutokuamini kama maisha ndio yanafikia mwisho. Ndani ya mda huo nilitamani ningerudisha mda nyuma hata kwa Siku kadhaa chache.

Anyway thanks God I'm still alive,baada ya kupoteza fahamu nilijikuta hospitali ya rufaa.
Aiseee...Kisa papuchi????[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]aiseee...
 
Aiseee...Kisa papuchi????[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]aiseee...
Hata wewe yanaweza kukukuta boss usicheke sana, kumbuka waligonganishwa na aliyemchoma kisu ni mwenzie si kwamba walichomana.
 
Hata wewe yanaweza kukukuta boss usicheke sana, kumbuka waligonganishwa na aliyemchoma kisu ni mwenzie si kwamba walichomana.
Duuh kweli mkuu...lakini huyo jamaa aliyemchoma mwana kisu aisee ni mpuuzi anastahili kifungo kabisaa
 
Niliwahi kuota nimekufa usingizini, nilivyostuka sikulala mpaka kumekucha usingizi uliyeyuka wote. Usicheze na kifo asee,ni mziki mwingine kabisa
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Nilinsurika kufa( kwa kuanguka kutoka juu ya mti mwaka 2009) ila tangu hapo nikikumbuka tukio hilo miguu na viganja vinapata alarm !!! Jamani kifo kisikie tu!!!
 
Nilinsurika kufa( kwa kuanguka kutoka juu ya mti mwaka 2009) ila tangu hapo nikikumbuka tukio hilo miguu na viganja vinapata alarm !!! Jamani kifo kisikie tu!!!
Pole mkuu
 
Zamani nikiwa kijana mdogo mkoani tabora tulikua tunatoroka shule na kwenda stesheni kudandia treni, tulienjoy tu vile tunadandia treni inaenda inarudi, sasa siku moja tuko kundi kila mmoja anang'ang'ania apande na huku treni inatembea basi ile kuvutana tukaanguka mwenzetu mmoja akaingia chini kabisa akasagwa na treni wengine kukatika miguu, mimi sikuumia ila kaptula ya shule ilichanika kuanzia mbele hadi nyuma ikawa kama sketi, shati lote lililoa damu za wale majeruhi, habari ikasambaa mji mzima watu wakaenda kitete hospital kuona kama watoto wao nao wamo, mama yangu alichanganyikiwa sana sasa kurudi mtaani kila mtu anajua stori aisee siku ile mimi na wenzangu tulikula kichapo cha mtaa kila mtu alijifanya anauchungu sitaisahau ile siku, r.i.p pendo hadi leo naikumbuka sura na viatu vyake.
 
Zamani nikiwa kijana mdogo mkoani tabora tulikua tunatoroka shule na kwenda stesheni kudandia treni, tulienjoy tu vile tunadandia treni inaenda inarudi, sasa siku moja tuko kundi kila mmoja anang'ang'ania apande na huku treni inatembea basi ile kuvutana tukaanguka mwenzetu mmoja akaingia chini kabisa akasagwa na treni wengine kukatika miguu, mimi sikuumia ila kaptula ya shule ilichanika kuanzia mbele hadi nyuma ikawa kama sketi, shati lote lililoa damu za wale majeruhi, habari ikasambaa mji mzima watu wakaenda kitete hospital kuona kama watoto wao nao wamo, mama yangu alichanganyikiwa sana sasa kurudi mtaani kila mtu anajua stori aisee siku ile mimi na wenzangu tulikula kichapo cha mtaa kila mtu alijifanya anauchungu sitaisahau ile siku, r.i.p pendo hadi leo naikumbuka sura na viatu vyake.
Duuh pole yaani wanawachapa tena
 
Aisee ilikuwa ajali mbaya snaaa.. Kushuhudia mtu anasagwa na treni duu[emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji22][emoji22][emoji22]
Zamani nikiwa kijana mdogo mkoani tabora tulikua tunatoroka shule na kwenda stesheni kudandia treni, tulienjoy tu vile tunadandia treni inaenda inarudi, sasa siku moja tuko kundi kila mmoja anang'ang'ania apande na huku treni inatembea basi ile kuvutana tukaanguka mwenzetu mmoja akaingia chini kabisa akasagwa na treni wengine kukatika miguu, mimi sikuumia ila kaptula ya shule ilichanika kuanzia mbele hadi nyuma ikawa kama sketi, shati lote lililoa damu za wale majeruhi, habari ikasambaa mji mzima watu wakaenda kitete hospital kuona kama watoto wao nao wamo, mama yangu alichanganyikiwa sana sasa kurudi mtaani kila mtu anajua stori aisee siku ile mimi na wenzangu tulikula kichapo cha mtaa kila mtu alijifanya anauchungu sitaisahau ile siku, r.i.p pendo hadi leo naikumbuka sura na viatu vyake.
 
Daah nimekumbuka nilivokulaga biskut zime expire. Akiamungu kifo nilikuwa nakiona hiki hapa.
Bwana Yesu asifiwe kwa wale wenzangu na mimi. Wengine habari zenu?

Ninapoelekea kutimiza miongo kadhaa ya kuwepo hapa duniani nimejikuta natafakari maisha yangu tangu pale nilipoanza kupata akili hadi leo hii nimejikuta natabasamu na kumshukuru sana Mungu maana nimekutana na mengi mazuri, mabaya, ya kukatisha tamaa ila katika yeye anitiaye nguvu nimeyaweza yote na nitaendelea kuyaweza yote.

Nimejikuta nakumbuka tukio moja la huko nyuma nikiwa na miaka sita hivi au saba (sikumbuki exactly ilikuwa mwaka gani). Mimi bwana nilikuwa naishi na sister tangu nikiwa mdogo sana na mpaka leo ukisikia nasema naenda nyumbani maana yake naenda kwa sister (naonekana kituko si eti eeh?)..tuachane na hayo kwanza.

My sister miaka hiyo alikuwaga mwalimu vijiji vya ndani kabisa huko, akiwa anaenda kuchukua mshahara anatumia siku tatu..siku ya kwanza kwenda, siku ya pili anaitumia kuchukua mshahara na kufanya mambo yake na hakukuwa ATM miaka hiyo kwa hiyo unaweza kupata picha na siku ya tatu anaitumia kurudi na wakati mwingine alikuwa anaweza kutumia hata siku nne.

Siku hiyo kabla hajasafiri alinunua kumbikumbi (wenyeji wa mikoa ya nyanda za juu kusini mtakuwa mnazijua, nilikuwa nazipenda sana) basi nilizifakamia zile ndude kama ugomvi, nilizikula kama lita moja hivi. Asubuhi ameamka zake hana hili wala lile akaondoka, mimi mida ya saa moja asubuhi nikaanza kuendesha, baadae nikaanza kutapika matapishi ya njano (mnaitaga nyongo sijui).

Kwa hiyo ikawa ni mwendo wa kuharisha na kutapika, sijui dawa yoyote na hata akili ya kwamba niende kwa jirani nikamwambie hali yangu nikawa sina sijui ndio utoto? Inafika mida ya saa nne mtoto nimechoka nikalala kwenye mkeka nje siwezi tena kusimama nikawa natapika hapohapo sina hata nguvu ya kusimama tena yaani nikawa nikifumbua macho hivi naona kila kilichopo mbele yangu kinazunguka. Ni miaka mingi imepita lakini picha ya siku ile haijawahi kunitoka.

Bahati nzuri akaja rafiki yake sister alikuwa hajui kama kasafiri ndio kunikuta katika hali hiyo akanibeba kunipeleka kwake maana kile kijiji hakikuwa hata na dispensary hadi kijiji cha jirani ... yule dada alikuwa anaitwa Fausta (RIP). Ndio ikawa pona yangu na sister alirudi baada ya siku tatu. Huwa najaribu kutafakari hivi asingekuwa yule dada kuja pale sister angenikuta niko hai kweli?

Tangu siku hiyo hakuwahi kuniacha peke yangu akisafiri maana siku zote nilikuwa najifanya konki siogopi kulala peke yangu. Tena wale wadudu niliwachukia jumla jumla sijawahi kuwala tenaa.

Kama na wewe mdau ulishawahi kupitia ugonjwa au hali yoyote ukaona kifo hiki hapa karibu tushee
 
Back
Top Bottom