Tujikumbushe vitabu vya zamani

Tujikumbushe vitabu vya zamani

hiki ndio kitabu bora Tanzania Hakijapata Kutokea Mpaka Leo ``HOFU`` kimeandikwa na A.E.MUSIBA muhusika mkuu katika kitabu hiki anaitwa WILLY GAMBA,kilichapishwa 1988 ni kizuri sana kwa wale wanaokijua na kama hauna naweza kukupa ukitoe copy ukakisome maana hakipatikaniki

Mkuu nipo Mwanza nina shida sana na kitabu hiki, nisaidie nakipataje?
 
dah nakumbuka darasa la la nne kitabu cha kiswahili enzi zile kuna stori moja tamu ya MANGASINI na MFALME, darasa la 3 kuna MUWA ULIOZAMISHA MELI, SAFARI YA MINJINGU, dah tumetoka mbali, la pili kulikua na PAMELA NA KIPINI, TOLA ALIA GIZANI
 
Naomba kama unacho cha HOFU cha jembe willy gamba naomba ndg nicheki kwa 0712905393 hii namba plz
 
Vitabu vyote mlivyotaja ni bongo fleva. Tafuteni hadithi ya UTOTOLE cha GW Mtendamema. Original Tanzania horror and drama story with a difference. Pia jaribuni FADHILI MSIRI WA NAUGUA
 
Polisi jamii plz njoo utusaidie kitabu hicho, tuwasiliane 0756444792
 
Mambo ya ajabu yaliyompata Allan Quterman na wenzake,,kuiendea nchi ya watu weupe.Bonge la kitabu japo kwa kiwango fulani kinamdhalilisha mwafrika
 
hiki ndio kitabu bora Tanzania Hakijapata Kutokea Mpaka Leo ``HOFU`` kimeandikwa na A.E.MUSIBA muhusika mkuu katika kitabu hiki anaitwa WILLY GAMBA,kilichapishwa 1988 ni kizuri sana kwa wale wanaokijua na kama hauna naweza kukupa ukitoe copy ukakisome maana hakipatikaniki

Ntakupataje mkuu nakihitaji sana ntakutoa kiume usijali
 
Dah umenikumbusha malikia Saraos na Nyleptha, msolopagazi wazuvendi. Sasa watoto ni magame tu

Mambo ya ajabu yaliyompata Allan Quterman na wenzake,,kuiendea nchi ya watu weupe.Bonge la kitabu japo kwa kiwango fulani kinamdhalilisha mwafrika
 
kuna kimoja cha kenya kuhusu mambo ya ujasusi...sikumbuki jina vizuri..NURU GIZANI,,,na kingine MAITI BILA KICHWA,,,,
 
Dah umenikumbusha malikia Saraos na Nyleptha, msolopagazi wazuvendi. Sasa watoto ni magame tu

machimbo ya mfalme suleiman and ALLAN QUATERMAN by H RIDDER HAGGARD ni zaidi ya burudani
 
NJAMA, HOFU, KUFA NA KUPONA! vya Musiba, muhusika mkuu Willy Gamba, Njama na bint Veronica Amadu yule binti wa Tanga au miss Tanzania. Yaani mmh!?
 
Dah umenikumbusha malikia Saraos na Nyleptha, msolopagazi wazuvendi. Sasa watoto ni magame tu

Solais bibi wa usiku alikuwa anapendwa sana na Sir Good wakati Henry alimpenda sana Nyleptha,.Unamkumbuka Mtoto Flosie pale mji wa mission?Vipi pale mtumbwi wao ulivyochukuliwa na mto wa chini ya ardhi?Unakumbuka kisa cha wale viboko?
 
NJAMA, HOFU, KUFA NA KUPONA! vya Musiba, muhusika mkuu Willy Gamba, Njama na bint Veronica Amadu yule binti wa Tanga au miss Tanzania. Yaani mmh!?

hicho cha HOFU ni kitabu kizuri sana mkuu nimepata kukijua miaka miwili iliyopita japokuwa cha kitambo sana lakini hadi leo bado nakisoma,huyu MUSIBA ni mtunzi bora ambaye hajapata kutokea hapa TANZANIA
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom