Tujikumbushe vitabu vya zamani

Tujikumbushe vitabu vya zamani

mzimu wa watu wa kale, roza mistika na kusadikika cha shaaban robert mnavikumbuka?
 
Ushauri wa bureeee, tafuta hivyo vitabu kama mtu anaweza fanya kazi hiyo, kisha toa copy chache kwa majaribio, tafuta kijana apite mtaa kwa mtaa atakutana na sisi wa zee wa zamani, na kisha piga pesa unaweza Shangaa

unaelewa nn kuhusu haki miliki?
 
Pia musiba alitoa kitabu HUJUMA muhusika mkuu akiwa willy gamba, lakini kilifungiwa, vipi kuna yeyote anacho?
 
Haramu! Mtunzi James Bwana. kiko vizuri sana hiki kitabu
 
kwakweli vilikuwa vizuri. Hakukuwapo haja ya television na social media.
Vilivuta hisia kiasi kwamba mtu hudhani ya kwamba tukio limetokea kweli.
Mtu ukiwa na kitabu kila akuitaye waona msumbufu akusumbua bureeee
vyangu nivikumbukavyo ni hivi
1. Mazungumzo ya alfu lela ulela
2. Kisiwa chenye hadhina
3. Maajabu ya mlima kolelo
4. Jamaaa hodari kisiwani
5. Hekaya za abunuwasi
5. Safari za juma ma sungura
6. Tunguli ya ajabu
7. Bulicheka
8. Mahugri mtoto aliye lelewa na nyani
9. Simba wa tsavo
10.???
Njoooni hapa tukumbushane uzuri huuu ambao kizazi hiki kimeukosa
karibuni

nataka iwe siri, rosa mistika, dunia tambara bovu, kuli, mine boy, songs of lawino, songs of okol, when an arrow of god, no longer at ease, things fall apart, the daughter of mumbi, whip not child
 
Kwa Tanzania Hajatokea Mtunzi Kama MUSIBA aliEtunga story ya HOFU na nina imani hakuna kitabu cha mfano kama hicho hapa TZ
 
Yeyote mwenye soft copy za vya kale dhahabu (old is gold) atuwekee humu tujisomee tupate uhondo.
 
haha WEZI wa mifugo ilikua dodoma hiyo walivamiwa na kupigwa mishale ma mikuki

Uko vizuri Chief... Waziikumbuka fikiri na Uledi, Mzee marebeto na mapambano dhidi ya Malaria, Mpapai na mitete?

kweli BRN imetushushia hadhi ya elimu yetu
 
Uko vizuri Chief... Waziikumbuka fikiri na Uledi, Mzee marebeto na mapambano dhidi ya Malaria, Mpapai na mitete?

kweli BRN imetushushia hadhi ya elimu yetu

mkuu, elimu ilikua zamani sasa hivi naona kila mtu mwandishi wa vitabu ubunifu kwisha kabisa!.
 
mkuu, elimu ilikua zamani sasa hivi naona kila mtu mwandishi wa vitabu ubunifu kwisha kabisa!.

Kweli mkuu. Hapo Karl Marx angetwambia ni 'ubidhaishaji wa elimu' au 'commodification of Education' kwa lugha ya Malkia. Kwa sasa uandishi ni kibidhaa zaidi na si kutoa huduma
 
Tumgidie -----, somo kaniponza, hivi nilivisoma na nilivipenda kweli mtunzi alikuwa Hamie Rajab, sikuwa naelewa maana yake ila sasa ndio naelewa.
 
Kweli mkuu. Hapo Karl Marx angetwambia ni 'ubidhaishaji wa elimu' au 'commodification of Education' kwa lugha ya Malkia. Kwa sasa uandishi ni kibidhaa zaidi na si kutoa huduma

nimekumbuka stori ya mipapai na mitete..tusiwe wabishi kama mipapai...tutavunjika
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom