Tujikumbushe vitabu vya zamani

Tujikumbushe vitabu vya zamani

1.Things Fall Apart
2.The River Between
3.A Man of the people
4.I will Mary when I want
5.Song of Lawino(Poem)
 
Hivi ni vitabu nilivyojibia mtihani wa form four, Three suitors one husband, The River Between, Things Fall Apart
Mimi nilijibia mtihani No Longer at easy The river between .....kitabu kimoja kina story ya kimasai hv nimesahau jina
 
Sanda ya Jambazi .....humo unawakuta akina Hakimu Mbaga....aliuwawa.....mahakimu tutoe haki jama
 
Mnamkumbuka huyu bwana?
Uh! umenikumbusha enzi za darasa la tano pale Muhimbili primary school,hizi comics zilikuwa
Mnamkumbuka huyu bwana?
Hizi comics nilizipenda sana mpaka tukafikia kuunda vikundi vya kuazimana comics,Mtu unazifuata kule ziliko hata kama ni mbali kiasi gani. Vitabu vya Umsolopogaas na Umbopa sivioni kabisa siku hizi. Ama kweli tumetoka mbali.
 
Uh! umenikumbusha enzi za darasa la tano pale Muhimbili primary school,hizi comics zilikuwa

Hizi comics nilizipenda sana mpaka tukafikia kuunda vikundi vya kuazimana comics,Mtu unazifuata kule ziliko hata kama ni mbali kiasi gani. Vitabu vya Umsolopogaas na Umbopa sivioni kabisa siku hizi. Ama kweli tumetoka mbali.
 
Ahsante sana mkuu kwa taarifa. Naomba unihakikishie kama nitavipata vitabu vifuatavyo hapo kwa Ben maana navihitaji sana:
Njozi iliyopotea
Gamba la Nyoka
Pepo ya Mabwege
Mzimu wa Watu wa Kale
Rosa Misitika


Nahitaji sana kitabu cha PEPO YA MABWEGE ili nimsome kwa UPYA Dr. Harrison Mwakyembe kama mawazo yake kwenye riwaya hii kwa wakati ule ndiyo aliyonayo sasa. Niliisoma riwaya hiyo mwaka 1989...!!
Utanisaidia sana kunielekeza duka lilipo ili siku nikija Dar nitembelee duka hilo.






Tafakari...!!
Cha Harrison Mwakyembe simo! Duka lipo IPS Building karibu na Askari Monument, ukifika utaliona Ben and Company Ltd, wanavitabu vingi sana na wanauza jumla pia!
 
Baadhi ya vitabu
3bfad5ff64e26b4542f1b12f4792d697.jpg
IMG_20170311_151038.jpg
IMG_20170311_151022.jpg
IMG_20170311_150949.jpg
 
safari za gulva (sijui kama nipo sahihi na jina) yule jamaa dr. wa kwenye meli alienda nchi yenye vijitu vifupi vya saiz ya nchi 6 tu, halafu badae akakutana na kisa kingine cha kwenda kwenye nchi yenye mijitu mirefu km minazi.

vingine ni kama TAFRIJA YA DAMU, SIMU YA KIFO, MPENZI JUZUU YA 1 na 2,
 
Navikumbuka vitabu vya Njama na Kikosi cha kisasi, mtunzi alikua akiitwa E.Musiba, hivi vitabu ukivisoma unakua unajihisi kama unashuhudia jambo halisia! Willy Gamba alikua hatari sana.
Ni kweli Mkuu.Musiba alikuwa na kipawa ya aina yake.

Anakutaji namba ya chumba (Mfano,Chumba namba 117 mtaa wa upanga),Urefu+Unene wa mhusika hadi unafurahi.
 
Mtunzi wake Rene Raymond alitumia majina mengi katika uandishi wake na moja ya majina hayo likiwa ni la James Hadley Chase. Alikuwa na kipaji cha pekee cha uandishi wa novel hadi kifo chake kwenye miaka ya 80. Baadhi ya vitabu vyake vilivyonisisimua mimi binafsi miaka hiyo ni pamoja na There's a Hippie on the Highway, Consider Yourself Dead, My Laugh Comes Last, Knock, Knock! Who's There, Just a Matter of Time, Have This One on Me, I Would Rather Stay Poor, Mission to Venice, You Find Him, I'll Fix Him na The Dead stay Dumb. Vitabu hivyo na vile vya Aristablus Elvis Musiba kama Kufa na Kupona, Kikomo, Kikosi cha Kisasi, Njama na Hofu vilinifanya nitamani sana kazi ya ukachero japo baada ya kukomaa kiakili nilifutilia mbali mawazo hayo.

Miaka hiyo ilikuwa ni fashion kutembea na novel kama hizo za James Hadley Chase mkononi hata kama hauisomi au kuiweka katika mfuko wa nyuma wa kaptula ya shule au suruali na kuiachia ionekane kidogo kwa juu ili kuwakoga wenzio au unaokutana nao njiani. Watu tumetoka mbali bwana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom